JERUSALEM 2006
JF-Expert Member
- Apr 23, 2012
- 527
- 596
Ndugu zangu mambo yanayoendelea huko bungeni kuhusu mahakama ya kadhi yanasikitisha sana. Inavyooelekea mahakama hiyo inaenda kukubalika kutokana na hoja zinazotolewa na ndugu zetu waislamu. Jambo hili linanitisha sana kwa sababu hakuna mtu anayepinga hoja hii, na kila mwakilishi wa kikristo akisimama anakwepa kabisa kuongelea jambo hili.
Mimi kama mwananchi wa kawaida kabisa, ninawatahadharisha kwamba iwapo mtajaribu kuweka jambo lolote linalohusu mahakama ya kadhi sisi WAKRISTO (CHRISTIANS) tutapiga kura ya hapana kwa katiba itakayopendekezwa. Nawahakikishia ndugu wajumbe wa bunge maalumu, hakuna mkristo atakaye iunga mkono katiba hiyo na haitopita.
Jambo hili tumelipigia kelele kwa muda mrefu kwamba mambo ya dini binafsi yaamuliwe na dini husika. Sasa wajumbe wanavyojitoa ufahamu na kusahu kwamba hii sio nchi ya kiislamu, waendelee kujadili dini yao na waipitishe, ila nina apa iwapo jambo la kadhi litakuwepo, basi ni kura ya hapana kwa wakristo wote.
Mwisho, naomba wajumbe wa BMK wajadili mambo ambayo hayaamshi hisia za kidini na wajikite kwenye hoja zinazogusa watu wote, wasipofanya hivyo na wakajisahau, basi wasije wakamlaumu mtu.
Mimi kama mwananchi wa kawaida kabisa, ninawatahadharisha kwamba iwapo mtajaribu kuweka jambo lolote linalohusu mahakama ya kadhi sisi WAKRISTO (CHRISTIANS) tutapiga kura ya hapana kwa katiba itakayopendekezwa. Nawahakikishia ndugu wajumbe wa bunge maalumu, hakuna mkristo atakaye iunga mkono katiba hiyo na haitopita.
Jambo hili tumelipigia kelele kwa muda mrefu kwamba mambo ya dini binafsi yaamuliwe na dini husika. Sasa wajumbe wanavyojitoa ufahamu na kusahu kwamba hii sio nchi ya kiislamu, waendelee kujadili dini yao na waipitishe, ila nina apa iwapo jambo la kadhi litakuwepo, basi ni kura ya hapana kwa wakristo wote.
Mwisho, naomba wajumbe wa BMK wajadili mambo ambayo hayaamshi hisia za kidini na wajikite kwenye hoja zinazogusa watu wote, wasipofanya hivyo na wakajisahau, basi wasije wakamlaumu mtu.