Katika safari yangu ya kufuta ujinga, nilikwenda nchi fulani kujifunza afya ya jamii. Tatizo kubwa katika jamii ile ilikuwa watu kuwa na uzito uliozidi. Katika kupigana na lile tatizo wakaangalia tabia za milo katika familia na mashuleni. Walikuja kugundua kuwa tofauti ya familia za kizungu na kiafrika ni kuwa mfano familia ya kizungu dinner: Familia ya watu wanne, packet ya mapaja manne ya kuku yamenunuliwa, yataokwa na viazi, sahani nne, kila sahani itapata kipande cha kuku, viazi na mboga, wamemaliza. Ukimaliza unaweza sindikizia na kibakuli cha ice cream au yoghurt.
Familia ya waafrika: familia ya watu wanne, wali utapikwa, mchuzi, mboga, mtoto ambae hajashiba anaenda kuongeza jikoni, chakula kikibaki mama anafurahi kuwa watoto wamekula mpaka wamesaza.
Hii ndiyo sababu kwa wazungu si rahisi kukaribishwa chakula kama hawana taarifa kuwa utakula nao. Haya mambo ya utandawazi yamenza kufanya baadhi ya waafrika kuacha mila zetu na kuthamini chakula. Heshima ya mwafrika ni mgeni wako ale chakula kwako, hata kama hakitoshi, mwenyeji atatoa portion yake kwa mgeni, ikibidi utakunywa chai na mkate au utapika uji mgeni akiondoka.