Kufutwa kwa POAC kuna siri nzito

mantegi

Member
Oct 16, 2012
27
20
Wana JF,

Napenda kujadili hii hoja ya kufutwa kwa kamati ya bunge ya hesabu za mashirika ya umma (POAC) kwa sababu mazingira ya kufutwa kwake yana utata pamoja na kamati ya ulinzi. Kufutwa kwa POAC kwa harakaharaka naona kama ni maandalizi ya EPA nyingine kuelekea 2015.

Nasema hivyo kwa sababu hii kamati imekuwa kamati muhiomu sana ndani ya bunge kwa kujadili matumizi ya pesa katika mashirika ya umma. kufutwa kwake kutatoa mwanya wa matumizi mabaya ya pesa za wananchi katika mashirika ya umma na kama imefutwa kwa makusudi na serikali taafsiri yake ni kuwa serikali inampango wa kufanya ufisadi katika mashirika ya umma na hii moja kwa moja ni mbinu teule kuelekea 2015.

Spika Anna Makinda wakati akifuta hii kamati alisema kazi hiyo itafanywa na PAC jambo ambalo aliyekuwa mwenyekiti wa poac, ZZK amepinga akisema PAC haitaweza kusimamia wizara za serikali na mikoa pamoja na mashirika ya umma kwani hata POAC yenyewe ilikuwa inashindwa kupitia taarifa za mashirika yote 258 ya umma kwa mwaka. Kwa maana hiyo hapa kinachoonekana ni kufanya PAC kushindwa kukagua hesabu hizo za mashirika ya umma hivyo kutoa mwanya wa kupiga EPA nyingine.

Kwa viongozi wapenda maendeleo POAC ingeboreshwa zaidi ili kupunguza matumizi mabaya ya pesa za umma.

Yangu macho ebu tusubiri tuone.

=============
Kuna uchambuzi mwingine umefanywa na Petro E. Mselewa hapa -> https://www.jamiiforums.com/great-t...ipi-kosa-la-zitto-na-kamati-yake-ya-poac.html unafaa kusomwa pia

=============

Napenda kuuliza swali hili ili kuweka kumbukumbu vizuri:

Hapo nyuma tuliambiwa kuwa POAC iligundua kuwa wakorea wako hatarini kufuta mkopo wao walioahidi kwa Tanzania uliokuwa utumike kujenga chuo kikuu cha afya Muhimbili katika ardhi yenye utata huko Mlongazila. Baadae tuliona michoro ya ujenzi wa chuo hiki ikitolewa kama mafanikio ya serikali ya CCM.

Kwa sasa sina uhakika ni fedha zipi zitatumika kujenga chuo hiki!

Walioibuwa hoja hii ya kupokonywa mkopo huu ni POAC chini ya Zitto na sasa tunaambiwa POAC imefutwa na Makinda.

Swali langu ni hili: Je, wakorea wameshaufuta huu mkopo wao? Kama ni hivyo nini kinaendelea?

Je, maazimio ya POAC yatatekelezwa au yatafutika kama ilivyofutika POAC?

ALIYELETA THREAD HII NI MUHITIMU WA FANI YA UDAKTARI MUHIMBILI!
 
Makinda uspika unamshinda,yeye anaongoza kiti emotionally,na hiyo sio sahihi,akigombana na mshikaji wake aliyemuweka kinyumba kule njombe,basi siku hiyo mbunge halikaliki maana hasira zote anazihamishia mbungeni.
 
Kuna siku Kuna uzi uulikuwepo hapa kwamba Spika ameitwa Ikulu nadhani ndo alikuwa anapewa maagizo, kazi ipo kwa kweli kwa namna hii mh!
 
Mnapokuwa mnauelimisha Umma basi tusaidieni kujua haya

POAC....................kirefu chake ni nini na utueleze kwa Kiswahili

PAC...................kirefu chake ni nini na kwa Kiswahili ni nini.

Kuna watu wanatuuliza wanasema POAC za Zittio iliyovunjwa ni Gari au Nyumba?
 
Mnapokuwa mnauelimisha Umma basi tusaidieni kujua haya

POAC....................kirefu chake ni nini na utueleze kwa Kiswahili

PAC...................kirefu chake ni nini na kwa Kiswahili ni nini.
Pole sana kaka
POAC-Parastatal Organizations Accounts Committee-Mashirika ya umma
PAC-Public accounts Committee-Serikali kuu n a idara zake
Njoo usome Government accounting utaelewa sana mambo ya bunge mzee
Kuna watu wanatuuliza wanasema POAC za Zittio iliyovunjwa ni Gari au Nyumba?
 
Mmewabana kwenye bomba la gesi wamekosa pesa za kampeni 2015 sasa wahaha popote penye mwanya lazima wapige pesa vinginevyo CCM watashindwa kununua wapiga kura na wasimamizi wa uchaguzi mwaka 2015.
 
Huyu bibi mpka ijekufika 2015 kama atafika basi atakuwa kasheligeuza ili bunge kituko maana kila aliambiwa fanya hivi nae ana kubali tu na tena ana msaidizi mwehu basi ndiyo balaa
 
Napenda kuuliza swali hili ili kuweka kumbukumbu vizuri:

Hapo nyuma tuliambiwa kuwa POAC iligundua kuwa wakorea wako hatarini kufuta mkopo wao walioahidi kwa Tanzania uliokuwa utumike kujenga chuo kikuu cha afya Muhimbili katika ardhi yenye utata huko Mlongazila. Baadae tuliona michoro ya ujenzi wa chuo hiki ikitolewa kama mafanikio ya serikali ya CCM.

Kwa sasa sina uhakika ni fedha zipi zitatumika kujenga chuo hiki!

Walioibuwa hoja hii ya kupokonywa mkopo huu ni POAC chini ya Zitto na sasa tunaambiwa POAC imefutwa na Makinda.

Swali langu ni hili: Je, wakorea wameshaufuta huu mkopo wao? Kama ni hivyo nini kinaendelea?

Je, maazimio ya POAC yatatekelezwa au yatafutika kama ilivyofutika POAC?

ALIYELETA THREAD HII NI MUHITIMU WA FANI YA UDAKTARI MUHIMBILI!
 
ningependa sana mheshimiwa Zitto aje kutoa ufafanuzi wa hili kwa cheo chake 'kilichofutwa' cha mwenyekiti wa POAC.mods mnaweza kumcontact zitto!

Haya ni baadhi ya mambo nyeti yaliyoibuliwa na kamati hii,kamwe hatuwezi kuyasahau kirahisi!
 
Last edited by a moderator:
Naamini kwamba huyu aliyemkubwa kuliko wote nchini ndiye huyo aliye nyuma ya kadhia yote katika nchi yetu.

Kuanzia kufutwa kwa kamati za bunge, AG kuleta bungeni sheria ya kumzima CAG na ripoti zake, Gesi ya mtwara kuja dar, ufisadi BOT, mikataba feki na TANESCO etc.

Hawa akina spika na Naibu wake, kwa maoni yangu, wao wanatumika tu
 
Kuna mengi nyuma ya pazia ngoja tusubiri

kama makinda alikurupuka kuifuta kamati hii basi ajue sisi wananchi tuna kumbukumbu muhimu za kazi iliyofanywa na POAC.kazi za kamati hii zilitugusa mno!
 
Yah mkuu mimi nilitegemea kuomba ajira kitakapofunguliwa japokuwa nina makalai mengie kwenye cheti changu. Si wanasemaga c yao ni A ya wengine?(nilikuwa nachukizwa sana na hizi kauli za kijinga)
 
Back
Top Bottom