Kufuatilia loss report polisi ni pasua kichwa. Jeshi la Polisi tunaomba mliangalie hili na mlifanyie kazi

KITAULO

JF-Expert Member
Apr 27, 2018
1,926
2,778
Wadau,

Jana asubuhi nikiwa njiani kwenye mwendo kasi nikiwa nakwenda kwenye mihangaiko yangu ya kila siku vijana wa mjini (wezi wa mifukoni) walinikwapulia simu yangu na vijisenti kiasi kadhaa. Nilistuka baada ya kusikia kijana wa pemebeni yangu alipokuwa analalama amekwapuliwa simu yake, na mimi kwa mstuko nikaanza kujipiga sachi ndipo nilipogundua na mimi ni muhanga pia.

Nilikwenda kwenye ofisi za mitandao yangu ya simu kuzifunga laini zangu kama ilivyo ada ili kuepuka matumizi mabaya wa wale mafedhuli walioniibia.

Changamoto ilianza pale nilipotakiwa kufuatilia loss report ili waweze kunirudishia line zangu (ofisi za haya makampuni zipo ndani ya jengo la J-MALL-Posta). Aisee hapo ndipo nilipoanza kuona namna gani kuna shida. Nilielekezwa kwenda kwenye stationary moja ya jirani ndani ya jengo hilohilo, nilipofika kwenye ile stationary kuulizia utaratibu na gharama, hapo niliambiwa gharama ni 4500/= kwa kila line, nikabaki na maswali mengi inakuwaje gharama inakuwa kubwa hivyo.

Nikaona hata hela imekuwa ngumu mno ngoja nisogee pale Police Central. Nikapewa maelekezo na Afisa mmoja pale nje, ila akaniambia zunguka kwa mbele kuna watu watakusaidia hapo nje. Kufika kwa wale vijana naambiwa gharama kwa line ni shilingi 3000/=

Kwa mimi niliyekuwa nimepoteza line zangu tatu gharama ilikuwa ina range kwenye 13500-10500

Hivi ni kweli tumefikia huku…na katika gharama zote serikali kupitia jeshi lapolisi linaingiza shilling 500/= kwa kila line hela iliyobaki inaishia kwenye mifuko ya watu wachache.

Wito wangu kwa jeshi la polisi naomba waliaangalie hili. Siyo haki kuwaumiza wanchi kwa maslahi binafsi ya watu wachache. Inakuwaje serikali inaingiza 500/= wakati mtu binafsi anajizolea kati ya 2500-4000/=?
 
KITAULO, Nchi hii sasa hv,watumishi wengi wa umma,ni majambazi,certified robbers,
Kuna wale wa TRA waliomba rushwa2M,waliponyimwa wakataifisha mzigo,na kutaka kumfilisi jamaa,uzuri mkulu,alizipata,sasa hv wananyea debe,
Kuna wale wa kawe,walioomba rushwa ya 200M,kesi inaendelea,
Watu wanataka mteremko,hawataki kutoa jasho.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nachojia mm lost report unapaswa kulipia Mia tano..Tena kupitia control number. Application ya lost report unafanya online, so ni bundle lako tu. Ingia link hapo Chini.
Nyumbani
 
Mtoa mada ni mzembe sana umeshindwa kudownload app ya polisi Tanzania inayopatikana playstore na kupata lose report kwa 500 tu au kuingia kwenye tovuti ya polisi na kufanya online ?
Mimi naona wamekuomba chache sana maana hii huduma kwa sasa ni rahisi mno huna haja ya kwenda polisi kabsa.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nahisi unalaumu jambo usilolijua.
Loss report ni 500
Unaingia katika webiste hii
Nyumbani
Unaandikisha majina yako, kitambulisho na vitu ulivopoteza.
Ukimaliza kama utakua umejaza kwa uhakika utapata control number kutoka kwenye hiyo hiyo website.
Utalipia 500 kwa kutumia mtandao wako wa simu “malipo ya serikali”
Ukimaliza hapa ndio unaweza kwenda kwenye ofisi ya mtandao wako wa simu wakupe barua, utaenda nayo polisi pamoja na zile control number, unaweza kuzinakili kwenye hiyo karatasi ya mtandao wako, polisi unaenda ku verify kua malipo yamepokelewa katika shirika la polisi.
Utarudi kwenye website hii Nyumbani
Uta print receipt kisha utaenda nayo kwenye mtandao wako wa simu ku renewe line.

Kwa haraka haraka
Loss report 500
Printing 1,000
Jumla 1,500

Kama hujui vijana wa mjini wanatumia mwanya huu kujiingizia kipato.
 
Mbona loss report ni online sasahivi? Ila tu utaonana na mhasibu wa kituo kwa ajili ya kukupa control number
 
Back
Top Bottom