Bususwa
JF-Expert Member
- Sep 30, 2021
- 429
- 1,011
Naandika uzi huu kwa huzuni kubwa sana.
Jana mnamo saa nne usiku,nilipigiwa simu na rafiki yangu, kwanza nilishituka, hii simu ya usiku hivi kwa yule jamaa, lazima kuna shida maana muda wa saa nne, yeye na familia yake hua wameshalala sio mtu wakukesha kuangalia mpira au kunywa pombe kama kina sisi!
Baada yakupokea ile simu,nilisikia sauti ya mke wake ikiwa yenye majonzi, kwikwi na huzuni, shemeji, ndugu yako amepata ajali, alikua anatoka hospital kumuangalia mfanyakazi mwenzake, baada yakutoka hospital alipita kwa dada yake kumusalimia pia nakumpa hongera kwa kupata mtoto!
Akili yangu iligonga haraka sana kwamba kaumia sana kiasi cha kwamba atapoteza baadhi ya viungo vyake? Au kafariki? Nikauliza yuko wapi? Mke wake akajibu tupo hospital hapa ila kavunjika mguu wakulia mara mbili, nikaenda pale hospital kutoa sapoti ya hapa na pale kuweza ndugu yetu apate matibabu! Hadi naandika hivi ni kwamba ndugu yetu, kafanyia upasuaji na kawekewa chuma kwenye paja.
Story iko hivi!
Sasa hivi kuna mtindo wa hovyo sana umejitokeza kwa vijana kuchinja pikipiki nakuzi pimp, kama wasemavyo wenyewe, pia wanatoa zile taa orginal za pikipiki nakuweka vile vitochi, sasa ndugu yangu alikua na usafiri wake wa pikipiki mida ya saa tatu anarudi kwake, akakutana na boda boda mwenye pikipiki amefunga kitochi, jamaa yangu alishituka tu yuko chini, hawezi hata nyanyua mguu, hii nikutokana nakugongwa na yule boda mwenye taa yakitochi.
Sasa basi jeshi la polisi usalama wa barabarani, mnasubiri nini kuzipiga marufuki hizi pikipiki? Kwanza wanaziiba huko wanakuja kuzichinja,na pikipiki inakua na muundo tofauti kabisa na chapa yake halisi, mfano TVS au Boxer inakua imebadilika kabisa!
Mbili hawa vijana wa boda boda, watakufa wengi sana, watauwa watu wengi sana,wataacha watu na vilema vyakudumu!
Ombi langu, wadau wenzangu hasa watumiaji wa hizi boda boda, ogopa sana mtu mwenye pikipiki yakitochi au kaichinja, hawa vijana watatumaliza tusipokua makini, they have nothing to loose, wengi hawana hata familia!
Tupaze sauti
Jana mnamo saa nne usiku,nilipigiwa simu na rafiki yangu, kwanza nilishituka, hii simu ya usiku hivi kwa yule jamaa, lazima kuna shida maana muda wa saa nne, yeye na familia yake hua wameshalala sio mtu wakukesha kuangalia mpira au kunywa pombe kama kina sisi!
Baada yakupokea ile simu,nilisikia sauti ya mke wake ikiwa yenye majonzi, kwikwi na huzuni, shemeji, ndugu yako amepata ajali, alikua anatoka hospital kumuangalia mfanyakazi mwenzake, baada yakutoka hospital alipita kwa dada yake kumusalimia pia nakumpa hongera kwa kupata mtoto!
Akili yangu iligonga haraka sana kwamba kaumia sana kiasi cha kwamba atapoteza baadhi ya viungo vyake? Au kafariki? Nikauliza yuko wapi? Mke wake akajibu tupo hospital hapa ila kavunjika mguu wakulia mara mbili, nikaenda pale hospital kutoa sapoti ya hapa na pale kuweza ndugu yetu apate matibabu! Hadi naandika hivi ni kwamba ndugu yetu, kafanyia upasuaji na kawekewa chuma kwenye paja.
Story iko hivi!
Sasa hivi kuna mtindo wa hovyo sana umejitokeza kwa vijana kuchinja pikipiki nakuzi pimp, kama wasemavyo wenyewe, pia wanatoa zile taa orginal za pikipiki nakuweka vile vitochi, sasa ndugu yangu alikua na usafiri wake wa pikipiki mida ya saa tatu anarudi kwake, akakutana na boda boda mwenye pikipiki amefunga kitochi, jamaa yangu alishituka tu yuko chini, hawezi hata nyanyua mguu, hii nikutokana nakugongwa na yule boda mwenye taa yakitochi.
Sasa basi jeshi la polisi usalama wa barabarani, mnasubiri nini kuzipiga marufuki hizi pikipiki? Kwanza wanaziiba huko wanakuja kuzichinja,na pikipiki inakua na muundo tofauti kabisa na chapa yake halisi, mfano TVS au Boxer inakua imebadilika kabisa!
Mbili hawa vijana wa boda boda, watakufa wengi sana, watauwa watu wengi sana,wataacha watu na vilema vyakudumu!
Ombi langu, wadau wenzangu hasa watumiaji wa hizi boda boda, ogopa sana mtu mwenye pikipiki yakitochi au kaichinja, hawa vijana watatumaliza tusipokua makini, they have nothing to loose, wengi hawana hata familia!
Tupaze sauti