Etwege
JF-Expert Member
- Jul 4, 2018
- 5,755
- 15,238
Spika wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania mh Job Ndugai wakati akihojiwa na kituo cha luninga kuhusu wabunge wa Chadema kukataa kuingia bungeni kwa madai ya kukwepa Corona amemshukia kama mwewe Freeman Mbowe!
Spika Ndugai amesema Freeman Mbowe kwa muda mrefu amekuwa na tabia za udikteta na hataki kubadilika hata baada ya chama chake kuwa kikubwa.! Spika ameenda mbali zaidi kwa kusema bunge lote ni timu moja na lina uongozi wake lakini Mbowe amechukua uamzi wa kuwatoa wabunge wa Chadema pekee bila kumshirikisha wala kujadiliana na mtu yeyote!
Amesema tabia hizi za ubabe na kuweka upinzani kwenye kila kitu ndiyo zinazopelekea wabunge na madiwani wengi wa chadema kuhama chama hicho. Mbowe anatakiwa ajue Corona ni janga na haijulikani litaishi lini hapa duniani .
Kwa upande wa wabunge waliobaki, Ndugai amesema wataendelea kuchapa kazi kama kawaida na kuwapitishia bajeti wananchi huku akisema kama bunge litaacha kupitisha bajeti na kuiacha serikali ianze kutumia hela bila kuidhinishwa na bunge ni Mbowe huyo huyo tena atakuja kulalamika kwamba serikali inatumia hela bila idhini ya bunge.!
Sent using Jamii Forums mobile app
Spika Ndugai amesema Freeman Mbowe kwa muda mrefu amekuwa na tabia za udikteta na hataki kubadilika hata baada ya chama chake kuwa kikubwa.! Spika ameenda mbali zaidi kwa kusema bunge lote ni timu moja na lina uongozi wake lakini Mbowe amechukua uamzi wa kuwatoa wabunge wa Chadema pekee bila kumshirikisha wala kujadiliana na mtu yeyote!
Amesema tabia hizi za ubabe na kuweka upinzani kwenye kila kitu ndiyo zinazopelekea wabunge na madiwani wengi wa chadema kuhama chama hicho. Mbowe anatakiwa ajue Corona ni janga na haijulikani litaishi lini hapa duniani .
Kwa upande wa wabunge waliobaki, Ndugai amesema wataendelea kuchapa kazi kama kawaida na kuwapitishia bajeti wananchi huku akisema kama bunge litaacha kupitisha bajeti na kuiacha serikali ianze kutumia hela bila kuidhinishwa na bunge ni Mbowe huyo huyo tena atakuja kulalamika kwamba serikali inatumia hela bila idhini ya bunge.!
Sent using Jamii Forums mobile app