Kufuatia Umuhimu wa Ripoti ya CAG, Je, Wajua Rais Wetu Anaamrishwa With Ultimatum?. Ikipita, Rais Anapuuzwa?.

Mkuu Kaka Wakudadavua, mimi sijengi hofu yoyote bali nafafanua kile mtunga katiba alichodhamiria, wakati Bunge lilipopitisha Azimio batili kuwa halitafanya kazi na CAG Prof. Assad, na Spika kufafanua kuwa Prof. Assad tuu as person lakini sio ofisi yake, na kutaka ripoti hiyo isainiwe na mtu mwingine ndipo ipokelewe, naamini kabisa Bunge letu na wabunge wetu, hawakujua Ripoti ya CAG ina hadhi gani, huwezi kumtenganisha CAG na Prof. Assad, Ripoti ya CAG bila saini ya CAG sio ripoti ya CAG.

Amini usiamini, mabandiko kama haya yanasaidia sana taifa letu, Bunge letu na serikali yetu, maana kuna vitu tunavisema humu, hata wenyewe walikuwa hawavijui, mfano mzuri ni angalia tarehe ya bandiko hili,
https://www.jamiiforums.com/threads...ccm-2015-could-be-john-pombe-magufuli.707165/
wakati huo hata Magufuli mwenyewe alikuwa hajui lakini watu humu tulijua.

Hivyo usikute hata Bunge wakati linatoa azimio hilo batili, hawakujua kuwa Bunge kufanyakazi na CAG sio a matter of choice ni utekelezaji wa amri za katiba. Spika aliposema hawapokei Ripoti ya CAG kama ina saini ya CAG Prof. Assad, ila ikisainiwa na mtu mwingine itapokelewa, hakujua kuwa Ripoti ya CAG bila saini ya CAG sio Ripoti ya CAG, na aliposema hawaipokea, alidhani Bunge lina optiion ya kuchagua kuipokea au kuikataa Ripoti ya CAG, katiba imeamrisha ripoti hiyo ipokelewe bila options, kama rais tuu anapuuzwa, ripoti inakuja Bungeni, who is Speaker asiipokee?.
Najua hofu kubwa kwa wengi ni kutojua kuwa Bunge likiikataa Ripoti ya CAG yenye sahihi ya CAG Prof. Assad, Katiba inamuelekeza rais kulivunja Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 90 (c).

Nakuomba sana Kaka yangu Wakudadavua, hapa ninafafanua tuu matakwa ya kikatiba, hivyo usiwe na hofu, hata Bunge likivunjwa, likiundwa tena, viti maalum vitaendelea kuwepo, hivyo wale wabunge wa viti maalum, waliohudumu vizuri kwenye nafasi zao za viti maalum na kutoa huduma maalum za viti hivyo maalum, watateuliwa tena kuendelea kuhudumu vitu maalum na kutoa huduma maalum za viti maalum kwa Bunge letu na Watanzania kwa ujumla.

P.
Ah ah ah brother ,you are a GENIUS.
Thank you kwa ufafanuzi mzuri.
Countdown is on.

Sent using Brain
 
Niliposoma tu kuwa "...Raisi yupo chini ya katiba..." nikaishia hapo, sikuona sababu ya kuendelea kwa sababu umeshindwa kuelewa pointi kubwa na ambayo ndiyo ya muhimu zaidi. Raisi wa Tz yuko juu ya sheria, sheria ikiwemo katiba, hiyo katiba ndiyo iliyompa ukuu pale iliposema kuwa hatashtakiwa kwa chochote atakachofanya kwenye madaraka yake, akiwa raisi au baada ya uraisi.

Hiyo hapo juu ndio mzizi wa fitina, kwa maana anaweza kufanya lolote ikiwemo kutoifuata, kuivunja na kuisigina kabisa hiyo katiba, hakuna mtu, bunge wala mahakama inaweza kumfanya lolote!
mkuu pascal ufafanuzi hapa kidogo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba tu nikusaidie,

Anaposema rais yupo chini ya katiba na sheria anamaanisha ni sheria na katiba ndizo zimemuumba mtu anaitwa Rais! Nje ya hapo asingekuwepo!
tukirudi kwenye maswali tatanishi ,je raisi asipowasilisha bungeni na CAG akaipeleka bungeni ikakataliwa kupokelewa je hapo hawajavunja katiba ?

kama wamevunja je hukumu yao ni ipi?


kama hawatachukuliwa hatua nikisema wapo juu ya sheria na katiba nitakua nimekosea??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Pascal Mayalla, let's say, Rais amegoma kuiwasilisha ripoti ya CAG Bungeni then CAG akaamua kum-bypass na kuiwasilisha yeye kama Katiba inavyomwagiza lakini Bunge likaamua kutoipokea (maana limeshaazimia kutofanya naye kazi) then what next? Ufafanuzi tafadhali.
Mkuu Dudus, kwenye issue ya Ripoti ya CAG, Katiba haikutoa option kwa Bunge kukataa kuipokea, Bunge ni lazima liipokee na kuiwasilisha mezani as must, lisipofanya hivyo, linatakiwa kuvunjwa.

Kuna vitu Katiba inampa rais wetu options, na kuna vitu hana options, kuvunjwa kwa Bunge kumezungumzwa katika ibara ya 90 na sio jambo la options, kwa sababu Bunge kuikataa Ripoti ya CAG ni kosa la insubordination kwa rais wa JMT, hukumu ya insubordination ni summary dismissal.
https://www.jamiiforums.com/threads...bunge-linavunjwa-kwa-mujibu-wa-katiba.1569237
P.
 
Sitakataa wala kukubali hoja yako - lkn tukumbuke tu kwamba nchi zinazoendelea utekelezaji wa katiba ni more theoretical na more fallacy katika practical
Mkuu Mkafriend, nakubaliana na wewe kwenye katiba kuna facts na fallacies, mfano ile principal ya usawawa mihimili na the doctrine of separation of powers, checks and balance, zipo kwenye maandishi tuu lakini in reality hakuna kitu kama hicho na hili nimewahi kulizungumza
https://www.jamiiforums.com/threads...aration-of-powers-nothing-just-a-myth.764217/
P.
 
ficha huu ujinga kwa wenye hekima. katiba ndio imetoa mgawanyo wa madaraka na mamlaka kwa mihimili ya dola, inakuwaje kiongozi wa muhimili mmoja akawa juu ya kiongozi mwingine kikatiba?

licha ya kwamba mimi si mwanasheria na wala sijawahi isoma sheria, lakini naweza kutofautisha kati ya katiba na sheria , na pia nafahamu katiba ni zaidi ya sheria ilhali sheria ndio zinatafsiri katiba.

Rais wa JMT hana mamlaka hayo uliyoyasema hapa ila ana mamlaka yote ya kutumia mamlaka yake kikatiba
Unachosema kiko kwenye makaratasi tu but reality is vicevercer

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Dudus, kwenye issue ya Ripoti ya CAG, Katiba haikutoa option kwa Bunge kukataa kuipokea, Bunge ni lazima liipokee na kuiwasilisha mezani as must, lisipofanya hivyo, linatakiwa kuvunjwa.

Kuna vitu Katiba inampa rais wetu options, na kuna vitu hana options, kuvunjwa kwa Bunge kumezungumzwa katika ibara ya 90 na sio jambo la options, kwa sababu Bunge kuikataa Ripoti ya CAG ni kosa la insubordination kwa rais wa JMT, hukumu ya insubordination ni summary dismissal.
https://www.jamiiforums.com/threads...bunge-linavunjwa-kwa-mujibu-wa-katiba.1569237
P.
... nimekuelewa sana Mkuu ila kumbuka Bunge limeshaazimia kutofanya kazi na CAG. Iko hivi, nakubali kwamba Rais anaelekezwa na Katiba kuiwasilisha ripoti ya CAG Bungeni; hata hivyo ikijulikana kuna uwezekano wa Rais kugoma kufanya hivyo, ndiposa Katiba inatoa option ya pili - CAG am-bypass Rais na kuiwasilisha mwenyewe. Hili lingewezakana endapo kungekuwa na mahusiano mabaya kati ya Rais na Bunge na hapo hapo mahusiano mazuri kati ya Bunge na CAG; tatizo kiuhalisia haiko hivyo - mahusiano kati ya CAG na Bunge sio mazuri kivile kwa kuzingatia msuguano wa hivi karibuni kati ya pande mbili hizo.

Hali iliyopo ni as if Rais ana mahusiano mazuri sana na Bunge wakati huo huo CAG anaonekana kutokubalika na pande mbili hizo. Je, pande mbili hizo (Rais/Bunge) zikiamua ku-collude ili kumhujumu CAG, kwa mfano, itakuwaje? Hapa Katiba imeacha mwanya kidogo! Ilitakiwa iende hatua moja mbele kwamba ikitokea hivyo, basi CAG awe na mamlaka ya kuifanya ripoti yake kuwa Public Document bila kutegemea "hisani" ya Bunge.
 
Dunia inatucheka aisee, lakini nyie mnaolinda nchi hii na mnalipwa kwa haya msilipolichukua kwa tahadhari hili la kuvunjwa katiba mnakuja angamiza taifa hili ni wakati wa magufuli na ndugai kuambiwa ukweli uoga na ukimya wenu ni angamizo la mikono yenu
Mkuu BAFA, dunia haitucheki, bali inatushangaa!, kisa neno "Udhaifu" kudhaniwa "dhaifu", hivyo Bunge sasa linaonyeshea sio dhaifu.
P
 
Nimekuelewa mkuu, tatizo wenye nafasi zao hawazitumii kumwambia bosi wao ukweli. Mkapa alitamka mara moja tu kuwa serikali ni ya CCM na ukawa mwisho wa mtu kusema serikali yake!
Mara nyingi tunasikia na kuona mtu akisema nimetoa bilioni kadhaa kufanya hili au lile, mfano bilioni 200 kulipa madeni, bilioni 10 kujenga sijui nini, ngapi kununua korosho nk. nk.
wale wanaosimamia bajeti hawasemi mzee, hiyo ni kazi yetu sema bunge limetenga kiasi hiki kufanya hiki au kile badala yake wanashangilia. Yule mkaguzi aligudua hilo akalisemea kwa kutumia neno lililowaudhi. wakachagua upande wa mamlaka dhidi ya uhalisia ikatolewa adhabu tata kwa kutumia kamusi sanifu.
Ni rahisi sana kama Mkapa alivyofanya kusema tu Bunge limeidhinisha/ halijaidhinisha,
so, Pascal hii inageuza utawala wa sheria kuwa utawala wa kimamlaka, mwenye mamlaka ndiye aliye sahihi sheria na katiba si chaguo letu! Na wananchi wengi mitaani tunafurahia mfano barabara za lami kariako kugeuzwa meza za wamachinga mradi mkono uende kinywani. Power matters mzee!
 
This is a Katibalessness if not lawlessness country, hivyo lolote linaweza kufanywa na wenye madaraka! msijisumbue na maandiko yoyote. Asipofanya mtamfanya nini? Bunge ni la kwake, kuna wa kuepeleka motion ya impeachment? 89% ni CCM, itapita na wote wanamuogopa? Shithole country ni yetu kweli kweli!
Mkuu Retired, nchi yetu sii katibaless wala hatuna lawlessness, kwa sababu tuna Katiba na Tanzania ni nchi inayofuata Katiba na utawala wa sheria.
Kuitukana nchi yako shithole ni kukosa uzalendo.
P.
 
tukirudi kwenye maswali tatanishi ,je raisi asipowasilisha bungeni na CAG akaipeleka bungeni ikakataliwa kupokelewa je hapo hawajavunja katiba ?

kama wamevunja je hukumu yao ni ipi?


kama hawatachukuliwa hatua nikisema wapo juu ya sheria na katiba nitakua nimekosea??

Sent using Jamii Forums mobile app
... exactly, hili ndio limekuwa swali tangu mwanzoni mwa thread hii! Rais hataki kuipeleka Bungeni na Bunge halitaki kuipokea moja kwa moja kutoka kwa CAG; CAG ana options zipi ikitokea hivyo? Tuko pamoja Mkuu.
 
At least wewe umeamua kuwa mkweli, hii nchi ni takataka tu.
Inaongozwa kwa utashi tu wa rais anaekuwa madarakani wala halazimiki kufuata hicho kikaratasi kinachoitwa katiba. Na hakuna wa kumfanya chochote.
Hata akitaka kuhamishia hazina nyumbani kwake, hakuna wa kumzuia wala kumuuliza.
Kuitukana nchi yako takataka ni kukosa uzalendo.
P
 
Nadhani ni wakati sasa Bunge liwe linampata Spika kwa kigezo cha uwezo kitaaluma na utashi. Sio kwa akili za iyena iyena.

Bunge letu limepwaya sana kwa sababu ya aina ya uongozi lililo nao, This is the hard fact.
Umepitia CV za viongozi wa bunge?

Ndugai, Tulia na Chenge?
 
Niliposoma tu kuwa "...Raisi yupo chini ya katiba..." nikaishia hapo, sikuona sababu ya kuendelea kwa sababu umeshindwa kuelewa pointi kubwa na ambayo ndiyo ya muhimu zaidi. Raisi wa Tz yuko juu ya sheria, sheria ikiwemo katiba, hiyo katiba ndiyo iliyompa ukuu pale iliposema kuwa hatashtakiwa kwa chochote atakachofanya kwenye madaraka yake, akiwa raisi au baada ya uraisi.

Hiyo hapo juu ndio mzizi wa fitina, kwa maana anaweza kufanya lolote ikiwemo kutoifuata, kuivunja na kuisigina kabisa hiyo katiba, hakuna mtu, bunge wala mahakama inaweza kumfanya lolote!
Sii kweli kuwa rais wa Tanzania yuko juu ya Katiba, ndio maana katiba imeweka Ibara ya 46 A
Bunge laweza kumshtaki Rais Sheria ya 1992 Na.20 ib.8 Sheria ya 1995 Na.12 ib.4
46A.-(1) Bila ya kujali masharti ya ibara ya 46 ya Katiba hii, Bunge linaweza kupitisha azimio la kumuondoa Rais madarakani endapo itatolewa hoja ya kumshtaki Rais na ikapitishwa kwa mujibu wa masharti ya ibara hii. (2) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya ibara hii, hoja yoyote ya kumshtaki Rais haitatolewa isipokuwa tu kama inadaiwa kwamba Rais-
Sheria ya …. (a) ametenda vitendo ambavyo kwa jumla vinaivunja Katiba au Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma; (b) ametenda vitendo ambavyo vinakiuka maadili yanayohusu uandikishwaji wa vyama vya siasa yaliyotajwa katika ibara ya 20(2) ya Katiba, au
(c) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano, na haitatolewa hoja ya namna hiyo ndani ya miezi kumi na miwili tangu hoja kama hiyo ilipotolewa na ikakataliwa na Bunge.
(3) Bunge halitapitisha hoja ya kumshtaki Rais isipokuwa tu kama- (a) taarifa ya maandishi, iliyotiwa sahihi na kuungwa mkono na Wabunge wasiopungua asilimia ishirini ya Wabunge wote itawasilishwa kwa Spika siku thelathini kabla ya kikao ambapo hoja hiyo inakusudiwa kutolewa Bungeni, ikifafanua makosa aliyoyatenda Rais, na ikipendekezwa kuwa Kamati Maalum ya Uchunguzi iundwe ili ichunguze mashataka yaliyowasilishwa dhidi ya Rais; (b) wakati wowote baada ya Spika kupokea taarifa iliyotiwa sahihi na Wabunge na kujiridhisha kuwa masharti ya Katiba kwa ajili ya kuleta hoja yametimizwa, Spika atamruhusu mtoa hoja kuiwasilisha hoja hiyo, na kisha Spika atalitaka Bunge, bila ya kufanya majadiliano, lipige kura juu ya hoja ya kuunda Kamati Maalum ya Uchunguzi na kama ikiungwa mkono na Wabunge waiopungua theluthi mbili ya Wabunge wote atatangaza majina ya wajumbe wa Kamati Maalum ya Uchunguzi. (4) Kamati Maalum ya Uchunguzi, kwa madhumuni ya ibara hii, itakuwa na wajumbe wafuatao, yaani- (a) Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, ambaye atakuwa ndiye Mwenyekiti wa Kamati; (b) Jaji Mkuu wa Tanzania Zanzibar na
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania _________________________________________________________________
38

(c) Wajumbe saba walioteuliwa na Spika kwa mujibu wa Kanuni za Bunge na kwa kuzingatia uwiano wa uwakilishi baina ya vyama vya siasa vinavyowakilishwa Bungeni. (5) Endapo Bunge litapitisha hoja ya kuunda Kamati Maalum ya Uchunguzi, Rais atahesabiwa kuwa hayupo kazini, kisha kazi na madaraka ya Rais yatatekelezwa kwa mujibu wa masharti ya ibara ya 37(3) ya Katiba hii hadi Spika atakapomfahamisha Rais juu ya azimio la Bunge kuhusiana na mashataka yaliyotolewa dhidi yake.
(6) Ndani ya siku saba baada ya Kamati Maalum ya Uchuguzi kuundwa, itakaa ichunguze na kuchambua mashataka dhidi ya Rais, pamoja na kumpatia Rais fursa ya kujieleza, kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Kanuni za Bunge. (7) Mapema iwezekanavyo, na kwa vyovyote vile katika muda usiozidi siku tisini, Kamati Maalum ya Uchunguzi itatoa taarifa yake kwa Spika. (8) Baada ya Spika kupokea taarifa ya Kamati Maalum ya Uchunguzi, taarifa hiyo itawasilishwa Bungeni kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Kanuni za Bunge.
(9) Baada ya taarifa ya Kamati Maalum ya Uchunguzi kuwasilishwa kwa mujibu wa ibara ndogo ya (8), Bunge litaijadili taarifa hiyo na litampa Rais fursa ya kujieleza, na kisha, kwa kura za Wabunge wasiopungua theluthi mbili ya Wabunge wote, Bunge litapitisha azimio ama kuwa mashtaka dhidi ya Rais yamethibitika, na kwamba hastahili kuendelea kushika kiti cha Rais, au kuwa mashtaka hayo hayakuthibitika. (10) Endapo Bunge litapitisha azimio kuwa mashtaka dhidi ya Rais yamethibitika na kwamba hastahili kuendelea kushika kiti cha Rais, Spika atawafahamisha Rais na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi juu ya azimio la Bunge, na hapo Rais atawajibika kujiuzulu kabla ya kuisha kwa siku ya tatu tangu Bunge lilipopitisha azimio hilo.

(11) Endapo Rais ataacha kushika kiti cha Rais kutokana na mashataka dhidi yake kuthibitika, hatakuwa na haki ya kupata malipo yoyote ya pensheni wala kupata haki au nafuu nyinginezo alizo nazo kwa mujibu wa Katiba au Sheria yoyote iliyotungwa na Bunge
P
 
Back
Top Bottom