Kufeli kwa Serikali kuhamia Dodoma

Kufeli kwa Serikali kuhamia Dodoma

Bonds la ufa! Japani kuna matetemeko mengi sana kuliko Dodoma, hata hivyo Japani inamajengo marefu kuliko yaliyopo Tanzania.
Ukame, pamoja na ukame lakini mji wa Dodoma hauna tofauti na Dar!
Mzunguuko wa pesa, makao makuu ya serikali si mji wa kibiashara, wengi wanadhani ndiko biashara zote zitakakofanyika, mji wa biashara utabaki kuwa Dar.
Makao makuu ya CCM, hili kwa sasa halina uhusiano na makao makuu ya serikali, vyama vyote vikohuru kujenga Dodoma.
Tatizo watu hawajapenda Dodoma kupewa hadhi yake,wanataka kila kitu kiwe Dar kwa kigezo cha bahari na starehe nyinginezo.Mungu akipenda inawezekana Dodoma ikawa chanzo cha mafanikio ya mikoa ambayo iliachwa na wakoloni pasipo maendeleo yoyote
 
Wakuu zipo sababu kibao ambazo tukizitaja zinaweza kuwa mwiba mchungu sana lakini itabidi tuzitaje ili kuuboresha mji wa Dodoma ambao umepewa hadhi ya jiji ikiwa kimuonekano baado sana

1. Geografia ya mji wa Dodoma
Mkoa huu ni miongoni mwa mikoa mikame na yenye asili ya jangwa kwa maana hauna mvua za kutosha ikiwa wastani wa mvua zake ni miezi mitatu au minne kasoro. Hivyo uoto wa asili muda wote ni ukame. Najiuliza sana serikali yetu imetenga bajeti kuwekeza katika eneo lenye ukame na kulifanya liwe la kuvutia au wamekurupuka tu.

Tukiangalia miji ya Dubai, Misri yenye hali kama hii ya ukame wametumia gharama kubwa kufanya miji ipendeze.pia ukiacha ukame kuna bonde la ufa limepita pale ambalo kitaalamu linakufanya usijenge majengo marefu kwenda juu.

2. Mzunguko wa pesa
Kwa sasa mkoa huu umekuwa na mzunguko wa pesa kwakuwa kuna uuzwaji mkubwa wa viwanja lakini baada ya hapo sidhani kama kutakuja kuwa na mzunguko wa pesa. Pia uwekezaji unaofanyika hauendani na ungezeko la watu.

Yaani unajenga majengo ya gharama mbali na miji ya watu halafu watu waje wajae kama maji ya bahari ni kitu kigumu sana.

Hii itatokea kwa miaka ya mbele kama 40 au zaidi. Kinachofanyika sasa ni kuharibu pesa za walipa kodi ambazo kurudi kwake itatugharimu miaka mingi.

3. Ni mji wa kisiasa (Makao makuu ya CCM)
Kwa mitazamo ya kawaida tunajua huu mji Nyerere na serikali waliufanya uwe makao makuu ya Chama cha Mapinduzi. Kimsingi sio wazo baya ila Nyerere mwenyewe alishtuka kuufanya katika kuufanyia maendeleo kwa kuwa kisiasa watu watajitambua na CCM itapoteza taswira. Serikali hii imevunja kanuni ya huu mji haukutakiwa kuendelezwa ili CCM itawale.

Yapo mengi ya kuelezea kwangu mimi. Wadau kama mnayo kuhusiana na mji huu mnaweza kutiririka.
Una matatizo.
Fika dodoma uone mji unavyo shamiri.
 
Wakati Nyerere alipoamua Dodoma iwe makao makuu ya nchi sababu kuu zilikuwa za kiusalama kwani nchi yetu ilikuwa kinara wa kusaidia ukombozi barani Afrika. So maadui wakubwa, makaburu that time walikuwa tishio sana kuushambulia, from Dar. Sababu hizo kwa sasa hazipo, kwani sasa hivi watu wanaangalia zaidi economic reasons lakini pia na mazingira mazuri ya investment. Nimesikia rais akigusia kwamba Dodoma sasa ndiyo makao makuu na hata akimaliza muda wake hakuna kurudi Dar. Hii kauli inaashiria wasiwasi uliopo kwamba maamuzi haya one day yanaweza kuwa reversed....


Aisee sasa kipi ni kipi maana mengi yanasemwa kuhusu Makao Makuu Dodoma.
 
Mzee lengo la wazee wa CCM ilikuwa ni kuweka makao makuu katikati ya nchi na si vinginevyo! Na Nyerere aliwakamatia kigezo cha usalama.

Dar Es Salaam ni kamji kadogo sana kama serikali ingeendelea kuwepo huko miaka 20 ijayo unadhani patakuwaje? Hivi tu kuna watu 5 million mmebanana vibaya mno.

Dodoma ni sehemu poa ila tu ina mapungufu makubwa ambayo yatafanya mji uwe mzuri kupita Dar Es Salaam na moja ya pungufu kubwa umeliainisha ni mvua.

Nilipasema Singida, pale ndio katikati kabisa sasa mwa Tanzania pia CCM ndo nyumba yake ya pili baada ya Dodoma Singida kuna vile viziwa angalau kungevutia na mawe mawe yale kama Rock city japokuwa Singida nayo ni semidesert ila ina kaunafuu!

Pengine haikuchaguliwa huenda miaka hiyo palikuwa chaka sana
Naisapoti sana serikali kuondoka Dar kwakweli hapafai padogo mno
Udogo wa Dar siyo issue kwani wangepanga vizuri Kibaha, mpaka Mlandizi, pugu, mkuranga yote ingekuwa part ya Dar.
 
Una matatizo.
Fika dodoma uone mji unavyo shamiri.
Swali moja kwako mkuu nitajie vivutio vitatu tu vya kiuchumi ambavyo vilikuepo dodoma kabla ya serikali kutangaza kuhamia huko.na ikibidi uvitolee ufafanuzi katika ufanisi wake na je serikali imeviendelezaje?? Isije kua tuna anza halafu tunapongezana bila ya kuwa na saababu za msingi.
 
Udogo wa Dar siyo issue kwani wangepanga vizuri Kibaha, mpaka Mlandizi, pugu, mkuranga yote ingekuwa part ya Dar.
Yes ingekuwa ni wilaya hata tano kiuchumi ilikua na faida sana yaani ingekusanya mlandizi kibaha ni wilaya za jirani halafu makao makuu yawe morogoro ungeona mji unavyokua kwa kasi ; maghorofa unayoyaona posta yangefika mpaka chalinze tena kwa masta plan yakueleweka na fly over za kimkakati zingejengwa
 
Dodoma ndipo panastahili kuwa makao makuu,
1. Ni karibu kufikika kwa watu wa mikoa mbali mbali. Dodoma ina barabara kuu 4, watu kufata huduma ni rahisi kuliko Dar

2. kuondoa tatizo la "centralization" haiwesekani nchi kubwa hivi kila kitu kiwe Dar, kuanzia Elimu vyuo vingi kurundikana Dar, mahospitali makubwa yote Dar, Majengo Marefu yote Dar, viwanja vya mpira Dar, kila kitu Dar

3. kupunguza foleni, population Dar,

4. pakiwa mji mkuu kamili ,hivo vilivyopo Dar vitajengwa na Dodoma pia kutokana na mahitaji
NB😀odoma waiplan vizuri isiye kuwa kama miji yetu mingine
 
Anahamasisha wahamie Dodoma lakini yeye muda mwingi kama si wote yupo Dar. Hameni na wake zenu. Mnaopewa ubalozi mwende na wake zenu.
 
Nakubaliana na maamuzi ya kuhamishia makao makuu ya nchi kuwa Dodoma ila kitu ambacho hakijanifurahisha ni kuharakisha uamuzi na kutowahusisha wataalamu ktk maamuzi
Wangefanya kama UAE, Mfalme alichukua vijana 10 akawapeleka katika 5 Big Cities(2@ in every city) in the World kazi yao kubwa ni kufanya Observation kwa miaka 2 mtawalio jinsi gani miji hiyo inatunzwa na kuendeshwa na kupeleka report kwa Mfalme hatimae ndio hii miji tuionayo sasa
Mimi ni muumini mzuri wa kitu kinaitwa " simulation" yaani kama unaamua kuhamia Dodoma unajipangia a number of steps za kuhama kulingana na mahitaji ya kuhama, na hiki kitu kiliishaanza kufanyika tena hamuwezi kuamini Wizara ya Kwanza kuhamia Dodoma ilikuwa ni Wizara ya Maji chini ya Edward Lowassa nina hakika it was a good strategy Wizara ya Maji kuhamia kule na kuweka sawa Infrastructure za Maji toka Ziwa Victoria ambapo kungekuwa na malengo ya lets say miaka 15 ijayo ambapo kwa wakati ule hivi sasa ingeishafika miaka 15
Kulikuwa na Wizara nyingine iliyokuwa chini ya Mizengo Pinda nayo ilikwishahamia kule nayo ingefanya mambo yake then hivyo hivyo mpaka Wizara zote zinaisha
 
Labda wayavute ya Ziwa victoria toka tabora.itasaidia
Viwanda vya maji kama Kilimanjaro, Dasani nk wawekeze kwa wingi Dodoma maana maji yao mabalozi watanunua kwa wingi sio kwa akili ya kunywa tuu bali hata kuogea ili wasipauke kwa chumvi!
Hakika mzee wetu ni mbunifu wa kuendeleza viwanda, pongezi kwake!
 
Hama acha maneno maneno..najua unapo angalia ulichowekeza Dar roho inakuuma.
 
Swali moja kwako mkuu nitajie vivutio vitatu tu vya kiuchumi ambavyo vilikuepo dodoma kabla ya serikali kutangaza kuhamia huko.na ikibidi uvitolee ufafanuzi katika ufanisi wake na je serikali imeviendelezaje?? Isije kua tuna anza halafu tunapongezana bila ya kuwa na saababu za msingi.
Dodoma kuna mawe mengi sana.
Hiyo ni fursa ya kiuchumi!
 
ni mara yangu ya kwanza kukaa ddm angalau kwa wiki mbili sasa, ukweli bado safari ni ndefu sana sana kuifikisha ddm kwenye hadhi ya jiji, ddm bado mno
 
Back
Top Bottom