Kufanana na watu wengi hii imekaaje?

Me nafananishwa sana na watu wengi kisa ubanaji wa nywele hizi wanaita natural hair sijui.... Si na mm ninazo bhn.
Basi full kupata offer, sema naogopa nisije fananishwa na mke wa mtu bure ndy maana saizi nasuka sanaaa.
Emu picha yako nikuone.😂😂
 
Hello JF

Nimejikuta nalazimika kuleta uzi sasa maana hii imeanza kunishangaza.

Tangu nakuwa ni kawaida kukutana na watu then wananiambia nimefanana na either ndugu yao fulani au jamaa zao. Imefika hatua now nimekuwa wengine mpaka hunipiga picha. Wakawaonyeshe wahusika. Ikafika muda nikawa nahesabu na kunote mahali, mpaka sasa ni zaidi ya watu 15 ambao nishakutana nao kisha wakanifananisha na jamaa zao.

Ingawa binafsi kihalisi nishakutana na watu watatu ukitutazama ni kama mapacha au ndugu wa tumbo moja. Uzuri mwingine nilikuwa nimemtangulia kidato shule moja.

Kiukweli inashangaza sana.
Mkuu kawaida tu, kuna rafiki yangu tulikuwa tunasoma nae watu wengi hata darasani walijua sisi ni mapacha kabisa, kuna time watu wengine na walimu walikuwa wanashindwa kututofautisha. So ni kawaida japo kwa case yako kufananishwa na wengi kwangu haikuwa hivyo
 
Wakati mwingine ni ndugu bila wewe kujua!
Mimi Kuna mtu alinifananisha na mtu mwingine, nilipochimba na kufuatilia sana nikaona naye kumbe ni ndugu yangu Mtoto wa inje ya ndoa wa baba yangu mkubwa,
Msiwe mapotezea jaribuni kufuatilia Kwa karibu
Aisee
 
Mungu alitengeneza sample kadhaa za watu na kuzipiga copy . Kinachotofautiana unakuta ni rangi lakini morphology zipo zenye mfanano kutoka Mkoa mmoja hadi mwingine ,nchi Moja hadi nyingine na bara Moja hadi jingine
 
Hello JF

Nimejikuta nalazimika kuleta uzi sasa maana hii imeanza kunishangaza.

Tangu nakuwa ni kawaida kukutana na watu then wananiambia nimefanana na either ndugu yao fulani au jamaa zao. Imefika hatua now nimekuwa wengine mpaka hunipiga picha. Wakawaonyeshe wahusika. Ikafika muda nikawa nahesabu na kunote mahali, mpaka sasa ni zaidi ya watu 15 ambao nishakutana nao kisha wakanifananisha na jamaa zao.

Ingawa binafsi kihalisi nishakutana na watu watatu ukitutazama ni kama mapacha au ndugu wa tumbo moja. Uzuri mwingine nilikuwa nimemtangulia kidato shule moja.

Kiukweli inashangaza sana.
Niliwahi kuambiwa nafanana na mwimbaji wa Nai Nai
 
Back
Top Bottom