Kuepuka laana, tuweke tozo angalau ya Tsh. 20 kwa kila chupa ya maji ya kunywa kuwanusuru wenzetu wenye mahitaji maalum

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
1653917358575.png

1653917382629.png
1653917453673.png
unajua misaada ambayo nchi zilizoendelea hutoa kwa nchi maskini ni sehemu ya kodi ya raia wa nchi husika ambazo wanatozwa na serikali zao ili kusaidia maskini kwenye nchi nyingine?

Kwenye jamii yetu kuna watu wenye mahitaji maalum ikiwemo walemavu, Watoto mayatima, waliotelekezwa n.k ambapo watu hawa hawawezi kujinusuru wenyewe mpaka wasaidiwe.

Kwa sasa watu hawa huomba omba mtaani wakitegemea kupewa 200 kotoka kwa raia wachache wenye huruma, wengine wakiomba wakikosa huamua kugeuaka kuwa wezi.

Badala ya kuacha hali hii iwe itakavyokuwa, Ni muhimu tuweke Tozo angalau ya Tsh. 20 kwa Kila chupa ya maji ya kunywa, Fedha itakayopatika itumike kujenga safe house ambazo zina kila huduma (bure) kwa ajili ya makundi haya maalum huku wakifundishwa fani mbalimbali, wanaoweza kujitegemea wanaachwa wanaanza kujitegemea, wanaoshindwa wanalelewa hadi mwisho wa Maisha yao.

Watu hawa hawajapenda kuwa walemavu n.k hivyo ni sahihi na ubinadamu kutumia kodi ya raia wazima kusaidia wenye uhitaji maalum. Hili ni jambo muhimu kiuchumi, Kijamii, Kiusalama na ki ubinadamu. Tunganeni kupigania jambo hili kwa kuwa ni muhumu kwa Taifa na ustawi wa mwanadamu.
 
Kama ukishindwa kunywa maji ya chupa, utakunywa ya bomba. Ni bora wewe unywe maji ya kudownload wenye mahitaji maalum nao wapate chakula na kulala ndani, kuliko unywe ya chupa wakati wenye mahitaji maalum wanalala kwenye mitaro na kula majalalani.

Wakati tunajadili bajeti ya Ustawi wa Jamii na Makundi maalum, hili ni muhimu sana.
 
Siungi mkono hoja.
Kwa nini? fikiria wewe ndio ungezaliwa mlemavu, huna mikono wala miguu, halafu watu wazima wakatae kutoa angalau kodi ya Tsh 20 kutoka kwenye bidhaa isiyo ya lazima ili na wewe uweze kula na kulala ndani ya nyumba, ungewatafsirije binadamu?

Ukumbuke, wewe ni mzima lakini mafuta tu yalivyopanda bei ukataka serikali iingilie iweke ruzuku ili ununue huduma kwa urahisi, vipi wenzako wasiojiweza na hawana sauti?
 
Mkuu, usiogope, kila kitu kina changamoto zake ila jambo hili linawezekana kabisa, la msingi nia. Tena tukianza, matajiri wa ndani na nje watajitokeza na kuongezea hela mfuko utaimarika na wenzetu wenye mahitaji maalum nao wataishi kama binadamu. Hii itakuwa ni heri kwetu sote.
 
Halafu yakale mafisi yanayokula kodi za walala hoyi badala ya kujenga nchi.
Kuna watu hawazalishi umeme ila wanatumia kwa gharama nafuu kabisa kuliko wanaozalisha kwa mtindo huu wa mafiemu
 
Ili uelewe vizuri uzito wa hoja yangu, chukulia wewe ulikuwa fundi, umepata ajali umekatika mikono, ndugu wamekutosa unafanya nini?

Fikiria umefariki, umeacha watoto wadogo, watoto wametelekezwa na wana ndugu, halafu wawili ni miongoni mwa hao hapo pichani ,ungeitafsiri je dunia?

Lakini kama tunaweza kuweka tozo kwenye umeme kuweka umeme vijijini, tukaweka tozo kwenye simu kujenga shule, hili kwa nini litushinde?
 
Ni wazo zuri Ila hao watakaopewa shamans ya kuisimamia Hiyo tozo ya maskini,Wataziiba watanunulia V8 na KUJENGA magorofa yao kwanza.Mtoa mada Naomba utupe pia mbinu za kuisimamia hizi tozo za maji zisiibiw
Hakuna namna tunaweza kudhibiti wizi kwa 100% maana hata yale maharage na ugali wa wanafunzi wa boarding kuna watu wanaiba, lakini hatuwezi kusema wanafunzi wasile maana kuna watu wanaiba unga. Tutatengeneza utaratibu mzuri ili kupunguza wizi na kuongeza ufanisi kuhudumia makundi maalum.
 
Hii Kodi ya maskini itozwe kwenye vitu ambavyo Ni vya anasa za kupindukia.e.g.Pombe Kali,bia kutoka nje ya nchi,sugars n.k.SIO KWENYE BIDHAA MUHIMU YA MAJI YA KUNYWA YA CHUPA.
Maji ya kunywa ya chupa sio bidhaa ya muhimu kihivyo kwa kuwa kuna mbadala kwa asiye na uwezo wa kuyanunua. Tumekunywa maji ya visima kwa muda mrefu kabla ya maji ya chupa na haijawahi kuwa ishu. Uzuri wa maji ni bidhaa inayogusa watu wote, wacha Mungu na wahuni.

Wewe unataka jukumu hili tuwaachie walevi peke yao?
 
unajua misaada ambayo nchi zilizoendelea hutoa kwa nchi maskini ni sehemu ya kodi ya raia wa nchi husika ambazo wanatozwa na serikali zao ili kusaidia maskini kwenye nchi nyingine?

Kwenye jamii yetu kuna watu wenye mahitaji maalum ikiwemo walemavu, Watoto mayatima, waliotelekezwa n.k ambapo watu hawa hawawezi kujinusuru wenyewe mpaka wasaidiwe.

Kwa sasa watu hawa huomba omba mtaani wakitegemea kupewa 200 kotoka kwa raia wachache wenye huruma, wengine wakiomba wakikosa huamua kugeuaka kuwa wezi.

Badala ya kuacha hali hii iwe itakavyokuwa, Ni muhimu tuweke Tozo angalau ya Tsh. 20 kwa Kila chupa ya maji ya kunywa, Fedha itakayopatika itumike kujenga safe house ambazo zina kila huduma (bure) kwa ajili ya makundi haya maalum huku wakifundishwa fani mbalimbali, wanaoweza kujitegemea wanaachwa wanaanza kujitegemea, wanaoshindwa wanalelewa hadi mwisho wa Maisha yao.

Watu hawa hawajapenda kuwa walemavu n.k hivyo ni sahihi na ubinadamu kutumia kodi ya raia wazima kusaidia wenye uhitaji maalum. Hili ni jambo muhimu kiuchumi, Kijamii, Kiusalama na ki ubinadamu. Tunganeni kupigania jambo hili kwa kuwa ni muhumu kwa Taifa na ustawi wa mwanadamu.

Tatizo hizo tozo mtaziiba tu. Mwizi hawezi kuacha wizi
 
Kwa nini? fikiria wewe ndio ungezaliwa mlemavu, huna mikono wala miguu, halafu watu wazima wakatae kutoa angalau kodi ya Tsh 20 kutoka kwenye bidhaa isiyo ya lazima ili na wewe uweze kula na kulala ndani ya nyumba, ungewatafsirije binadamu?

Ukumbuke, wewe ni mzima lakini mafuta tu yalivyopanda bei ukataka serikali iingilie iweke ruzuku ili ununue huduma kwa urahisi, vipi wenzako wasiojiweza na hawana sauti?
Siungi mkono hoja, siyo kwa sababu siguswi na matatizo ya watu wengine! La hasha!! Tatizo ni kwa wale watao simamia hilo zoezi. Hao ndiyo watanufaika zaidi kuliko hao walemavu.

Na jambo hili halikubaliki hata kidogo. Halafu isitoshe hiyo tozo inaweza kusababisha viwanda vya maji kufa! Maana itafikia wakati baadhi ya watu wataanza kutembea na madumu ya maji wawapo katika mizunguko yao, ili kupunguza matumizi ya maji ya kununua.
 
Back
Top Bottom