Chupa za plastiki ziwe chanzo kipya cha tozo kwa Serikali bajeti ya mwaka 2023/2024

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,681
46,360
Mnaondaa bajeti ya serikali tazameni uchafuzi wa mazingira kama chanzo muhimu cha mapato kwa mwaka unaokuja wa fedha . Anzisheni tozo ya mazingira kwa wazalishaji bidhaa zinazofungashwa kwenye chupa na mifuko ya plastic. Mtapa pesa nyingi sana kwa mfano mkitoza shilingi 100 ya mazingira kwa kila chupa ya plastic kutoka kampuni kama MeTL, Azam, Sayona n.k

Kwa tozo hii mtapata mapato ambayo yanaweza kusaidia kuboresha mazingira ya miji ya nchi hii iliyo michafu sana kwa kuzagaa chupa za plastiki za maji ya kunywa na vifungashio vingine vya plastiki kama vya mikate, sabuni, pampas n.k

Kama iliwezekana kuanzisha tozo ya mshikamano kwa raia pia inawezakana kuanzishwa tozo ya mazingira ikiwalenga wazalishaji bidhaa.
 
Mnaondaa bajeti ya serikali tazameni uchafuzi wa mazingira kama chanzo muhimu cha mapato kwa mwaka unaokuja wa fedha . Anzisheni tozo ya mazingira kwa wazalishaji bidhaa zinazofungashwa kwenye chupa na mifuko ya plastic. Mtapa pesa nyingi sana kwa mfano mkitoza shilingi 100 ya mazingira kwa kila chupa ya plastic kutoka kampuni kama MeTL, Azam, Sayona n.k

Kwa tozo hii mtapata mapato ambayo yanaweza kusaidia kuboresha mazingira ya miji ya nchi hii iliyo michafu sana kwa kuzagaa chupa za plastiki za maji ya kunywa na vifungashio vingine vya plastiki kama vya mikate, sabuni, pampas n.k

Kama iliwezekana kuanzisha tozo ya mshikamano kwa raia pia inawezakana kuanzishwa tozo ya mazingira ikiwalenga wazalishaji bidhaa.
Sheria ndogo za Halmashauri za Usafi wa Mazingira kila siku zinatungwa na Halmashauri, zinapitishwa na Wizara na kuwekwa kwenye gazeti la serikali.

Mawakala wanawekwa mitaani na POS wanakusanya pesa, zinaingia kwenye FUKO LA HALMASHAURI zinaishia kulipa POSHO za Madiwani, Wakurugenzi na maboss wa Halmashauri.

USAFI siyo kipaumbele tena.

Kwahiyo, hata ikiwekwa TOZO YA TAKA kwenye wazalishaji zitafanya matumizi tofauti yasiyohusu taka. Na hapo ndipo tatizo kubwa lilipo.


Halmashauri zinaendeshwa na wapumbavu
 
Sio lazima aongeze mia moja yote, anaweza kuongeza sh 50 na yeye akalipia sh 50, na kwa sababu haya mapato yatakuwa kwa ajili ya kuboresha mazingira yetu wote ni sawa pia tukichangia wote kwa pamoja.
Hapo mzalishaji ataongeza shilingi mia moja kwenye bidhaa hivo mtumiaji wa mwisho ndio ataathirika, unafahamu stika za tra wananunua bei gani tuanzie hapo kwanza
 
Yaani hamjui gesi mnapata kiasi gani,mbuga milima yote na wanyama wahuni wakiamua wanawatia kwenye ndege ya mizigo hapo KIA na kuelekea kusikojulikana ninyi kutwa kuja na hoja ya Tozo mpya...badala ya kufikiri rasilimali zilizopo zinamsaidia vip Mtanzania pana shule hazina madawati ya kutosha ila mbao zinaenda Nje...
 
Inategemea aina ya bidhaa, kuna bidhaa ukiongeza sana bei mauzo yako yatapungua.
Watu watatafuta mbadala wake, hapa watu wanaweza kununua madumu makubwa ya maji na kuwa wanajimiminia kidogo kidogo kwende nayo kwenye mizunguko yao, wazalishaji wanaweza kujiongeza kwa maji ya kuwekwa kwenye chupa za glasi kama za bia maeneo ya Hotelini na Bar.
Viwanda haviumizwi na kodi yoyote au tozo yoyote ile anayeumia mtumiaji wa mwisho.

Mbona hizo chupa ni biashara watu wanazikusanya na kuziuza?
 
Huo mzigo watabebeshwa wanywaji wa maji, hapana, kodi wanazochukua zinatosha. Afterall, chupa hizo ni mali, ukitupa zinaokotwa hapo hapo kwenda kuuzwa, hivyo zinajiokota zenyewe na hakuna uchafuzi wowote.
 
Kwa rasilimali za Tanzania ilitakiwa kodi iwe chini sana kama mianya ya ufujaji na rushwa vingekua havipo, akipatikana msimamizi mzuri wa rasilimali na mbunifu wa kuongeza wigo wa mapato nakuhakikishia nchi itafika mbali sana
 
Suluisho sio kuweka tozo mana tozo itaturudia sisi walaji wala sio mfanyabiashara.
Jambo la kufanya ni kupiga marufuku makopo ya rangi kama Novida na Energy.
Mana ukiangalia walokota makopo wanalokota makopo yote isipokuwa haya yenye rangi hivyo serikali na wizara yake ipige marufuku kutumika kopo hizi..
 
Tozo ya plastic ni good idea lakini

1. Tozo iendane na wajibu wa serikali kuhakikisha inasimamia ipasavyo kutozagaa mitaani kwa chupa hizo. Sasa hivi hizo chupa zinaharibu mazingira sana.

2. Bei za vinywaji, hiyo tozo atakayekuja kuilipa eventually ni mtumiaji wa mwisho. Kwa hiyo fikiria vizuri kama hiyo tozo itaishia kumpunguzia ukali wa maisha mlaji
 
Sio zote mkuu makopo ya Energy wanayaacha pamoja na Novida.
Huo mzigo watabebeshwa wanywaji wa maji, hapana, kodi wanazochukua zinatosha. Afterall, chupa hizo ni mali, ukitupa zinaokotwa hapo hapo kwenda kuuzwa, hivyo zinajiokota zenyewe na hakuna uchafuzi wowote.
 
.mapato kwenye gesi
. VAT kwenye bidhaa mbalimbali
. Mbunga za wanyama
. Dhahabu
. Madini mengine
.vitalu vya uwindaji
.mbuga za wanyama
.ushuru wa mazao
. Ushuru wa bidhaa mbalimbali
. Ushuru na kodi kwenye mafuta na gesi
.ushuru wa kuingiza magari na vipuri vyake
.ushuru wa bidhaa kutoka nje ya nchi
.utalii wa fukwe za bahari ya hindi na fukwe za maziwa kama nyasa, victoria, tanganyika viboreshwe na kutangazwa
.kodi ya ardhi na kodi ya majengo
.mapato vyuo mbalimbali vya serikali
.mapato kwenye hsopital zetu ambapo huduma dhaifu malipo makubwa
.mapato ya ATCL
.mapato ya meli zetu
.mapato yatokanayo na uvuvi
.mapato ya stendi zote za mabasi
.mapato ya miamala ya uhamishaji fedha kwa simu na njia ya benki
.mapato yatokanayo na kodi kwa watumishi wa umma
.mapato na faida kutoka kwenye bima mbalimbali za afya, majengo, na kadhalika
.mapato ya bia na vinywaji mbalimbali
.mapato ya sigara na tumbaku
.mapato ya korosho
.mapato ya kahawa
.mapato ya mafuta ya kula
Kwa ufupi yote hayo bado hatutosheki hadi tuongeze kodi kwa mlaji wa mwisho
 
Uko sahihi, au pia wakaweka kodi kubwa zaidi kwenye hizo plastiki za energy, juice na soda kuliko za maji ya kunywa.
Suluisho sio kuweka tozo mana tozo itaturudia sisi walaji wala sio mfanyabiashara.
Jambo la kufanya ni kupiga marufuku makopo ya rangi kama Novida na Energy.
Mana ukiangalia walokota makopo wanalokota makopo yote isipokuwa haya yenye rangi hivyo serikali na wizara yake ipige marufuku kutumika kopo hizi..
 
Uko sahihi, au pia wakaweka kodi kubwa zaidi kwenye hizo plastiki za energy, juice na soda kuliko za maji ya kunywa.
Ni vema kuviondoa mana kodi ni za kupunguzwa sio kuongezwa tena hapa tulipo yenyewe kodi zimekuwa ni mzigo kwa walaji.
 
Makonda wa daladala nao walipe tozo,maana samtaim Kwa siku wanagawana mpaka kumi na Tano elfu mambo yakichanganya.
Posho za wabunge nazo zikatwe kidogo,baa
Angalau afu ishirini,Kwa siku wanakula laki tati kipindi Cha bunge,pesa mingi sana hiyo.
 
Tatizo lako unahisi kuwa kodi ikiongezwa ni mfanyabiashara anaongezewa, kodi anayelipa ni mlaji wa mwisho kwa hiyo ni kuongeza tu mzigo kwa mtanzania!!

Kama hazihitajiki ni kupiga marufuku na siyo kuweka mzigo wa kodi kwa mwananchi kila kukicha!
 
Back
Top Bottom