Uchaguzi 2020 Kuelekea Oct 2020 m-NEC Mara ajiandaa kuweka safu yake ya uongozi mkoa wa Mara

Nyamemba

JF-Expert Member
Nov 3, 2011
845
446
TAMBUA MIPANGO KABAMBE KATIKA KUELEKEA UCHAGUZI WA OCTOBER 2020

GACHUMA APANGA SAFU YA VIONGOZI MARA

Ndugu wana ccm wenzangu naomba kuleta kwenu taarifa ya masikitiko iliyotufikia kutoka Mkoa wetu pendwa wa Mara kwa namna ambavyo tunapangiwa safu ya uongozi katika ngazi za ubunge kutoka kwa matakwa MNEC Gachuma ambaye amepoteza hadhi ya Mkoa kwa baadhi ya majimbo pamoja na kupanga wapendwa wake katika Ubunge wa viti maalumu Mkoa wa Mara.

Harakati tayari zimepamba moto ambapo katika kikao kilichokaa katika eneo la Bukenye nyumbani kwa Mzee Gachuma tarehe 31/05/2020 huku hoja kuu ikiwa ni kupanga safu ya wabunge wa majimbo na viti maalumu ambapo waliafikiana kama ifuatavyo...

Jimbo la Tarime Mjini apitishwe Ndugu Michael Kembaki au kijana wa Kangoye..

Jimbo la Tarime vijijini apitishwe Mwita Mwikwabe Waitara.

Jimbo la Rorya Mr. Sanya

Jimbo la Butiama Magori Zeba

Jimbo la Bunda vijijini Boni Getere.

Jimbo la Serengeti Mr. Patrick Chandi.

Musoma Mjini Vedastus Mathayo.
Mwibara Kangi A Lugola


Baada ya makubaliano hayo kikao kiliweka mkakati kuwa ni lazima Gachuma aandaliwe kuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara 2022 ili kumwondoa Mwenyekiti aliyepo kwa sasa kwa sababu tu hakubaliani na Mzee Gachuma katika mipango ya kuitawala Mara.

Pia katika kikao hicho walikubaliana wote kwa pamoja kuwa ni lazima viti maalumu vichukuliwe na Rhobi Kabaka ambaye ni mtoto wa Mama Kabaka kwa gharama yoyote ile pia kikao hicho kiliwapendekeza wabunge wengine wa Viti Maalumu kuwa ni Amina Makilagi pamoja Mossy Magere.

Katika kukamilisha Mkakati huo waliazimia na kukubaliana kuwa Mama Kabaka ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya NEC na Mjumbe wa NEC apewe jukumu la kuhakikisha kuwa hayo majina yote yaliyopendekezwa na Kikao hicho cha faragha yanarudi na kwamba kwa gharama yoyote ile yasikatwe huko juu. Mama Kabaka ahakikishe wahusika wote wanapewa chao ili wakamilishe Mkakati huu kwa manufaa yao.

Mkakati mwingine katika kikao hicho ilikuwa ni kuwadhibiti kwa gharama yoyote ile watia nia wengine ambao siyo wa kundi hilo na ambao wanaonekana tishio katika Majimbo hayo.
Azimio lingine katika kikao hicho ilikuwa ni jukumu la Mama Kabaka kuhakikisha kuwa anawadhibiti Viongozi wa Makao Makuu ya Chama kwa gharama yoyote ile.

Aidha Mzee Gachuma aliwajulisha wajumbe wa kikao hicho kuwa yeye yupo karibu sana na Mzee Mangula na Katibu wa CCM Taifa Dr. Bashiru Ali na Bwana Humphrey Polepole na kwamba anawamudu ila alionesha hofu yake kwa Makamu Mwenyekiti wa zanzibar na Mwenyekiti wa Taifa.
Hivyo alitoa ombi lake kwa Mama Kabaka afikishe hoja hiyo kwa viongozi hao wa juu jukumu ambalo Mama Kabaka alikubali na akasema hilo lipo ndani ya uwezo wake na kuwa atalimudu kwa asilimia mia moja.

Baada ya makubaliano kikao hicho kilihiarishwa na wajumbe kuondoka kutoka Bukenye ambapo ndiyo ngome kuu ya mipango yote kwa sasa.

Hoja yangu hapa ni kuwa ni kweli kwamba mipango hii ya kuchaguliwa viongozi sisi wananchi wa Mkoa wa Mara bado ni endelevu na inafanywa na Mzee Gachuma? Tuendelee kuvumilia kweli mpaka lini?

Hii kambi ya Gachuma ambaye pia ni zao la kupoteza majimbo mengi Mkoa wa Mara kwenda Upinzani bado ataendelea kuvuruga mkoa wetu ili wengine tunaangalia? Tuseme imetosha na SASA GACHUMA NA KABAKA BASI

Ni kweli kuwa swara la kura za maoni kwa sasa mkoa wa mara ni viini macho tu na pia ni danganya toto na kuwa uchaguzi sasa ni dhahili uliisha isha kitambo?

Nani wa kuikomboa ccm mkoa wa mara?

Tunamasikitiko makuu juu ya mipango hii dhalimu ndani ya chama chetu ccm mkoa wa Mara.

*HILI NI SIKIO LA MWANACCM ASIYE NA KAMBI KUTOKA MKOA WA MARA.*
 
Kwakua nyinyi wote mliotajana hapo ni Ndugu (wana CCM), basi wacha mi nichukue tu jembe nikalime.
 
Kwa kifupi hawo wote uliowataja ktkt majimbo yote ya mara ni CCM Maslahi iliyoasi 2015 na kukipigia chadema Kampeni ishinde kwenye uchaguzi mkuu.

1.Musoma mjini - Mathayo, huyu aliandaa vijana kudeki barabara kila alipokanyaga Lowassa akishirikiana na Sanya aliyekuwa mwkt mkoa wa Mara.

2.Bunda vijijini - Bonface Getere,huyu siihitaji kumzungumzia na yeye anajua aliokota embe juu ya mnazi na kama kuna mpango wa kumrudisha kwa mgongo wa ukabila hatapata.

3.Serengeti - Mbunge wa sasa licha ya kuwa TANGATANGA hakubaliki kabisa.

Kumleta Chandi Marwa ni kuendelea kuuaminisha umma kuwa usaliti ndani ya CCM unalipa.Chandi amekuwa mwkt wa CCM wilaya kwa vipindi viwili, 2015 Chandi akiwa mnec alimrubuni mwkt wa Ccm wilaya ndg Vicent Nyamasagi akishirikiana na Sanya mwkt CCM mkoa, Mathayo mgombea ubunge Musoma, Mnec na wengine kwenda uwanja wa sheikh Amri Abeid Arusha kwenye safari ya matumaini na kudanganya eti wametumwa na wana Serengeti kumuomba mzee Lowassa akagombee urais.

Baada ya vikao vya chama kuliondoa jina la Lowassa, Mnec wa Serengeti Chandi na mwenyekiti Vincent waligoma kufanya kampeni kwenye majukwaa ya CCM, tukapoteza jimbo kwa chadema na kura chache kwa mh Rais.

Utaratibu wa kupanga safu za uongozi kikabila siyo mzuri ktk nchi yetu na nashangaa vikao vya nanma hiyo kusemwa vimekaa kwa Gachuma anayejinasibu kuwa rafiki wa Mwalimu.

Mara kuna makabila mengi, ni bora sasa wengine washirikishwe kwenye uongozi ili kuleta mabadiliko ktk mfumo wa utawala maana mzee Gachuma kwa leo ang'atuke tu .
 
Kama ni kweli basi Gachuma achukuliwe hatua. Toka nikiwa sekondari namsikia tu huyu mzee mhuni, alizoe kuitafuna ccm toka zamani
 
Kwa kifupi hawo wote uliowataja ktkt majimbo yote ya mara ni CCM Maslahi iliyoasi 2015 na kukipigia chadema Kampeni ishinde kwenye uchaguzi mkuu.
1.Musoma mjini - Mathayo, huyu aliandaa vijana kudeki barabara kila alipokanyaga Lowassa akishirikiana na Sanya aliyekuwa mwkt mkoa wa Mara.
2.Bunda vijijini - Bonface Getere,huyu siihitaji kumzungumzia na yeye anajua aliokota embe juu ya mnazi na kama kuna mpango wa kumrudisha kwa mgongo wa ukabila hatapata.
3.Serengeti - Mbunge wa sasa licha ya kuwa TANGATANGA hakubaliki kabisa.
Kumleta Chandi Marwa ni kuendelea kuuaminisha umma kuwa usaliti ndani ya CCM unalipa.Chandi amekuwa mwkt wa CCM wilaya kwa vipindi viwili, 2015 Chandi akiwa mnec alimrubuni mwkt wa Ccm wilaya ndg Vicent Nyamasagi akishirikiana na Sanya mwkt CCM mkoa, Mathayo mgombea ubunge Musoma, Mnec na wengine kwenda uwanja wa sheikh Amri Abeid Arusha kwenye safari ya matumaini na kudanganya eti wametumwa na wana Serengeti kumuomba mzee Lowassa akagombee urais.
Baada ya vikao vya chama kuliondoa jina la Lowassa, Mnec wa Serengeti Chandi na mwenyekiti Vincent waligoma kufanya kampeni kwenye majukwaa ya CCM, tukapoteza jimbo kwa chadema na kura chache kwa mh Rais.
Utaratibu wa kupanga safu za uongozi kikabila siyo mzuri ktk nchi yetu na nashangaa vikao vya nanma hiyo kusemwa vimekaa kwa Gachuma anayejinasibu kuwa rafiki wa Mwalimu.
Mara kuna makabila mengi, ni bora sasa wengine washirikishwe kwenye uongozi ili kuleta mabadiliko ktk mfumo wa utawala maana mzee Gachuma kwa leo ang'atuke tu .
Mkuu hapa kuna ukweli mwingi sana
 
Siamini uliyoyaandika hapa, kwenye hicho kikao jimbo la musoma vijijini walimweka nani? Je,Bunda mjini nani aliwekwa? CCM ya sasa haitaki figisufigisu, hata mzee Gachuma analijua hilo.Mleta uzi kama una ushahidi wa haya uliyoyaandika hapa, kwa nini usiwasilishe malalamiko kwenye chama ukiambatanisha na ushahidi?Comrade Polepole alitoa namba ya simu kwa ajili ya mawasiliano ya WhatsApp,hukuiona?Kulalamika hapa JF haisaidii kitu na utaonekana una lengo la kuchafua watu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom