Elections 2015 Kuelekea 2015: Kama CCM Itamsimamisha Edward Lowassa...

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,467
113,578
Wanabodi,

Baada ya kumsikiliza kwa makini Waziri Mkuu "Mstaafu", Edward Lowassa katika two- series za kipindi cha Dakika 45 cha ITV, kwanza nimemkubali sana huyu jamaa!, pili kama yeye ndiye angekuwa rais, ile 2005, Tanzania tusingefikia hapa tulipofikishwa sasa na utawala wa JK!, ila kikubwa zaidi, (kama ni kweli afya yake sio mgogoro kama anavyodai mwenyewe kuwa yuko fit, japo he looks sick!), CCM ikimsimamisha yeye kugombea urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi, then matokeo ya urais kwa 2015, ni CCM tena!. Mkubali!..., mkatae!.

Hizi ni baadhi tuu ya sababu, kwanini CCM itashinda tena kwa ushindi wa kishindo kikuu, endapo and only if itamsimamisha Edward Lowassa!.

1. Uwezo wa Kusema, Kupanga, Kutenda na Kusimamia!.
Viongozi karibu wote waliopo CCM, wana uwezo mkubwa sana kesema!, tutafanya hiki, tutafanya kile!, ni maneno tuu! na pia wana uwezo mkubwa wa kupanga mipango kwa maneno tuu na sii matendo, au usimamizi, mfano mipanga kamambe kama (Mkukuta, Mkuza, Mkumbita, Mkurabita, na sasa Dira 2025)!. Mipango yote hii ni mizuri kwa maneno tuu, lakini wengi hawana uwezo wa kutenda na kusimamia utekelezaji!. Mipango mingi iliyopangwa, inaishia kwenye maneno na mabuku na makabrasha tuu, lakini utekelezaji kwa vitendo ni sifuri!. Kwa Edward Lowassa, yeye sio msemaji sana, bali ni mtendaji kweli!, yeye sio mtu wa maneno mingi!, ni mtu wa vitendo virefu!, he is an action oriented man!. Mfano hai ni pale alipokutana na madudu ya City Waters!, aliwafurusha there and then!. Hata madudu ya Richmond, alitaka kuwafurusha na kutaifisha kila kitu ila alishindwa!, kutokana na "mwenye mitambo!".

Tulipopata uhuru miaka ya 60, maadui wetu wakuu watatu, walikuwa ni Ujinga, Umasikini na Maradhi, na tulijiwekea misingi yetu mikuu minne ya maendeleo kuwa ili tuendelee, tulihitaji vitu vinne: Watu, Ardhi, Siasa Safi na Uongozi Bora!. Kwenye hiyo misingi, tulisema Pesa sio msingi, pesa ni matokeo!, hili ndilol lililokuwa kosa pekee la Mwalimu, kutofautiana na misingi ya ukweli ya uchumi, kama ilivyofundishwa na Adam Smith (land, labor, capital na interpreneureship)!. Kwenye ile misingi minne tulisahau capital kwa kudai "pesa sii msingi!".

Watu tunao na ardhi ya kutosha, yenye rutuba, vyanzo lukuki vya maji, madini, maliasili etc etc tunazo. Tulikuwa na tatizo kidogo la utekelezaji wa siasa safi ya Ujamaa na Kujitegemea na uongozi bora, ndio maana nchi tulizopata nazo uhuru, ile miaka ya 60, wao wakiwa ni masikini wa kutupwa kuliko sisi, with nothing, kana Tiger nations, leo wako mbali!, sababu pekee iliyowafikisha wenzetu pale walipo, wakati sisi tunaendelea kupiga mark time ni Elimu!. Sisi tulitaja tuu kuwa Ujinga ni adui, lakini we never invested on Elimu because we had no capital!. Nyerere aligombana na maprofesor wa uchumi, Kina Prof. Rweyemamu, wakajitimkia zao, akagombana Edwin Mtei na IMF, WB etc matokeo sote tunayajua!.

Lowassa na timu yake ya Boys II Men, walipoingia tuu madarakani, EL akafanya study tour ya nchi tulizoanza nao wakati wa uhuru!, kwanini wao wamefanikiwa, wako mbali na sisi wametuacha nyuma sana!, akagundua wali invest kwenye elimu!. Akarudi nyumbani, akahamasisha kila kata iwe na shule ya sekondari ili kila Mtanzania apate kwanza elimu, mengine yote, yatafuatia!. Baada ya kujengwa shule, zilikuwa zipatiwe vifaa na waalimu wa kutosha!.

Baada ya kujiuzulu, serikali ya JK ikazi abandon zile shule za EL ili kumkomoa!. Sasa zinaitwa St. Kayumba!. Mpango wa kufundisha waalimu wa ukweli, ukaachwa, nanachukulia wale failures wenye Div IV karibu na zero, na kuwa brush kwa miezi mitatu! (Waalimu wa Voda Faster!). Jana alipozungumzia umuhimu wa kuwaelimisha kwanza watu wetu, amenigusa sana!. Tungekuwa tumeelimika, tusingeibiwa hivi madini yetu!, tunaibiwa madini yetu huku tunaangalia kwa sababu hatuna elimu ya madini!, sasa tumegundua gesi,serikali inakimbilia kugawa vitalu kwa umiliki wa miaka 99 huku Watanzania hatuna hili wala lile kuhusu elimu ya gesi, hatuna sera wala sheria ya gesi!. Kwa kifupi, hutujui lolote wala chochote kuhusiana na gesi!, na tutaishia kuibiwa tena gesi yetu kwa kukosa elimu ya gesi!. Edward Lowassa ameshauri, hiyo gesi tuiache kwanza!, lets invest kwenye elimu kwanza kwa watu wetu, ili kuwa empower hawa watu wetu kielimu ndipo tuingie kwenye ambitious projects kama za kuvuna gesi, au kilimo kwanza etc!.

Kwa hili pekee, CCM ikimsimamisha EL, Tanzania itapata ukombozi wa kweli wa pili wa Mtanzania!.

Nimesema, CCM ikimsimamisha EL, 2015, itakuwa ni CCM tena, kwa sababu katika wapinzani wote, hakuna hata mgombea mmoja anayeweza kusimama na Lowassa kwenye urais wa 2015 na bado akaambulia kura!, there is no one!, none!.

Mwenye masikio na asikie!.

2. Dhambi Kubwa ya Lowassa ni Richmond Tuu!.

Najua wapinzani wa dhana ya ukweli, watakuja na hoja za dhambi kubwa ya Lowassa ni fisadi wa Richmond!, then time will tell, hiyo ni mizigo tuu ya watu, alijitolea kuibeba ili kwa kuteswa kwake, wao waokoke!, wakati muafaka ukifika, hili litawekwa wazi na Watanzania mtawafahamu wenye zigo lao haswa ni kina nani!. Wenye akili wameshang'amua ile metarmophosis process from Richmond -Dowans -Simbion na kwa msio jua, mkae mkijua Tanesco bado inailipa Simbion capacity charge ile ile ya dola 152 kama Richmond na Dowans, hivyo tumeruka majivu na kukanyaga moto, tumeruka maji na kukanyaga tope, na kwa usafi tumeruka nyasi, tukakanyaga ma..!.

3. CCM Haina zaidi ya EL na Upinzani hawana wa Kushindana Nae!.

Wanabodi ni mimi niliwahi kusema, CCM imechokwa na Chadema Haijajipanga, baadae nikasema CCM imechokwa mpaka basi!, Baada ya Chadema kuanza kujipanga nikasema Chadema, Njia Nyeupe Ikulu, lakini sasa baada ya kumsikia Edward Lowassa, kama ni kweli afya yake sii mgogoro kama anavyoonekana!, na CCM ikamsimamisha yeye, come 2015, then, mshindi wa uchaguzi wa 2015, ni CCM tena!, kinyume cha hapo, CCM ikimsimamisha mwingine yeyote, 2015, Chadema inachukuwa nchi kiulaini kama kumsukuma mlevi, unless kama CCM itamtosa Lowassa na kulisimamisha jembe lake pekee, John Pombe Magufuli, tatizo la Magufuli anaweza kuja kuwa dikiteta wa ajabu hadi hao CCM wenyewe wakajuta!.

Mwisho.
Namalizia kwa swali moja tuu, Jee CCM inaujasiri wa kuukubali ukweli huu mchungu wa kumsimamisha Edward Lowassa ili kuweza kujiokoa?! au itaendeleza kiburi uongozi na jeuri ya uchama tawala kusubiria kifo cha mende, kwa kufa huku inajiangalia kwa kutegemea itaendeleza uking'ang'anizi wake kwa kuamini this time pia itashinda tena kwa kuutumia uwongo ule ule, na mbinu zile zile za uchakachuaji ule ule, kwa matarajio katiba mpya pia ita provide opportunities za aina ile ile ya miaka ya nyuma, kuwa ita endelea "to fool all the people all the times?!.

Asante.

Pasco.

NB. Japo Pasco wa JF ni mwanachama wa Chama cha siasa, pia mshabiki wa wanasiasa mbalimbali, kwa CCM ni Pro Lowassa, kwa Chadema ni Pro ZZK na kwa CUF ni Pro-Jussa!.

Input ya Tanganyika Tanu.

Mpaka sasa kuna kila dalili kuwa mgombea urais wa CCM 2015 huenda akawa Edward Lowassa kutokana na nguvu ya kisiasa aliyonayo ndani ya CCM kwa sasa hususani kwa wajumbe wengi wa vikao vikuu vya juu vya maamuzi ndani ya CCM(Kamati kuu, Halmashauri kuu na Mkutano Mkuu).
Wakati huo huo kama kuna jambo wanachama wa CHADEMA wangependa kuliona basi ni Lowassa kuwa mgombea urais wa CCM 2015.
Kwa sababu zifuatazo:

1/Moja ya hoja zilizoipa nguvu sana na Umaarufu mkubwa sana CHADEMA ni Vita dhidi ya Ufisadi, Lowassa ni mtu anaaminiwa kama fisadi zaidi kuwahi kutokea ndani ya CCM, hivyo kutaipa nguvu zaidi CHADEMA katika harakati zao.

2/Kumbukumbu isiyofutika ya kitendo cha Lowassa kujiuzuru uwaziri mkuu kutokana na kuhusika katika Ufisadi mkubwa wa mkataba tata wa kampuni ya kufua Umeme wa dharura(Richmond).

3/Vita ya kufa na kupona kati ya Lowassa dhidi ya makundi mengine ya wanaCCM wenzie wanaoutaka urais pia, ambao wamekuwa kila mara wakianikana baadhi ya maovu yao hadharani. Katika hili atakosa 'Support' muhimu kutoka kwa wanaCCM wengine 'muhimu' wanaomchukia.
Mkuu Tanganyika TANU (now Konkereti), pole sana, hii kitu yako imeunganishwa kwangu!. Ili kukutendea haki, nimeiweka kule juu kwenye main post.
Pasco.
 
nilijua utakuwa wew tu...ni mawazo yako labda na familia yako....lakini watanzania wanjua nin wanahitaji katika hiki kipindi kigumu katika maisha yao...
 
Pasco

Mbona kwenye thread za polisi kufanya mauaji morogoro sikuoni?

au hizi thread za EL zina maslahi ?
 
Pasco unatumia sabuni gani na brash gani na maji yenye kemikali hipi kusafisha hii kitu yenye kutu???Naomba jibu this is too late maana CCM wanajua kisasi alichonacho rohoni wamsimamishe apate uraisi awafanye kama Chiluba na Kenneth Kaunda??no way na haitakuja kuwa!!for your info!
 
Last edited by a moderator:
Quote: NB. Japo Pasco wa JF sio mwanachama wa Chama chochote cha siasa, kwa CCM ni Pro Lowassa, kwa Chadema ni Pro ZZK na kwa CUF ni Pro-Jussa!.

..Leo ndio nimekusoma itikadi yako Brother Pasco!!. Leka Tutigite
 
You really need help Pasco
seriously

Wapo watu waliamini kwa asilimia 100 kuwa Rais aliefaa mwaka 1995 na 2005 alikuwa
Salim A Salim
Watu hao ni pamoja na Mwalimu Nyerere

lakini hawakuwahi kuwa 'this crazy over one person'....

Nahofia coming 2016 na Rais sio huyu unaemtaka
unaweza usi recover mentally kwa kweli......You need help now
 
Mkuu kama ni hivi bado safari ni ndefu sana ya kutusababisha tumwamini..Convincing yake inahitaji kuchukua miaka 20 ambapo umri wake utakuwa umeshaenda sana..kama nafasi alikuwa nayo akaichezea kuirudisha ni ngumu sana..Namshauri atafute mtu wa type yake amweke but not him.
 
Quote: NB. Japo Pasco wa JF sio mwanachama wa Chama chochote cha siasa, kwa CCM ni Pro Lowassa, kwa Chadema ni Pro ZZK na kwa CUF ni Pro-Jussa!.

..Leo ndio nimekusoma itikadi yako Brother Pasco!!. Leka Tutigite

Leka Dutigite EL...!!!!
 
..Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema aliwahi kuulizwa nini vitakuwa vipaumbele vitatu vya Chadema endapo itakamata Dola, alijibu:
1. Elimu
2. Elimu
3. Elimu
Nilimsikiliza Lowassa jana, nae anasisitiza haungi mkono Kilimo Kwanza, bali Elimu Kwanza.
What a coincidence?
 
Wanabodi,

Baada ya kumsikiliza kwa makini Waziri Mkuu "Mstaafu", Edward Lowassa katika two- series za kipindi cha Kipima Joto cha ITV, kwanza nimekubali sana huyu jamaa!, pili kama yeye ndiye angekuwa rais, ile 2005, Tanzania tusingefikia hapa tulifikishwa sasa na utawala wa JK, ila kikubwa zaidi, (kama ni kweli afya yake sio mgogoro kama anavyodai yuko fit, japo he looks sick), CCM ikimsimamisha yeye kugombea urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi, them matokeo ya urais kwa 2015, ni CCM tena!. Mkubali, mkatae!.

Hizi ni baadhi tuu ya sababu, kwanini CCM itashinda tena, endapo and only if itamsimamisha Lowassa!.

1. Uwezo wa Kupanga, Kusema, Kusimamia na Kutenda.
Viongozi karibu wote waliopo CCM, wana uwezo mkubwa sana kupanga wa kusema tuu, (Mkukuta, Mkumbita, Mkurabita, Mkuza, na sasa Dira 2025), lakini hawana uwezo wa kusimamia na kutenda!, mipango mingi iliyopangwa, inaishia kwenye maneno na vitendo sifuri!. Edward Lowassa sio msemaji, bali ni mtendaji, yeye sio mtu wa maneno mingi, ni mtu wa vitendo virefu, he is an action oriented man!.

Tulipopata uhuru miaka ya 60, maadui wetu wakuu watatu, walikuwa ni Elimu, Umasikini na Maradhi, na tulijiwekea misingi yatu mikuu minne ya maendeleo kuwa ili tuendelee, tulihitaji Watu, Ardhi, Siasa Safi na Uongozi Bora!. Kwenye hiyo misingi, tulisema Pesa sio msingi, pesa ni matokeo!, hili ndilol lililokuwa kosa pekee la Mwalimu, kutofautiana na misingi ya ukweli ya uchumi, kama ilivyofundishwa na Adam Smith (land, labor, capital na interpreneureship)!. Kwenye ile mising minne tulisahau capital!.

Watu tunao na ardhi ya kutosha, yenye rutuba, vyanzo lukuki vya maji, madini, maliasili etc etc tunazo. Tulikuwa na tatizo la siasa safi na uongozi bora, ndio maana nchi tulizopata nazo uhuru, wao wakiwa ni masikini wa kutupwa with nothing, kana Tiger nations, leo wako mbali!, sababu pekee iliyowafikisha wenzetu pale walipo, wakati sisi tunaendelea kupiga mark time ni Elimu!. Sisi tulitaja tuu kuwa Elimu ni adui, lakini we never invested because we had no capital. Nyerere aligombana na maprofesor wa uchumi, Kina Prof. Rweyemamu, wakajitimkia zao, akagombana na IMF, WB etc matokeo tunayajua!.

Lowassa na timu yake ya Boys II Men, walipoingia tuu madarakani, akafanya study tour ya tulioanza nao kwanini wamefanikiwa, wako mbali na sisi wametuacha sana!, akagundua wali invest kwenye elimu!. Akarudi akahamasisha kila kata iwe na shule ya sekondari ili kila Mtanzania apate kwanza elimu, mengine yote, yatafuatia!.

Baada ya kujiuzulu, serikali ya JK ikazi abandon zile shule za EL ili kumkomoa!. Jana alipozungumzia umuhimu wa kuwaelimisha kwanza watu wetu, amenigusa sana!. Tungekuwa tumeelimika, tusingeibiwa hivi madini yetu, sasa tumegundua gesi,serikali inakimbilia kugawa vitalu kwa umiliki wa miaka 99 huku Watanzania hatuna hili wala lile kuhusu gesi, kwa kifupi, hutujui lolote na tutaishia kuibiwa tena!. EL ameshauri, lets invest kwenye elimu kwanza ili kuwa empower watu wetu ndipo tuingie kwenye ambitious projects kama za kilimo kwanza gesi etc!.

Kwa hili pekee, CCM ikimsimamisha EL, Tanzania itapata ukombozi wa kweli wa puli wa Mtanzania!.

Nimesema, CCM ikimsimamisha EL, 2015, itakuwa ni CCM tena, kwa sababu katika wapinzani wote, hakuna hata mgombea mmoja anayewa kusimama na Lowassa kwenye urais na bado akaambulia kura!, there is no one!.

Mwenye masikio na asikie!.

2. Dhambi Kubwa ya Lowassa ni Richmond Tuu!.

Najua wapinzani wa ukweli, watakuja na hoja za dhabi kubwa ya Lowassa ni Richmond, then time will tell, hiyo ni mizigo tuu ya watu, alijitolea kuibeba ili kwa kuteswa kwake, wao waokoke, wakati muafaka ukifika, hili litawekwa wazi na Watanzania mtawafahamu wenye zigo lao!. Wenye akili wameshang'amua ile metarmophosis process from Richmond -Dowans -Simbion na kwa msio jua, mkae mkijua Tanesco bado inailipo Simbiaon capacity charge ile ile ya dola 152 kama richmond na Dowans, hivyo tumeruka majivu na kukanya moto, tumerika maji na kukanyaga tope, na kwa usafi tumeruka nyasi, tukakanyaga ma..!.

3. CCM Haina zaidi ya EL na Upinzani hana wa Kushindana Nae!.

Wanabodi ni mimi niliwahi kusema, CCM imechokwa na Chadema Haijajipanga, baadae nikasema CCM imechokwa mpaka basi!, Baada ya Chadema kuanza kujipanga nikasema Chadema, Njia Nyeupe Ikulu, lakini sasa baada ya kumsikia Edward Lowassa, kama ni kweli CCM itamsimamisha, then, 2015, ni CCM tena, kinyume cha hapo, CCM ikimsimamisha mwingine yoyote, 2015, Chadema inachukuwa nchi kiulani kama kumsukuma mlevi!.


Mwisho.

Namalizia kwa swali moja tuu, Jee CCM itaukubali huu ukweli mchungu wa kumsimamisha Lowassa ili kuweza kujiokoa?, itakubali kusubiria kifo cha mende huki inajiangalia kwa kutegemea itaendeleza uking'ang'anizi wake kwa kuamini this time pia itashinda tena kwa kuutumia uwongo ule ule, na mbinu zile zile za uchakachuaji, kwa kutegemea katiba impya ita provide opportunities za aina ile ile ya miaka ya nyuma, kuwa ita endelea "to fool all people all times?!.

Asante.

Pasco.

NB. Japo Pasco wa JF sio mwanachama wa Chama chochote cha siasa, kwa CCM ni Pro Lowassa, kwa Chadema ni Pro ZZK na kwa CUF ni Pro-Jussa!.

Manywele juu, juu juu zaidi
 
Wanabodi,

2. Dhambi Kubwa ya Lowassa ni Richmond Tuu!.

Najua wapinzani wa ukweli, watakuja na hoja za dhabi kubwa ya Lowassa ni Richmond, then time will tell, hiyo ni mizigo tuu ya watu, alijitolea kuibeba ili kwa kuteswa kwake, wao waokoke, wakati muafaka ukifika, hili litawekwa wazi na Watanzania mtawafahamu wenye zigo lao!.

Hauko serious. Lowasa u-billionea wake ule unafikiri kapatia Richmond? Au unafikiri ni ali-save mshahara wake akawa bilionea wa kutisha? Uliza watu alifanya nini alipokuwa waziri pale wizara ya Ardhi. Kumbuka Nyerere alimkataa Lowasa kwamba hana ethics za uongozi KABLA ya hiyo Richmond. Kumbuka wahindi waliomwambia Lowasa ananuka rushwa KABLA ya hiyo Richmond. Yes, anajua sana kuongea na kupanga hoja, lakini hivi unamjua Lowasa wewe?
 
Kama kweli jamaa alikuwa msafi na anauchungu na wa TZ angewataja wa husika wa richmond ili wamuamini ni mtendaji na mtetezi. Bt jamaa kiukweli bila kuficha hafai tena hafai coz hakuona shida kuwasulubu wezi bali akabeba msalaba huo ambao hatautua kutoka mioyo ya watu up to the death. Namshauri ndoto hizo za mchana asiote tena. Wa TZ si maiti tena.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom