Kudai haki hakuwezi kuwa bila gharama

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,848
35,856
Kuna thwawabu kubwa kwa wote wasimamao kuipigania haki kwa ajili ya wote. Kwa maana njia hiyo si kila mtu anaweza kuipita.

Njia hii si lazima kwa kila mtu kuipita. Waipitao njia hii ni wale tu walio na wito kamili. Kama ile iendayo uzimani, ina vikwazo vingi.

IMG_20210729_192941_480.jpg


Kipi ambacho kamanda Mbowe, Heche au yeyote aliyeichagua njia hii iliyotukuka ambacho hakukifahamu?




Kwamba ni awamu hii sasa ndiyo ambayo eti ingeacha kubambika kesi wakati ikijaribu kukomaa ili, hali ya fursa kwao iliyopo sasa isiendelee kubakia? Labda iwe ni kurukwa na akili kuwa na matumaini kama hayo!

Inajulikana wazi kuwa katika harakati hizi madhara (consequences) haziwezi kuepukika. Kutakuwa na watakao kamatwa, watakao bambikiziwa kesi, watakao potezwa, na hata watakaokufa vile vile kama kwenye awamu ile.

Ni gharama kama hizi ambazo kina Julius Nyerere, Nelson Mandela, Solomon Mahlangu, Chris Hani, Kwame Nkrumah, Kenneth Kaunda, na wenzao wa aina hiyo, walizijua na bado hazikuwafanya kughairi. Wapumzike kwa amani mashujaa wetu watukuka hawa wa Afrika.

Makamanda Mbowe, Heche na wote waliokamatwa, watakaokamatwa, watakaopetezwa, kufa na hata ambao hawatakamatwa kwenye harakati hizi, kama ilivyokuwa kwa akina Nyerere, wako tayari kuzilipa gharama hizo kwa ajili Tanzania iliyo bora zaidi ya kesho.

Hakipo kitakacho simamisha jitihada hizi ambazo ni kwa maslahi yetu sote kama taifa wakiwamo watoto wetu na hata watoto wa watoto wetu.

Wito kwenu nyie mnaobambikizia watu kesi hadi maaskofu na hata wazee wastaafu:

"La msingi zaidi ongezeni magereza. Ikibidi ili kuwapunguzia gharama, muwafahamishe tu wapi mngependa kukutana nao mkayafanye yawapendezayo. Kwa hakika watakuja wenyewe kwani wanacho kihitaji ni haki yao tu, iliyopo kwa mujibu wa katiba."

Itambulike kuwa kumedhamiriwa kwelikweli. Kama mnachagua shari dhidi ya maelewano, uchaguzi huo utakuwa ni wenu na utapokelewa kwa mikono miwili.
 
Ukweli mchungu ulipo kwenye uzi huu ni kama ule wa kwenye Mathayo 19:21:

"Yesu akamwambia, “Kama unapenda kuwa mkamilifu, nenda ukauze mali yako, uwape maskini fedha hiyo, nawe utakuwa na hazina mbinguni, kisha njoo unifuate.” Huyo kijana aliposikia hayo, akaenda zake akiwa mwenye huzuni, maana alikuwa na mali nyingi."

Wale wanaotaka kula matunda lakini si kuyapigania, hao ni mzigo. Heri wakaufyata au wakajisogeza Lumumba kama kina mzee Mdee.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
berty ukweli mchungu ilipo kwenye uzi huu ni ule wa Mathayo 19:21

"Yesu akamwambia, “Kama unapenda kuwa mkamilifu, nenda ukauze mali yako, uwape maskini fedha hiyo, nawe utakuwa na hazina mbinguni, kisha njoo unifuate.” Huyo kijana aliposikia hayo, akaenda zake akiwa mwenye huzuni, maana alikuwa na mali nyingi."

Wale wanaotaka kula matunda lakini si kuympigania ni mzigo. Heri wakaufyata au wakajisogeza Lumumba kama kina mzee Mdee.

Au nasema uongo ndugu yangu Pascal Mayalla
Haki haiombwi hudaiwa kwa nguvu, na hupewi mkononi, you have to grab it by force
 
Mzee mbona kelele nyingi mitandaoni harafu huingii barabarani kupambania haki yako?

Hizi kelele za nyuki wa mashineni tushazichoka bana...

Jikusanyeni muingie barabarani mdai haki yenu, simple!
Sio kutupigia makelele yasiyo na tija miaka nenda rudi huku mkitafuta huruma ya huyohuyo mbaya wenu
 
Mzee mbona kelele nyingi mitandaoni harafu huingii barabarani kupambania haki yako?

Hizi kelele za nyuki wa mashineni tushazichoka bana...

Jikusanyeni muingie barabarani mdai haki yenu, simple!
Sio kutupigia makelele yasiyo na tija miaka nenda rudi huku mkitafuta huruma ya huyohuyo mbaya wenu
Kama vile mlivyoingia barabarani kupinga Tozo za solidarity au sio.
 
Mzee mbona kelele nyingi mitandaoni harafu huingii barabarani kupambania haki yako?

Hizi kelele za nyuki wa mashineni tushazichoka bana...

Jikusanyeni muingie barabarani mdai haki yenu, simple!
Sio kutupigia makelele yasiyo na tija miaka nenda rudi huku mkitafuta huruma ya huyohuyo mbaya wenu

Ngoja tuchanjwe kwanza tujihakikishie kuwa ninyi mmeshabakia na m@vi yenu.

IMG_20210728_134628_357.jpg


Serikali 'sikivu' Inaposikia nusu nusu

Subirini tuchanjwe sauti zetu mtazisikia!


IMG_20210711_205649_038.jpg


Kwani hata chanjo ninyi mlitaka tuchanjwe? Si mnajua mnahusika kwenye mauaji ya halaiki ya wahanga wa Corona hapa nchini kwa porojo zenu za awamu ile kuhusiana na ugonjwa huu?

Chawa wahedi wa mwendazake nyie! Eti makelele? Umeguswa eeh? Na bado!

Mmebakia kulia lia mitandaoni eti nchi imeuzwa. Nendeni mkapumzike kwa amani Chatto kama hamuwezi tena kuingia barabarani kupinga ujio wa chanjo. Hayo nayo yakiwashinda fuateni ushauri wa Mwigulu mhamie hata Burundi. Wala hatutawakumbuka.

Ukweli mchungu hata mawazo yenu tu, watu pori nyie, hatuyahitaji.

Habari ndiyo hiyo.
 
Ngoja tuchanjwe kwanza tujihakikishie kuwa ninyi mmeshabia na m@vi yenu.

View attachment 1872367

Kwani hata chanjo ninyi mlitaka tuchanjwe? Si mnajua mnahusika kwenye mauaji ya halaiki ya wahanga wa Corona hapa nchini kwa porojo zenu za awamu ile kuhusiana na ugonjwa huu?

Chawa wahedi wa mwendazake nyie! Eti makelele?

Mmebakia kulia lia mitandaoni eti nchi imeuzwa. Nendeni mkapumzike kwa amani Chatto kama hamuwezi tena kuingia barabarani kupinga ujio wa chanjo. Hayo nayo yakiwashinda fuateni ushauri wa Mwigulu mhamie hata Burundi. Wala hatutawakumbuka.

Ukweli mchungu hata mawazo yenu tu, watu pori nyie, hatuyahitaji.

Habari ndiyo hiyo.
Hahahahaaah! Kachanjwe tu mkuu harafu ukishachanjwa njoo tuendelee kuvaa barakoa...

sijawahi lazimisha/shwa kuingia barabarani kwa jambo lolote lile, kwa vile naonaga ni upuuzi tu... unaongelea tozo ova upo ulaya huko wakati wote tupo kuhenya kuzilipa
 
Hahahahaaah! Kachanjwe tu mkuu harafu ukishachanjwa njoo tuendelee kuvaa barakoa...

sijawahi lazimisha/shwa kuingia barabarani kwa jambo lolote lile, kwa vile naonaga ni upuuzi tu... unaongelea tozo ova upo ulaya huko wakati wote tupo kuhenya kuzilipa

Ngoja sisi tuchanjwe. Mengine yote kelele za mlango.
 
Back
Top Bottom