Kuchapwa viboko wanafunzi wakuchoma mabweni wa mali za shule hakutoshi tuwe na sheria ya KUNYONGA watakaobainika.

Adhabu ya kunyonga siafiki. Lakn adhabu aliyotoa RC haitoshi alitakiwa acharaze bakora hadi washindwe kutembea ili iwe fundisho kwa wengine. Kuna ndg yake m1 aliwahi kucharaza walimu!
Basi iwepo sheria inayotamka kunyongwa ili ilete utisho
 
Nyinyi mbona mmeifisadi hii nchi tangu 1961 mpaka leo, na bado mnatembea barabarani na minguo yenu ya kijani huku mkiwa hamna hata chembe ya aibu?

Si mnastahili kabisa adhabu ya kunyongwa! Majambazi wakubwa nyinyi.
Mimi siyo kada na sijawahi kuwa mwanasiasa ni mfanyabiashara huru na nachukia wanasiasa hasa wa CCM hapa nipo kutetea maslahi ya mama Tanzania
 
Hujakosea mkuu Mimi nadhani paweke sehemu kama kisima cha acid watupwe na wapotelee huo haiwezekani wapuuzi wachache walete hasara yote ile kisa usela mavi walioufanya marehemu babu zao,Na wakupingao humu ujue miongoni mwa wale wahuni wamejipumzikia majumbani mwao wanatamani waichome na Jf kabisa .
 
Write your reply...Ingetokea Amepga Fimbo Wale Vjana Then Wakafa Hapo Ndpo Ungejua Kuwa Watanzania Cc N Wamoja
Hamna kitu wangapi wamefia mikononi mwa polisi na kupotea kama kuku, kupigwa risasi hadharani mbona hamna habari nao ??
Sembuse hawa wanaofanya mambo ya hovyo ya kuchoma mabweni na uharibifu wa wazi wa mali za umma
 
Wahujumu uchumi ambao wengine wamesabisha hasara ya mabilioni ya shilingi, fedha ambazo huenda zingetosha jenga mabweni ya mkoa mzima hawanyongwi lakini waliochoma madarasa katika shule moja tu wao wanastahili kunyongwa ati?
Hata wahujumu uchumi na watawala viongozi mafisadi na wauaji haki yao wangenyongwa tu au kufungwa maisha
 
Mkuu wewe ni ME au KE? Una watoto? wameshafikia u teenage au bado ni underfive? Una amini katika uwepo wa MUNGU? Ni hayo tu.
Tuwe na sheria bila kujali haya kuwa watoto wetu au watoto wa nani mkuki kwa nguruwe ikitokea wangu watawajibika tu lazima tuwe na sheria kali ambazo kila mmoja wetu atazitii
 
Huoni kujidanganya hadharani. Tangu lini watanzania mkawa wamoja.

Katika Afrika nzima hakuna watu waoga kama watanzania.
Wa Tanzania ni waoga mno mtu kapigwa risasi hadharani, watu wanapotea hakuna hata uchunguzi wala lolote juu yao wa Tanzania hawana umoja labda ni unafiki na uoga
 
Ukilivuta usiandike JF of GT.
Mimi sivuti wala kutumia kilevi chochote nachotaka ni sheria kali ambazo kila mmoja wetu atazitii kuanzia mafisadi watawala na wetu na wote wanaojiona kuwa wapo juu ya sheria
 
Nimpe pongezi kidogo Mkuu wa mkoa wa Mbeya.
Adhabu ile haitoshi (angechapa viboko 100) uharibifu ni mkubwa, mno kuchoma mabweni na uharibifu mkubwa wa mali wa namna ile haivumiliki.
Hizi ni kodi za walalahoi Zinazojenga na kuweka Samani Mashuleni.
Ikitokea wapuuzi 2 wavutaji bangi wahamasishe uharibifu wa mali zilizowekwa kwa mamilioni ya pesa yafaa WANYONGWE kwa maana wakiachwa ni tatizo kwa jamii hao ndio wezi na majambazi tusilee ugonjwa ni heri wafe tutatue tatizo (PANAPO FUKA MOSHI ZIMA MOTO CHINI)
Kama taifa tufike wakati tusiendekeze ujinga wa namna hii tukiacha haya matatizo kila sehemu yatakua hatutakuwa na suluhisho maana yatakuwa yameota mizizi ambayo kuikata ni vigumu.
SULUHISHO:
Tuwe na sheria kali ya KUNYONGA kwa wote watakaohusika hata kama ni shule nzima ili mradi imethibitika wamehusika.

Haya ni maoni binafsi lakini ni kwa msitakabali wa maendeleo ya taifa letu kutokuruhusu ujinga ujinga unaoweza kuleta hasara zinazo gharimu Taifa.
Ukishanyonga then utafaidikaje? Kama adhabu hiyo ndiyo jibu basi wale wanaowatakia wengine mabaya nao wangenyongwa pia.
 
Mimi sivuti wala kutumia kilevi chochote nachotaka ni sheria kali ambazo kila mmoja wetu atazitii kuanzia mafisadi watawala na wetu na wote wanaojiona kuwa wapo juu ya sheria
Nadhani sheria kali siyo jibu, jibu ni kuwa na sheria zinazowasaidia walio na hatia kubadilika na hapa ndipo hatujafanikiwa.
 
Nyie ndiyo mnaoletaga vita duniani! Unyonge watu kwa makosa madogo madogo! Wao na ndugu zao watakuacha!!! Wewe si binadamu kama wao, walikuwepo wababe dunia hii kina Hitler, Qaddaffi, Sadam, Mobuttu, Mussolini,nk nk wao kila kosa kuua walikufa vifo vya kikatili na fedheha sana mfano Qaddaffi kusukumiziwa kipisi cha chuma njia ya haja kubwa! Damu na roho ya binadamu siyo sawa na ya mbuzi. Ubabe haulipi na hakuna mbabe zaidi ya Mungu
Kwani hawa wamesababisha mangapi ni hasara kiasi gani wamesababisha?
Watoto wa ngapi wanaenda kukosa haki zao za msingi kwa sababu ya wapuuzi wachache?
Lakini tungekuwa na sheria kali ambazo kila mmoja wetu atazitii kuanzia mafisadi watawala wetu haya matatizo yasingetokea
 
Mimi siyo kada na sijawahi kuwa mwanasiasa ni mfanyabiashara huru na nachukia wanasiasa hasa wa CCM hapa nipo kutetea maslahi ya mama Tanzania

Bado hata wewe na wenzako mnastahili kunyongwa mpaka kufa maana hata nyinyi wafanyabiashara ni wahujumu wa uchumi na wakwepa kodi wakubwa! Hapo ulipo utakuta hata mashine ya EFD yenyewe hutumii, unaendesha biashara zako kwa ujanja ujanja tu!

Yaani ni kwamba, hiyo ishu ni ya kawaida sana. Na siyo mara ya kwanza na ya mwisho kutokea kwenye shule zetu. Sema tu imekuzwa na wanasiasa.

Wazazi kufidia uharibifu, wanafunzi kuadhibiwa kwa voboko, adhabu ya mazingira, kurudishwa nyumbani kwa muda (suspension), kufukuzwa shule moja kwa moja, kubadili uongozi wa shule kama ulizembea au kuchangia tukio hilo kutokea, nk. ndiyo adhabu zinazostahili kuchukuliwa siku zote.
 
Back
Top Bottom