Nasikitika kwanza kuwa pendekezo hili naliweka katika maneno ambayo hayajadailutiwa hata kidogo. Kwa maoni yangu, umefika wakati sasa wa kusema no kwa michango ya harusi, ama fedha au mda. Maoni yangu yanazingatia kuwa kwanza kuoana ni uamuzia na muhimu kwa wanaooana. Yapo mambo mengi yenye faida ambayo tunaweza kuchangiana kama vile ada za watoto mashuleni, kuhudumuia wagonjwa na kadhalika. Kama anadhani anataka kufanya harusi, basi aandae kwa fedha zake na awaalike watu waje wamuunge mkono kusheherekea, sio kuwakalisha watu kwa zaidi ya masaa 400 (e.g vikao 5 x masaa mawili kila kikao x wanakamati 20) eti wakiumiza vichwa na hela ili mtu aoe!