Kuchaguliwa tena kwa Wagombea waliohama Vyama, pamoja na kuwapokea kifalme viongozi waliotumbuliwa, ni kielelezo kuwa wanajali maendeleo na si maadili

Daimler

JF-Expert Member
Sep 11, 2018
556
973
Tangu skendo kubwa kubwa za rushwa zianze kujitokeza nchini, hasa katika kipindi cha Utawala wa Awamu ya Nne, ambazo zilipekekea kujiuzulu kwa Viongozi wengi wa Serikali kusnzia Mawaziri, Makatibu Wakuu na Wanasheria wa Serikali, mpaka wenyeviti wa Kamati za Bunge. Hata hivyo, mara zote tuhuma hizo zimeonyesha kuwa, hazina umuhimu mkubwa kwa Watanzania linapokuja suala la maadili. Baadhi ya Viongozi waliotumbuliwa, walipokelewa kishujaa majimboni kwao na kuua ile dhana ya awali kuwa, hawakuwa na maadili. Kwa wananchi wao huko majimboni kwao, hawakuona kama maadili ni kitu muhimu kwao, kulinganisha na utumishi wa wawakilishi wao hao. Wapiga kura hao wameonyesha kujali zaidi uwezo wa wawakilishi wao kwao na si maadili ya kitaifa:
  • Edward Lowassa alipokelewa kishujaa kwao Monduli alipojiuzulu uwaziri mkuu Februari 2008.
  • Andrew Chenge alipokelewa kishujaa kwao Bariadi alipojiuzulu uwaziri wa miundombinu April 2008.
  • William Ngeleja alipokelewa kishujaa kwao Sengerema baada ya kujiuzulu uwaziri wa nishati na madini mwaka 2012.
  • Nape Nnauye alipokelewa kishujaa jimboni kwake Mtama hadi kupanda migongo ya akina mama baada ya kuondolewa uwaziri wa Habari mwaka 2017.
  • Mwigulu Nchemba alipokelewa kishujaa huko kwao Iramba mwaka huu 2018.
IMG_8464.JPG IMG_8462.JPG IMG_8463.JPG IMG_8461.JPG IMG_8460.JPG

Hayo yote ni tisa na cha mtoto tu. Kinachostaajabisha tabia ya Watanzania, ni namna ambavyo Wabunge na Madiwani waliojiuzulu na kuhamia CCM kutoka CHADEMA, walifanikiwa kurejesha nafasi zao tena ikionekana kwa urahisi zaidi kuliko walivyozipata nafasi hizo mwaka 2015. Katika jumla ya Kata zipatazo 188, ni mbili pekee zilizoenda CHADEMA huku nyingine zote zikichukuliwa na CCM. Katika Majimbo nane, yote yamerudi CCM.
IMG_6909.jpg

CCM ya Magufuli ime-revolutionize Siasa za Tanzania completely.

Nini kinachowafanya wananchi wawakubali tu kirahisi rahisi hivyo? Je hiyo haituonyeshi kuwa, somewhere something is still not yet right? Je, si kweli kuwa wananchi hawajali sana masuala ya kisiasa ya Vyama bali wanajali wagombea? Kama ni hivyo, mbona CCM inaendelea kushindwa kwa urahisi licha ya mara kadhaa Upinzani kuonekana kuwa na wagombea vijana na ambao mara nyingi wako smart upstairs kuliko wa CCM?
 
Ccm wanatakiwa kutafakari haya;
kama wanapendwa kwanini wanatumia 'nguvu kubwa sana' ili washinnde?
Bila mapolisi na nec kuwa upande wao kuna ushindi wa haki?
Nini ishara ya huko mbeleni?
 
Hapo upinzani wamekuja na gia mpya ukininunua shart nigombee mwenyewe tena yaani hapo kifupi ccm wanatawaliwa na upinzani ndani ya chama chao wenyewe
 
Tangu skendo kubwa kubwa za rushwa zianze kujitokeza nchini, hasa katika kipindi cha Utawala wa Awamu ya Nne, ambazo zilipekekea kujiuzulu kwa Viongozi wengi wa Serikali kusnzia Mawaziri, Makatibu Wakuu na Wanasheria wa Serikali, mpaka wenyeviti wa Kamati za Bunge. Hata hivyo, mara zote tuhuma hizo zimeonyesha kuwa, hazina umuhimu mkubwa kwa Watanzania linapokuja suala la maadili. Baadhi ya Viongozi waliotumbuliwa, walipokelewa kishujaa majimboni kwao na kuua ile dhana ya awali kuwa, hawakuwa na maadili. Kwa wananchi wao huko majimboni kwao, hawakuona kama maadili ni kitu muhimu kwao, kulinganisha na utumishi wa wawakilishi wao hao. Wapiga kura hao wameonyesha kujali zaidi uwezo wa wawakilishi wao kwao na si maadili ya kitaifa:
  • Edward Lowassa alipokelewa kishujaa kwao Monduli alipojiuzulu uwaziri mkuu Februari 2008.
  • Andrew Chenge alipokelewa kishujaa kwao Bariadi alipojiuzulu uwaziri wa miundombinu April 2008.
  • William Ngeleja alipokelewa kishujaa kwao Sengerema baada ya kujiuzulu uwaziri wa nishati na madini mwaka 2012.
  • Nape Nnauye alipokelewa kishujaa jimboni kwake Mtama hadi kupanda migongo ya akina mama baada ya kuondolewa uwaziri wa Habari mwaka 2017.
  • Mwigulu Nchemba alipokelewa kishujaa huko kwao Iramba mwaka huu 2018.
View attachment 868685View attachment 868683View attachment 868684View attachment 868682View attachment 868681

Hayo yote ni tisa na cha mtoto tu. Kinachostaajabisha tabia ya Watanzania, ni namna ambavyo Wabunge na Madiwani waliojiuzulu na kuhamia CCM kutoka CHADEMA, walifanikiwa kurejesha nafasi zao tena ikionekana kwa urahisi zaidi kuliko walivyozipata nafasi hizo mwaka 2015. Katika jumla ya Kata zipatazo 188, ni mbili pekee zilizoenda CHADEMA huku nyingine zote zikichukuliwa na CCM. Katika Majimbo nane, yote yamerudi CCM.
View attachment 868693
CCM ya Magufuli ime-revolutionize Siasa za Tanzania completely.

Nini kinachowafanya wananchi wawakubali tu kirahisi rahisi hivyo? Je hiyo haituonyeshi kuwa, somewhere something is still not yet right? Je, si kweli kuwa wananchi hawajali sana masuala ya kisiasa ya Vyama bali wanajali wagombea? Kama ni hivyo, mbona CCM inaendelea kushindwa kwa urahisi licha ya mara kadhaa Upinzani kuonekana kuwa na wagombea vijana na ambao mara nyingi wako smart upstairs kuliko wa CCM?
Mkuu ulicho kiandika ni zaidi ya ukweli ila wapo wabishi watakuja kutupa nawe upande
 
Back
Top Bottom