Mimi kila wiki sikosi kusoma magazeti manne -- Mwanahalisi, Raia Mwema, Kulikoni na Dira. Haya ndiyo magazeti "huru" kwa maana halisi ya neno katika mazingira yetu ya Tanzania na yamekuwa yakijitahidi kueleza ubayana ufisadi unaoendelea nchini.
Ila kama wadau wengine walivyogundua, gazeti la Mwanahalisi limepoteza mwelekeo katika kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja sasa na sielewi haswa hii inatokana na nini. Tatizo la Watanzania ni wavivu kufikiri na kufanya uchambuzi. Pia ni wepesi wa kupuuza mawazo, fikra au hoja mbadala.
Hauhitaji kuwa rocket scientist wa NASA kubaini kuwa kuna mdudu ameingia Mwanahalisi katika kipindi hiki cha sasa. Ila sielewi kama mmiliki wa hili gazeti sasa ameanza kuwaogopa kina RACHEL au kanunuliwa.
Ila kama wadau wengine walivyogundua, gazeti la Mwanahalisi limepoteza mwelekeo katika kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja sasa na sielewi haswa hii inatokana na nini. Tatizo la Watanzania ni wavivu kufikiri na kufanya uchambuzi. Pia ni wepesi wa kupuuza mawazo, fikra au hoja mbadala.
Hauhitaji kuwa rocket scientist wa NASA kubaini kuwa kuna mdudu ameingia Mwanahalisi katika kipindi hiki cha sasa. Ila sielewi kama mmiliki wa hili gazeti sasa ameanza kuwaogopa kina RACHEL au kanunuliwa.