Kijembe ambacho mmoja wa mapacha watatu wa ufisadi, Rostam Aziz Abdulrasul, alikirusha kwa Saed Kubenea kuwa anaweza kumnunulia mtambo wa kuchapishia gazeti lake la MwanaHalisi mapema mwaka huu, kimegeuka kuwa "azma iliyotimia" baada ya mwandishi huyo machachari aliyejizolea sifa kemkem kwa ujasiri kutiwa mfukoni na sasa ni sehemu ya majeshi ya Rostam ya kumlinda na kuwasambaratisha wabaya wake!
Kubenea ambaye mwaka juzi alishambuliwa na watu "wasiojulikana" na kumwagiwa tindikali machoni karibu apofuke, kasahau yote hayo na sasa ni silaha ya kuaminika ya Rostam katika kujihami dhidi ya kampeni kali ya CCM inayoongozwa na Katibu Mwenezi Taifa Nape Nnauye ili mkuu wake mpya Rostam abakie na gamba lake.
Taarifa za ndani kwenye duru za mwanahabari huyo zinasema kijembe kile cha kumnunulia Kubenea mtambo wa kuchapishia magazeti kimefanyiwa kazi na Kubenea yuko mbioni kupata mtambo mpya wa kisasa lakini kwa sharti la kuachana na habari hasi za Rostam na Lowassa kwenye gazeti lake na kuendesha kampeni kali dhidi ya msururu wa watu aliopewa katika miaka mitatu ijayo. Baadhi ya watu hao ni JK na familia yake, "Mtoto wa Mkulima", Magufuli, Chilligati, Nape, Sitta, Anne Kilango, Ole Sendeka, Lembeli, Mwandosya, Membe, Kinana, Mwakyembe, Mkuchika, Chatanda na Kigoda. Kubenea kakubali dili hilo ambalo tayari limemwingizia zaidi ya sh. milioni 20.
Gazeti la MwanaHalisi ambalo limekuwa kwa muda mrefu msumari wa moto kwa mapacha watatu wa ufisadi kutokana na Kubenea kuamini kwamba wawili kati ya mapacha hao watatu walihusika na mpango wa kumtoa roho au kumpa kilema cha maisha, halitabeba taarifa tena za Lowassa wala Rostam ila za wabaya wao hao.
Mathalan, toleo la kesho kutwa la MwanaHalisi tayari lina taarifa ndefu ya Daniel Porokwa akiwamwagia sumu "maadui" wa RA na EL bila kujali kuwa gazeti lake lilimwandika Porokwa mwaka jana kuwa kibaraka wa Lowassa baada ya kujitoa kugombea Ubunge jimbo la Monduli. Porokwa "alizawadiwa" kazi ya Katibu Msaidizi wa CCM wa Wilaya, gari mpya aina ya NOAH, shilingi milioni 2, na ng'ombe kadhaa baada ya kujisalimisha na kukubali Lowassa amkanyage kichwani kwa mila eti ya Kimasai kama siyo ya kishirikina.
Hizi ni habari za uzushi. Habari za uhakika nilizopata kwa mtu wa karibu na Kubenea ni kwamba mtambo wa kuchapa kisha nunua kutoka kwa Mengi -- ule wa zamani uliokuwa unatumika kuchapishia magazeti yake ya IPP media hadi 2006 aliponunua mpya. Mtambo huo ni mzima ingawa ni wa kizamani kidogo. Sijui bei aliyonunulia lakini nasikia ilikuwa ni bei rahisi tu kwa sababu Mengi na Kubenea wana uelewano mzuri kutokana harakati zao za vita dhidi ya mafisadi.
Kisha toa instalment moja na nyingine atalipa polepole pale atakapoanza kuchapisha magazeti yake na pengine ya wateja wengine. Hivi sasa yuko mbioni kutafuta mahal;i pa kuufunga.
Linganisha huyu kijana Kubenea na Habari Corporation kamopuni ya Rostamu -- nasikiavyo sasa hivi wanahangaika kupiga chapa magazeti yao, walikimbia Jamana kutokana na deni kubwa wakaenda Mwananchi ambako ni bei ghali sana. Nasikia wameshindwa na wamerudi tena Jamana bila aibu. Wakati huo huo nasikia wafanya kazi hawajalipwa mishgahara ya Aprili, na sasa Mai inamalizika.
mwehu uyo m/halisi ni taasisi iuzayo nakala nyingi sana sembuse kurubuniwa kwa sh 20mil...au ni dola
Gazeti linalouza nakala zaidi ya 70,000 kila wiki ataweza kweli kubenea kukosa milioni 20 hadi alambe miguu ya RA, mtu ambaye amekuwa anampiga vita kwa ufisadi wake?
WELL SAID! TAARIFA NI KWAMBA 'AWAMU YA KWANZA YA JMK, RA ALIOMBA AUZIWE HALIHALISI ILA SAEED ALIMKATALIA. RA WAS READY TO DISH OUT 900M+ TO BE A SHAREHOLDER BUT KUBENEA REFUSED, WHAT IS 20M THEN?' I THINK THERE'RE CERTAIN INDVDLS WHO DON'T TO B WRITTEN SO THEY'RE CREATING UPRONT SELF DEFENSE, WAZEE WA 'SI TULISEMA' KWIKW!
WanaJF, maandishi hayaozi. Mtoa mada ametuambia kuwa jumatano kutaandikwa habari za Porokwa na jumatano si mbali na hii thread huenda itakuwepo na kama haitakuwepo karibu tutaihuisha ili kujua ili kumsuta mtoa mada ama kumuona shujaa kwa kutupa habari za ndani. Tusimhukumu kwa sasa ila tusubiri jumatano tuone kisha ahukumiwe kama aliyoyasema hayatatokea. Jamani mafisadi si watu wa kuandermine wanaweza kufanya lolote they can turn a hero to a zero!!
Kijembe ambacho mmoja wa mapacha watatu wa ufisadi, Rostam Aziz Abdulrasul, alikirusha kwa Saed Kubenea kuwa anaweza kumnunulia mtambo wa kuchapishia gazeti lake la MwanaHalisi mapema mwaka huu, kimegeuka kuwa "azma iliyotimia" baada ya mwandishi huyo machachari aliyejizolea sifa kemkem kwa ujasiri kutiwa mfukoni na sasa ni sehemu ya majeshi ya Rostam ya kumlinda na kuwasambaratisha wabaya wake!
Kubenea ambaye mwaka juzi alishambuliwa na watu "wasiojulikana" na kumwagiwa tindikali machoni karibu apofuke, kasahau yote hayo na sasa ni silaha ya kuaminika ya Rostam katika kujihami dhidi ya kampeni kali ya CCM inayoongozwa na Katibu Mwenezi Taifa Nape Nnauye ili mkuu wake mpya Rostam abakie na gamba lake.
Taarifa za ndani kwenye duru za mwanahabari huyo zinasema kijembe kile cha kumnunulia Kubenea mtambo wa kuchapishia magazeti kimefanyiwa kazi na Kubenea yuko mbioni kupata mtambo mpya wa kisasa lakini kwa sharti la kuachana na habari hasi za Rostam na Lowassa kwenye gazeti lake na kuendesha kampeni kali dhidi ya msururu wa watu aliopewa katika miaka mitatu ijayo. Baadhi ya watu hao ni JK na familia yake, "Mtoto wa Mkulima", Magufuli, Chilligati, Nape, Sitta, Anne Kilango, Ole Sendeka, Lembeli, Mwandosya, Membe, Kinana, Mwakyembe, Mkuchika, Chatanda na Kigoda. Kubenea kakubali dili hilo ambalo tayari limemwingizia zaidi ya sh. milioni 20.
Gazeti la MwanaHalisi ambalo limekuwa kwa muda mrefu msumari wa moto kwa mapacha watatu wa ufisadi kutokana na Kubenea kuamini kwamba wawili kati ya mapacha hao watatu walihusika na mpango wa kumtoa roho au kumpa kilema cha maisha, halitabeba taarifa tena za Lowassa wala Rostam ila za wabaya wao hao.
Mathalan, toleo la kesho kutwa la MwanaHalisi tayari lina taarifa ndefu ya Daniel Porokwa akiwamwagia sumu "maadui" wa RA na EL bila kujali kuwa gazeti lake lilimwandika Porokwa mwaka jana kuwa kibaraka wa Lowassa baada ya kujitoa kugombea Ubunge jimbo la Monduli. Porokwa "alizawadiwa" kazi ya Katibu Msaidizi wa CCM wa Wilaya, gari mpya aina ya NOAH, shilingi milioni 2, na ng'ombe kadhaa baada ya kujisalimisha na kukubali Lowassa amkanyage kichwani kwa mila eti ya Kimasai kama siyo ya kishirikina.
majungu tu hana lolte huyu mtoa mada, yaani mwenzetu mpaka toleo lijalo ameshajuwa litaandika nini, kama si wehu huu tuuwitaje?
Kama ni kweli basi money can buy anything except peoples' power!!! Lakini nina wasiwasi mkubwa na mtoa mada hivi ni mtambo wa aina gani unaouzwa mil.20 labda tupe ufafanuzi kidogo!!