Kwanza nikusihi jambo moja: Heshimu watu ata kama huwapendi. Kumpenda au kumchukia mtu hakuwezi kumwondolea taaluma aliyonayo. Unaposema 'anayejiita Padri' una maana kuwa siyo padri, jambo ambalo siyo kweli. Dr. Slaa ni Padri kwa usomea fani hiyo na kutumikia kanisa kwa kazi ya upadri. Huwezi kufuta ukweli huo na taaluma ya upadri imo kichwani mwake hata kama ungemnyang'anya cheti chake. Kuna madaktari 63%ya waliohitimu fani ya udaktari, lakini bado wanatambulika kama madaktari.
Pili umesema 'mgombea urais katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu' Siyo kweli, hakuwahi hata kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa na chama chake wala chama chake hakijawahi kupitisha jina lake na kulipeleka Tume ya uchaguzi (NEC). Wewe kama mwandishi wa habari (sina hakika kama ni kweli) hupaswi kuegemea upande, hupaswi kutumia fani yako kupambana na wanajamii ukitumia uandishi wako wa habari. Once biased huwezi kuandika habari kitaaluma.
Azungumzie na tuhuma za kumwagiwa tindikali ofisini, lakini mambo ya Slaa na mkewe ni upuuzi kweli kweli. Akishamaliza apotee kwani hakuna suala hata moja linalomgusa. Tunataka Lowassa na wafuasi wake kina Mbowe na Lissu wazungumze. Kubenea ni mnafiki wa kutupa
NIMEMSIKILIZA kwa makini, Dk. Willibroad Slaa, aliyekuwa katibu mkuu wa Chadema na mgombea urais katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.
Akihojiwa na kituo cha televisheni cha Star TV, Dk. Slaa alimtuhumu Edward Lowassa kuwa ni fisadi na akataka wananchi kumchagua mgombea mwenye nafuu ya ufisadi. Akamtaja John Pombe Magufuli.
Ameeleza pia kuwa taarifa mpya aliyonayo na ambayo aliitumia katika mkutano wake na waandishi wa habari Jumanne iliyopita, kuhusu sakata la Richmond, aliipata kutoka kwa Dk. Harrison Mwakyembe, aliyekuwa mwenyekiti wa kamati Teule ya Bunge, juu ya Richmond.
Niliamua kutojibizana na Dk. Slaa rafiki yangu wa miaka mingi katika mradi wake huu. Lakini kwa hapa alipofika, uvumivu umenishinda. Sitaruhusu mtu mzima, anayejiita padri na ambaye alitaka kuwa rais wetu, kuendelea kulindanganya taifa na kuwapotosha wananchi.
Hivyo basi, nimeamua kuanzia leo hii, kukabiliana na Dk. Slaa kwa kila kona ili ukweli ufahamike. Kwa kuanzia, leo hii Jumamosi, naelekea mkoani Mbeya ambako nitahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara katika jimbo la Kyera, linaloshikiliwa na Mwakyembe, swahiba mpya wa Dk. Slaa.
Nikiwa Mbeya nitaeleza ukweli wa kilichotokea na kile ambacho Dk. Slaa anakificha.
Aidha, nikirejea Dar es Salaam, nimepanga kuitisha mkutano na waandishi wa habari, kueleza ukweli uliokamilika kuhusu Dk. Slaa na mkewe Josephine Mushumbuzi na sababu
NIMEMSIKILIZA kwa makini, Dk. Willibroad Slaa, aliyekuwa katibu mkuu wa Chadema na mgombea urais katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.
Akihojiwa na kituo cha televisheni cha Star TV, Dk. Slaa alimtuhumu Edward Lowassa kuwa ni fisadi na akataka wananchi kumchagua mgombea mwenye nafuu ya ufisadi. Akamtaja John Pombe Magufuli.
Ameeleza pia kuwa taarifa mpya aliyonayo na ambayo aliitumia katika mkutano wake na waandishi wa habari Jumanne iliyopita, kuhusu sakata la Richmond, aliipata kutoka kwa Dk. Harrison Mwakyembe, aliyekuwa mwenyekiti wa kamati Teule ya Bunge, juu ya Richmond.
Niliamua kutojibizana na Dk. Slaa rafiki yangu wa miaka mingi katika mradi wake huu. Lakini kwa hapa alipofika, uvumivu umenishinda. Sitaruhusu mtu mzima, anayejiita padri na ambaye alitaka kuwa rais wetu, kuendelea kulindanganya taifa na kuwapotosha wananchi.
Hivyo basi, nimeamua kuanzia leo hii, kukabiliana na Dk. Slaa kwa kila kona ili ukweli ufahamike. Kwa kuanzia, leo hii Jumamosi, naelekea mkoani Mbeya ambako nitahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara katika jimbo la Kyera, linaloshikiliwa na Mwakyembe, swahiba mpya wa Dk. Slaa.
Nikiwa Mbeya nitaeleza ukweli wa kilichotokea na kile ambacho Dk. Slaa anakificha.
Aidha, nikirejea Dar es Salaam, nimepanga kuitisha mkutano na waandishi wa habari, kueleza ukweli uliokamilika kuhusu Dk. Slaa na mkewe Josephine Mushumbuzi na sababu
Upadre ni wito siyo fani,umbea usipitilize ndugu.
Huwezi kuwa padri bila kusomea miaka 6. Unaweza kuitwa kama hukufaulu huwezi kuwa padri. Makanisa ya wokovu ndiyo watu walikuwa wanajiingiza tu kwa kisingizio cha wito siyo Upadri
Tanzania ya sasa haitaki watu, vigeugeu na wasio na misimamo kama kubenea wanasiasa njaa.