Hivi zile voices of reason ndani ya Chadema zimekwenda wapi? Sitaki kum-hold Lowassa kuwa ndio sababu ya kupotea kwa busara ndani ya chama hicho, ambacho kabla ya ndoa ya Ukawa na baadae ujio wa Lowassa, kilikuwa chama kikuu cha upinzani.
Kubenea ana haki ya kikatiba kufanya lolote apendalo lakini haihitaji busara japo kidogo kuwa he has more to gain kwa ku-focus katika kibarua kinachomkabili kwenye jimbo analowania ubunge kuliko hayo malumbano anayotaka kuyaanzisha dhidi ya Dkt Slaa. Suppose akishinda malumbano hayo kisha akapoteza ubunge, kipi kitakuwa na faida?
Ninachokiona sasa ndani ya Chadema/UKAWA ni ukosefu wa strategy ya ku-deal na Slaa. Mara huyu kasema hili, yule kasema lile, muda unakwenda. Ni muhimu kutambua kuwa Dkt Slaa si mgombea ubunge au urais. Muda wowote unaopotezwa kulumbana nae unawaathiri zaidi Chadema/UKAWA kuliko yeye. He has got nothing to lose (ameshapoteza nafasi yake ya uongozi, anyway) but akina Kubenea na Chadema/UKAWA have got everything to lose.
Kama Kubenea, Chadema au UKAWA wanaamini kuna upotoshaji wa makusudi unaofanywa na Dkt Slaa, suluhisho sio kubishana nae kwenye majukwaa ya kuombea kura (I repeat yeye si mgombea wa nafasi yoyote) bali MAHAKAMANI.Chadema ina mawakili kadhaa wasomi: Marando, Prof Safari, Lissu,nk. Kwanini wasomi hawa wasishughulikie tatizo hili kisheria kama wanaamini kuna kosa linafanyika?
Wasiwasi wangu ni kwamba Chadema inajitwisha mzigo isiostahili: wakati jukumu la kumsafisha Lowassa halijakamilika, wanajitwisha mzigo mwingine wa kumchafua Dkt Slaa. Busara zatukumbusha kuwa MSHIKA MAWILI MOJA HUMPONYOKA. Wanaweza kushinda katika kumchafua Dkt Slaa, lakini wakafeli kushinda uchaguzi (najua kuna wengi hawataki hata kusikia neno KUSHINDWA japo wanatambua sio tu na CCM ileile inayoshinda 'kimiujiza' kila uchaguzi bali wanashiriki uchaguzi ilio katika mfumo uleule unaoiwezesha CCM kushinda kiurahisi)
Kuna yeyote anayetambua kuwa (a) katika uchaguzi kuna kushinda au kushindwa (b) there's life after the election? Priority kwa sasa iwe katika kushinda uchaguzi, lakini with a realisation kuwa iwapo kura hazitotosha, Chadema shurti iendelee kuwa hai, unless imani ya mabadiliko ina lifespan isiyozidi Oktoba 2015.
Sitarajii ushauri huu kusikilizwa kwa sababu inaelekea wengi wetu tumeamua kutanguliza emotions in front of common sense, and that's quite dangerous.