Kuanguka kwa CCM: Kutimilika kwa Unabii...

Hata Mwigulu alishasema ana ushaid hadi sasa hajautoa,MM ameshamaliza kabisa.lisemwalo lipo kama halipo laja.
mark my words too.
 
Hilo la kutokea machafuko limekuwa linatumiwa sana na ccm, kwa bahati mbaya kipindi hiki habari zinapatikana kwa urahisi zaidi hivyo upotoshaji watu eti kwa kisingizio cha kuwepo machafuko upinzani ukipewa madaraka hauna mashiko!

na CCM wametumia swala la kuwatishia wananchi kwa kudhani watanzania ni wa mwaka arubaini na saba(1947 )baada ya vita vya pili vya dunia maana dunia yote ilikuwa inaogopa vita na something that relating to that
 
Wakuu

heshima kwenu........


Iko siku ambapo Watanzania wataamka na
watakuta kwamba Chama cha Mapinduzi
hakishiki tena hatamu za uongozi wa nchi, na
badala yake Ikulu na Bunge vimechukuliwa na
chama kingine. Siku hiyo ambayo haina jina,
itakuwa ni siku ambapo Chama cha Mapinduzi
kitaanguka kwa kishindo kikuu na sauti ya
kuanguka kwake itasikika kila kona ya
Tanzania, na mwangwi wa kuporomoka kwake
kurindima katika bara letu la Afrika na
mabaki ya mtetemo wa kuvunjikavunjika
kwake kusimuliwa kama hadithi za Alfu Leyla
wa Uleyla kwa vizazi vijavyo vya Watanzania.

Kuanguka kwa Chama cha Mapinduzi
kutakuwa ni mwanzo wa msemo, na bila ya
shaka kutatungiwa methali.

Siku hiyo ni siku ambayo kina Malecela,(jumanne) kinana mangula nape mgwillu
Msuya, Kingunge, Kikwete,Lowassa,Maka-
mba,Karume na magwiji wengine wa Chama
hicho waombee wasijeiona.

Kwani itakuwa ni
siku ya huzuni kwa watawala "watalia na kusaga meno" na furaha kwa
watawaliwa! Itakuwa ni siku ambapo “nyota
ya jaha” itaangazia Taifa letu na nuru ya
“jua la haki” itachomoza na miale yake
kumulika kila kona ya Taifa letu.

Hiyo ni siku
ambayo kama mwali atolewaye nje, kila mtu
atatamani kuiona isipokuwa wale ambao huyo
mwali ni ishara ya wao kukosa mke na
wengine kupata!

Bila ya shaka unajiuliza iweje nianze kwa
kusema maneno hayo. Nilikuwa natafakari
maneno ya Mwalimu aliyoyatoa mwanzoni
mwa miaka ya 90 mara baada ya vyama vingi
kuruhusiwa tena nchini. Baada ya Mwalimu
Nyerere kutoa maneno makali ya “Ikulu
inanuka Rushwa” watu wengi walianza
kujiuliza mapenzi ya Mwalimu kwa chama
alichokiasisi na kama anaweza kujitoa kwenye
chama hicho. Alipoulizwa kuhusu kujiondoa
CCM, mwalimu alijibu “CCM siyo Mama yangu”.
Maneno hayo ya Mwalimu yamebakia
mawazoni mwangu (na bila shaka ya wengine
pia) kama unabii na kama wosia.

Hii leo kuna
baadhi ya viongozi wa Chama tawala ambao
wanasisitiza maneno ya Mwalimu ya “Bila CCM
madhubuti Tanzania Itayumba” na kusahau
kabisa maneno hayo ya onyo kali kuwa hata
kama mtu ana mapenzi kiasi gani na CCM, iko
siku anaweza kukiacha na kujitahidi
kukivunja! Ni rahisi kukiacha CCM kuliko
kumuacha Mama mzazi!

Siku hiyo ambapo Chama hiki maarufu
kitakapojikuta kiko katika kambi ya upinzani
ndipo viongozi wake na mashabiki wake
watakapotambua kuwa “CCM siyo Mama” na
Tanzania itaendelea na inaweza kuwepo bila
CCM kuwa madarakani! Hiyo siku isiyo na jina,
iko, yaja, na yafanya hima kufika! Kwanini
basi CCM itakuja kuanguka kwa mshindo mkuu
namna hiyo?


Ndugu zangu, punda mnyama wa kazi kuna
mahali anafikia kikomo! Na akifikia kikomo,
punda hendi hata kwa mijeredi mia. Mtu
unaweza kumtwisha punda mizigo, lakini
akifikia kikomo chake hata umfanye nini
punda hanyanyui mguu.

Kuna baadhi ya
viongozi ambao wanadhani kuwa Watanzania
wataendelea kuinama na kukubali kutwishwa
mizigo ya kila namna kana kwamba hawasikii
maumivu! Ni hawa viongozi ambao huendelea
kutuingiza katika mikataba mibovu,
wanaendelea kuvumilia ufujaji wa mali ya
umma katika maofisi yao, wanaendelea
kupuuzia rushwa hadi imezoeleka na
kuonekana kama kawaida. Viongozi hawa
wanaimba wimbo na pambio ya uongozi bora
wakitumbuiza kwa kasida za maneno ya
kizalendo.

Mawazoni mwao wanaishi wakifikiri
kwamba Watanzania wataendelea kuvumilia.
Kama punda iko siku hugoma, iko siku
Watanzania nao watasema “Sasa inatosha”

siku hiyo yaja na haiko mbali
TUTAHESHIMIANA TU
 
ccm wataangamia wote bila kuamini itakuwa kama ilivyo ngumu kuamini kama ile meli ya TITANIC ingezama kutokana na ukubwa wake pamoja watu waliokuwepo ndani yake lakini ilizama mpaka watu hawajaamini ccm itakufa kifo hicho na watu hawataamini lakini ndo itakuwa hivyo UONEVU una mwisho wake muda wa ukombozi umeshakaribia
View attachment 187457




MUNGU IBARIKI TANZANIA
MUNGU IBARIKI CHADEMA
 
ccm wataangamia wote bila kuamini itakuwa kama ilivyo ngumu kuamini kama ile meli ya TITANIC ingezama kutokana na ukubwa wake pamoja watu waliokuwepo ndani yake lakini ilizama mpaka watu hawajaamini ccm itakufa kifo hicho na watu hawataamini lakini ndo itakuwa hivyo UONEVU una mwisho wake muda wa ukombozi umeshakaribia
View attachment 187457




MUNGU IBARIKI TANZANIA
MUNGU IBARIKI CHADEMA

pamoja sana kamanda
 
Leo Nimeota CCM imeng'olewa madarakani na Umoja Wa Katiba Ya Wananchi (UKAWA).Wananchi walijitokeza kwa wingi kwenda kupiga kura.Baada ya matokeo ya awali kuanza kuonyesha CCM ina hali mbaya na UKAWA kuonekana kuwa tishio,kama kawaida yao CCM wakaanza mbinu zao chafu za kutaka kutumia mabavu kuchakachua matokeo lakini mawakala wa UKAWA na wafuasi wao walisimama kidete kuhakikisha matokeo hayachakuchuliwi na CCM,baada ya kushindikana kwa hila hiyo ikabidi kwa shingo upande Tume ya Uchaguzi ianze kutangaza matokeo rasmi,lakini kadri matokeo yalivyozidi kutangazwa ndivyo CCM ilivyozidi kugaragazwa na UKAWA katika nafasi zote za Wagombea kuanzia Urais,Wabunge na Madiwani.Baada ya CCM kuona matokeo yamewaendea ndivyo sivyo,wakailazimisha Tume ya Uchaguzi kusitisha kuutangaza matokeo kwa kisingizio kwamba kuna baadhi ya maeneo yalikiuka kanuni na taratibu za uchaguzi hivyo matokeo yaliyotangazwa yatafutwa na kuhesabiwa upya.Wananchi kusikia hivyo nao hawakukubali,wakaiingia mitaani kuandamana na kuipinga serikali kwa hatua yake ya kubatilisha matokeo,serikali kuona wananchi wanaandamana ikawapeleka askari polisi mitaani kwenda kuwadhibiti wananchi,safari hii wananchi hawakukimbia kwani walijiandaa hasa kupambana na lolote lile litakalo kuja mbele yao.Mapambano kati ya wananchi na polisi yakaanza,polisi wakitumia silaha za moto na wananchi wakitumia kila aina za silaha za jadi,polisi wakazidiwa kwani wananchi walikuwa wakiongezeka makundi kwa makundi,likaitwa jeshi la wananchi kusaidia kudhibiti wananchi walioamua kulinda na kutetea haki yao inayotishiwa kuporwa na Watawala.Lakini wananchi hawakurudi nyuma,sasa ikawa vita kamili,wananchi wakaanza kuvamia vituo vya polisi na baadhi ya kambi na kupora silaha,hali ikawa mbaya sana,baadhi ya wanajeshi na polisi wakaanza kuasi na kuungana na wananchi,CCM na baadhi ya wanausalama wake watiifu wakazidiwa na kuamua kukimbia nchi.Hatimaye UKAWA wakaitwaa nchi. Na Ndoto yangu ikaishia hapo.
 
Nimeipenda hii ndoto.....
Ila ingekuwa mimi ndo ninayeota ningeota CCM ishindwe moja kwa moja na ikubali matokeo bila kulazimisha ghasia baina ya polisi na wananchi!!

Tunawahitaji polisi na zaidi ya yote tunawahitaji wananchi wakiwa na afya zao!!
 
Leo Nimeota CCM imeng'olewa madarakani na Umoja Wa Katiba Ya Wananchi (UKAWA).Wananchi walijitokeza kwa wingi kwenda kupiga kura.Baada ya matokeo ya awali kuanza kuonyesha CCM ina hali mbaya na UKAWA kuonekana kuwa tishio,kama kawaida yao CCM wakaanza mbinu zao chafu za kutaka kutumia mabavu kuchakachua matokeo lakini mawakala wa UKAWA na wafuasi wao walisimama kidete kuhakikisha matokeo hayachakuchuliwi na CCM,baada ya kushindikana kwa hila hiyo ikabidi kwa shingo upande Tume ya Uchaguzi ianze kutangaza matokeo rasmi,lakini kadri matokeo yalivyozidi kutangazwa ndivyo CCM ilivyozidi kugaragazwa na UKAWA katika nafasi zote za Wagombea kuanzia Urais,Wabunge na Madiwani.Baada ya CCM kuona matokeo yamewaendea ndivyo sivyo,wakailazimisha Tume ya Uchaguzi kusitisha kuutangaza matokeo kwa kisingizio kwamba kuna baadhi ya maeneo yalikiuka kanuni na taratibu za uchaguzi hivyo matokeo yaliyotangazwa yatafutwa na kuhesabiwa upya.Wananchi kusikia hivyo nao hawakukubali,wakaiingia mitaani kuandamana na kuipinga serikali kwa hatua yake ya kubatilisha matokeo,serikali kuona wananchi wanaandamana ikawapeleka askari polisi mitaani kwenda kuwadhibiti wananchi,safari hii wananchi hawakukimbia kwani walijiandaa hasa kupambana na lolote lile litakalo kuja mbele yao.Mapambano kati ya wananchi na polisi yakaanza,polisi wakitumia silaha za moto na wananchi wakitumia kila aina za silaha za jadi,polisi wakazidiwa kwani wananchi walikuwa wakiongezeka makundi kwa makundi,likaitwa jeshi la wananchi kusaidia kudhibiti wananchi walioamua kulinda na kutetea haki yao inayotishiwa kuporwa na Watawala.Lakini wananchi hawakurudi nyuma,sasa ikawa vita kamili,wananchi wakaanza kuvamia vituo vya polisi na baadhi ya kambi na kupora silaha,hali ikawa mbaya sana,baadhi ya wanajeshi na polisi wakaanza kuasi na kuungana na wananchi,CCM na baadhi ya wanausalama wake watiifu wakazidiwa na kuamua kukimbia nchi.Hatimaye UKAWA wakaitwaa nchi. Na Ndoto yangu ikaishia hapo.


kaka ndoto yako sio sawa,hawa jamaa wameshajipanga vizuri sana,na kwa kifupi hii ya kujiandikisha kwa kutumia BVR ni bao la kisigino,hapo mtasubiri sana nawahakikishieni,tuna wanasheria mbumbu sana tanzania,ukitaka kujua tuko nyuma kwa asilimia ngapi angalia jirani zetu wa kenya wanavyofanya wako njema mbaya na hawafanyi makosa kabisa,hata kama ni rais amekosea anashtakiwa mahakamani
 
Nimeipenda hii ndoto.....
Ila ingekuwa mimi ndo ninayeota ningeota CCM ishindwe moja kwa moja na ikubali matokeo bila kulazimisha ghasia baina ya polisi na wananchi!!

Tunawahitaji polisi na zaidi ya yote tunawahitaji wananchi wakiwa na afya zao!!
Jitahidini kuweka kumbukumbu zenu sawa ili siku ikifika tuweze kukumbushana mtapata aibu kweli siku ikifika msijifike.
 
mmm! Noma sana mwaka huu nawaomba polisi wackubal kutumika kisiasa kwani watachinjwa sana watu hawaogopi kwa sasa wanataka mabadiliko

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom