Kuacha mwanamke kisa amekuudhi, utaacha wangapi?

Kuacha mwanamke kisa amekuudhi, utaacha wangapi?

figganigga

Platinum Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
26,715
Reaction score
59,251
Habari wakuu,

Mimi sikubaliani na kitendo cha kumuacha mwanamke unayempenda kisa kakulet down au kakukwaza kwa namna moja ama nyingine.

Kila mwanamke ana maudhi yake. Kikibwa na kumchagua mmoja ambaye unaweza vumilia madahifu yake. Hakuna mkamilifu hata mmoja.

Ukisema kila anayekukatisha tamaa unamuacha, utajikuta umetongoza dunia.

Nakubaliana na usemi mwanamke kaa naye kwa akili si kwa maguvu na ubabe. Jifanye mjinga siku ipite. Kumbuka Mke ni baraka na heshima ndani ya nyumba. Tukosoane kwa upendo na heshima. Mia
 
Kwahiyo ww hujawahi kuacha wala kuachwa?!
 
Sidhani kama kakuudhi mara moja ndo lije wazo la kuachana!
Huwa linapokuja suala la kuachana ni uvumilivu huwa unafika mwisho.

Lakini kama kakosa mara ya kwanza kuna kuongea na kuweka mambo sawa! Kuna wengine hutumia fursa ya upendo kuwaumiza wengine na hii ipo kwa pande zote mbili.

Kwenye mapenzi mikwaruzano ipo sana na mara nyingi huwa inaimarisha mahusiano lakini yale ya kumuumiza mwingine kisa tuu unajua anakupenda hiyo ni HAPANA, utavumilia utachoka moyo wenyewe ndo huamua kwamba hapa basi, yaani yatoshaaa!!
 
Sijaoa bado mkuu, ila siamini katika wanawake kuwa bora zaidi ya mwingine. Huwa wanatengenezwa. Ndo maana unakuta kicheche anaolewa anakuwa na tabia njema kuliko mlokole. Unavyomtreat ndivyo anavyokuwa.

Sijakuuliza kuhusu kuoa...mada ya yako inasema mambo ya kuacha hujasema kama kwny ndoa au la
 
Sidhani kama kakuudhi mara moja ndo lije wazo la kuachana!
Huwa linapokuja suala la kuachana ni uvumilivu huwa unafika mwisho.

Lakini kama kakosa mara ya kwanza kuna kuongea na kuweka mambo sawa! Kuna wengine hutumia fursa ya upendo kuwaumiza wengine na hii ipo kwa pande zote mbili.

Kwenye mapenzi mikwaruzano ipo sana na mara nyingi huwa inaimarisha mahusiano lakini yale ya kumuumiza mwingine kisa tuu unajua anakupenda hiyo ni HAPANA, utavumilia utachoka moyo wenyewe ndo huamua kwamba hapa basi, yaani yatoshaaa!!
Umeandika point. Hongera sana malaika wa nguvu.
Umemaliza kila kitu sina cha kuchangia
 
Sidhani kama kakuudhi mara moja ndo lije wazo la kuachana!
Huwa linapokuja suala la kuachana ni uvumilivu huwa unafika mwisho.

Lakini kama kakosa mara ya kwanza kuna kuongea na kuweka mambo sawa! Kuna wengine hutumia fursa ya upendo kuwaumiza wengine na hii ipo kwa pande zote mbili.

Kwenye mapenzi mikwaruzano ipo sana na mara nyingi huwa inaimarisha mahusiano lakini yale ya kumuumiza mwingine kisa tuu unajua anakupenda hiyo ni HAPANA, utavumilia utachoka moyo wenyewe ndo huamua kwamba hapa basi, yaani yatoshaaa!!
Umeongea sahihi. Tatizo linakuja pale mtu anapoona ni fedheha kujishusha kwa mke wake ili mambo yaishe. Unakuta anasema nenda, kwani mwanamke ni wewe peke yako? Sidhani kama ni sahihi. Ni vizuri kutengeneza kile ulicho nacho.

Natambua. Mjusi ukimkimbiza sana anageuka nyoka na kuanza kukukimbiza.

Kuna wengine wanatumia fimbo ya kupendwa kuwanyanyasa wale wanaowapenda. Ila bado nasisitiza, jitahidi kadiri ya uwezo wako kuyaokoa mapenzi kabla ya kuanza kufikiria penzi la pili.

Yaani usimuache mke wako sababu kuna wanawake wengine. Bali muache sababu umejitahidi kila namna kuokoa penzi umeshindwa. Unamkabidhi Mungu.
 
Sijakuuliza kuhusu kuoa...mada ya yako inasema mambo ya kuacha hujasema kama kwny ndoa au la
Ndio mkuu, sipendi tabia ya kukaa na mtu mwaka halafu unamuacha kisa kakuudhi au kakulet down. Nashauri kama kweli unaona anakufaa mvumilie zaidi ya chochote. Ila nlichogundua.. Kuanza kufanya ngono kabla ya ndoa ndo kinapelekea penzi kuchuza na kumuona mwenzio si chochote si lolote.
 
Wanawake wakishaingia kwenye mahusiano wana penda kutengeneza mazingira ya kugombana unaweza kuwa na rafki wa kike ata miaka mitatu bila kugombana jaribu sasa kuingiana kweny mahusian wiki mbili tayari mshaanza kununiana
Mara nyingi inasababishwa na wivu. Nakuhakikishia, ukiwa muwazi kwa mpenzi wako hakutakuwa na ugomvi wa mara kwa mara. Ugomvi mwingi unasabishwa na wivu anajaribu kulinda mali yake isiibiwe. Ugomvi mwingi ni wa kimapenzi.

Mpenzi wako akikuambia acha kuongea na mtu fulani acha. Wamejaliwa uwezo wa kujua yajayo kabla hayajatokea. Mara nyingi utajifanya mtakatifu lakini huwa machale yanawacheza sana.

Muhimu ni kumsikiliza na kumheshimu.
 
Umeongea sahihi. Tatizo linakuja pale mtu anapoona ni fedheha kujishusha kwa mke wake ili mambo yaishe. Unakuta anasema nenda, kwani mwanamke ni wewe peke yako? Sidhani kama ni sahihi. Ni vizuri kutengeneza kile ulicho nacho.

Natambua. Mjusi ukimkimbiza sana anageuka nyoka na kuanza kukukimbiza.

Kuna wengine wanatumia fimbo ya kupendwa kuwanyanyasa wale wanaowapenda. Ila bado nasisitiza, jitahidi kadiri ya uwezo wako kuyaokoa mapenzi kabla ya kuanza kufikiria penzi la pili.

Yaani usimuache mke wako sababu kuna wanawake wengine. Bali muache sababu umejitahidi kila namna kuokoa penzi umeshindwa. Unamkabidhi Mungu.
Kuna baadhi ya wanaume huwa wanafikiri jukumu la kuijenga ndoa ni la mwanamke pekee, halafu ukiona mwanaume anakimbilia kusema tuachane jua ashakukinai tayari na zaidi ana mwingine wa nje!

Kuna kukosea, kuna kurekebishana na kuelekezana pia! Neno NISAMEHE huwa linabeba mengi sana!! Watu hawajuagi tuu!!
 
Habari wakuu,

Mimi sikubaliani na kitendo cha kumuacha mwanamke unayempenda kisa kakulet down au kakukwaza kwa namna moja ama nyingine.

Kila mwanamke ana maudhi yake. Kikibwa na kumchagua mmoja ambaye unaweza vumilia madahifu yake. Hakuna mkamilifu hata mmoja.

Ukisema kila anayekukatisha tamaa unamuacha, utajikuta umetongoza dunia.

Nakubaliana na usemi mwanamke kaa naye kwa akili si kwa maguvu na ubabe. Jifanye mjinga siku ipite. Kumbuka Mke ni baraka na heshima ndani ya nyumba. Tukosoane kwa upendo na heshima. Mia
Kwani inamaana wao KAZI YA NI KIUUDHI TU??
 
Yani Mimi tutavumiliana tu kukosea kupo na kupishana kauli kupo, kosa kubwa atakalofanya tuachane achepuke halafu nijue taraka Tatu zitamuhusu na naoa mwingine.
 
Kuna baadhi ya wanaume huwa wanafikiri jukumu la kuijenga ndoa ni la mwanamke pekee, halafu ukiona mwanaume anakimbilia kusema tuachane jua ashakukinai tayari na zaidi ana mwingine wa nje!

Kuna kukosea, kuna kurekebishana na kuelekezana pia! Neno NISAMEHE huwa linabeba mengi sana!! Watu hawajuagi tuu!!
Mwanaume hakinahiwi na mwanamke. Wala mwanaume hajuagi kuacha mwanaume. Unaweza ukaachana na mwanaume kwa maneno mabaya na kashifa lakini mkija kuonana lazima atakuomba mchezo.

Hiyo kusema hakutaki anakuwa anatikisa kiberiti huku moyoni akiomba usiondoke. Ndo maana walio wengi baada ya muda wataanza kuomba msamaha utafikir walikuwa sio wao.

Kuliko kujifanya unamuacha unayempenda kisa wamawake wengine, ni garama na mateso kuliko kijishusha na kumaliza tatizo.

Hii nmeigundua baada ya kukua. Zamani nlikua sijali wala sibabaiki kumuacha mwanamke nikaja kugundua si suruhisho. Ndo sababu ya hii thread. Ndo maana mababu zetu ukiwauliza mumefikaje hapa hawatakujibu tulipendana sana bali watakuambia tumevumiliana sana na kusameheana.
 
Kwani inamaana wao KAZI YA NI KIUUDHI TU??
Hapana, hata wao wanatuvumilia mengi. Wanawake nao kuna ambao hawajatulia, yaani bila mwanaume wa pembeni hana amani. Lakini nimegundua wengi wanaharibiwa na marafiki.
 
Nawapenda Sana waislam, japo mie mkristo :
1.Talaka moja = Sikutaki ww mwanamke
2.Talaka mbili = Sikutaki ww na Familia yako
3.Talaka 3= Sikutaki ww na ukoo wako wote...
 
Yani Mimi tutavumiliana tu kukosea kupo na kupishana kauli kupo, kosa kubwa atakalofanya tuachane achepuke halafu nijue taraka Tatu zitamuhusu na naoa mwingine.
Mwanaume yoyote si rahisi kivumilia umalaya. Yaani mwanaume akufamanie akuvumilie yataka moyo ila mambo mengine ni rahisi. Hadi anagawa uchi kwa mtu mwingine huyo sio mpenzi wako bali mpenzi wenu. Anaweza akafanya umkolohee sumu afe. Ikifika hapo pa kumpanulia miguu mwanaume mwingine, atakayetoa ushauri ni Mungu na Malaika zake. Si kwa ushawishi wa kibinadamu.
 
Nawapenda Sana waislam, japo mie mkristo :
1.Talaka moja = Sikutaki ww mwanamke
2.Talaka mbili = Sikutaki ww na Familia yako
3.Talaka 3= Sikutaki ww na ukoo wako wote...
Una uhakika ndo inavyotafsiri? Waislam wamejiwekea misingi mizuri ya ndoa. Haileti migogoro kama unafuata dini.

Mzee naomba usaidie hapa. Mafundisho yanasemaje?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom