NAMTUMBA
JF-Expert Member
- Feb 20, 2014
- 1,939
- 594
Hali ni mbaya. Wakati Malipo ya korosho hakuna kinachoeleweka mpaka sasa viongozi wa vyama vya ushirika wanapigwa ili wataje majina ya Kangomba. Wanakamatwa, wanafungwa kisha wanapigwa na wanapewa vikaratasi ili kila kiongozi analazimishwa aandike majina matano au zaidi ya kangomba.kwasasa sio ukaguzi tena, wanaandikisha majina kwablazima. Hatakama viongozi hawajui majina kinafuata ni kipigo kikali, wanarushwa kichurachura, wanafagia boma lote, wanatishwa, na mateso ya kila namna hadi kila mmoja aandike majina matano ndo wanaachwa. Lengo lao kupunguza idadi ya wakulima ili walipwe watu wachache.
Chomachoma in nani?
Hapa kuna makundi kama manne hivi.
1. Kundi la kwanza la chomachoma ni wajasiriamali ambao wanakopesha pembejeo wakulima. Pembejeo kama vile madawa, vifaa vya kupuliza madawa, na pesa tasilimu kwa ajili ya mkulima kuhudumia shamba kwa palizi na mambo mengine kwa makubaliano ya kulipwa kipindi ambapo korosho itakuwa zimezaa. Mikopo hii wanakopeshwa mienzi kama nane kabla ya msimu wa mavuno kwakuwa wanakopeshana mwezi wa march na April, hivyo pesa ya huyu mjasiriamali ambae anaitwa kangomba pesa yake inakaa kwa mkulima kwamiezi nane au zaidi. Ni aina ya mkopo ambao hata benki hawawezi kukopesha mkulima. Lakini chomachoma yeye ana take risk pesa yake inakaa kwa mkulima kwa miezi nane, lakini pia kipindi hiki chote chomachoma anakuwa anapeleka marejesho benki kwa kutumia vyanzo vingine vya mapato ukizingatia chomachoma wengi ni wale wenye maduka na biashara zingine hivyo wanakuwa na sifa za kukopesheka benki tofauti na mkulima ambae hana sifa za kukopa benki hivyo kimbilio pekee la mkulima ni kwenda dukani kwa chomachoma kukopa pembejeo au pesa. Kumwambia chomachoma anadhulumu wakulima sio kweli huu ni onevu wa wazi. Ukimwondoa chomachoma kwenye mfumo huu ni kuumiza wakulima labda Kabla serikali haijamuondoa chomachoma lazima wakubali kukopesha wakulima kwa mfumo uleule wa chomachoma ambapo repayment inaanza miezi nane hadi kumi tangu siku ya kukopeshana. Na hili swala la kwamba mkulima anapewa riba kubwa ni hivi; Chomachoma anakopa benki kwa riba, nae ana kopesha mkulima kwa riba, hivyo ni automatically mkulima atalipa riba ambayo ni double. Chomachoma hawezi kukopa benki alafu yeye amkopeshe mkulima bila riba na ukizingatia repayment muda mrefu, ni haiwezekani. Serikali ikitaka kumuokoa mkulima kutokana na hiki kitanzi cha chomachoma lazima ikubali kuanzisha mfuko au benki maalumu kukokopesha wakulima at high risk kama chomachoma anavyokopesha.
2. Kundi la pili ni wajasiriamali ambao wanakopesha wakulima pesa tasilimu kwa kulipwa pesa kwa pesa au pesa kwa korosho. Hawa ndo wale wanatajwa kwamba wanakula maua. Lakini chanzo kikubwa cha mfumo huu ni bei kubwa ya pembejeo za kulimia korosho hivyo mkulima anashindwa kumudu garama na kuamua kutafuta vyanzo vya pesa za ziada zitakazomwenzesha kuhudumia shamba. Msimu wa mavuno ukifika mkulima anachukua kiasi kidogo cha korosho kulipa deni au kwa wale waliokubaliana kulipwa pesa kwa pesa hulipwa pesa kwa kadiri mikataba walivyokubaliana.
3. Kundi la tatu hawa wananunua korosho kabisa. Ingawa wanazunguka na mizani mashambani kununua korosho lakini maranyingi wakulima wenyewe ndo wanaenda na korosho zao kuziuza kwa chomachoma ili wapate pesa ya kujikimu. Na wanauza kiasi kidogo sana. Mfano kwa mkulima mwenye gunia hamsini za korosho anaweza kuuza kilo 50 hadi 100 kwa lengo la kutatua shida ndogondogo za nyumbani lakini mzigo mkubwa anapeleka galani kuikopesha serikali. Sio kweli kwamba mkulima anauza korosho zote kwa chomachoma, na sio kweli kwamba mkulima chomachoma wanadhulumu wakulima. Wakulima wanajitambua. Chomachoma wanatumia fursa hii kwakuwa serikali inachelewa kuwalipa wakulima hivyo kama ilivyo kwa wajasiriamali wa bidhaa zingine kama vile nyanya, vitunguu, mahindi nk. pia hawa wakorosho mfumo ni uleule wa bidhaa nyingine.
4. Kundi la nne hawa wanapewa mashamba na wakulima wenyewe iwapo mkulima ameshindwa kuhudumia hivyo kwa kuhofia shamba kuungua moto au mikorosho kwakukosa huduma anaamua kukodisha kwa mjasiriamali ambae anauwezo wakuhudumia shamba. Wanaweka makubaliano fulani au mikataba. Lakini kuna mashamba ambayo wakulima wametelekeza hivyo baadhi wanaomba kuhudumia kutoka kwa ndugu wa karibu au kutoka kwa mkulima mwenywewe lakini wengi wao ni wale wakulima waliofariki au wamehama kijiji.
sikiliza audio hapo chini.
Chomachoma in nani?
Hapa kuna makundi kama manne hivi.
1. Kundi la kwanza la chomachoma ni wajasiriamali ambao wanakopesha pembejeo wakulima. Pembejeo kama vile madawa, vifaa vya kupuliza madawa, na pesa tasilimu kwa ajili ya mkulima kuhudumia shamba kwa palizi na mambo mengine kwa makubaliano ya kulipwa kipindi ambapo korosho itakuwa zimezaa. Mikopo hii wanakopeshwa mienzi kama nane kabla ya msimu wa mavuno kwakuwa wanakopeshana mwezi wa march na April, hivyo pesa ya huyu mjasiriamali ambae anaitwa kangomba pesa yake inakaa kwa mkulima kwamiezi nane au zaidi. Ni aina ya mkopo ambao hata benki hawawezi kukopesha mkulima. Lakini chomachoma yeye ana take risk pesa yake inakaa kwa mkulima kwa miezi nane, lakini pia kipindi hiki chote chomachoma anakuwa anapeleka marejesho benki kwa kutumia vyanzo vingine vya mapato ukizingatia chomachoma wengi ni wale wenye maduka na biashara zingine hivyo wanakuwa na sifa za kukopesheka benki tofauti na mkulima ambae hana sifa za kukopa benki hivyo kimbilio pekee la mkulima ni kwenda dukani kwa chomachoma kukopa pembejeo au pesa. Kumwambia chomachoma anadhulumu wakulima sio kweli huu ni onevu wa wazi. Ukimwondoa chomachoma kwenye mfumo huu ni kuumiza wakulima labda Kabla serikali haijamuondoa chomachoma lazima wakubali kukopesha wakulima kwa mfumo uleule wa chomachoma ambapo repayment inaanza miezi nane hadi kumi tangu siku ya kukopeshana. Na hili swala la kwamba mkulima anapewa riba kubwa ni hivi; Chomachoma anakopa benki kwa riba, nae ana kopesha mkulima kwa riba, hivyo ni automatically mkulima atalipa riba ambayo ni double. Chomachoma hawezi kukopa benki alafu yeye amkopeshe mkulima bila riba na ukizingatia repayment muda mrefu, ni haiwezekani. Serikali ikitaka kumuokoa mkulima kutokana na hiki kitanzi cha chomachoma lazima ikubali kuanzisha mfuko au benki maalumu kukokopesha wakulima at high risk kama chomachoma anavyokopesha.
2. Kundi la pili ni wajasiriamali ambao wanakopesha wakulima pesa tasilimu kwa kulipwa pesa kwa pesa au pesa kwa korosho. Hawa ndo wale wanatajwa kwamba wanakula maua. Lakini chanzo kikubwa cha mfumo huu ni bei kubwa ya pembejeo za kulimia korosho hivyo mkulima anashindwa kumudu garama na kuamua kutafuta vyanzo vya pesa za ziada zitakazomwenzesha kuhudumia shamba. Msimu wa mavuno ukifika mkulima anachukua kiasi kidogo cha korosho kulipa deni au kwa wale waliokubaliana kulipwa pesa kwa pesa hulipwa pesa kwa kadiri mikataba walivyokubaliana.
3. Kundi la tatu hawa wananunua korosho kabisa. Ingawa wanazunguka na mizani mashambani kununua korosho lakini maranyingi wakulima wenyewe ndo wanaenda na korosho zao kuziuza kwa chomachoma ili wapate pesa ya kujikimu. Na wanauza kiasi kidogo sana. Mfano kwa mkulima mwenye gunia hamsini za korosho anaweza kuuza kilo 50 hadi 100 kwa lengo la kutatua shida ndogondogo za nyumbani lakini mzigo mkubwa anapeleka galani kuikopesha serikali. Sio kweli kwamba mkulima anauza korosho zote kwa chomachoma, na sio kweli kwamba mkulima chomachoma wanadhulumu wakulima. Wakulima wanajitambua. Chomachoma wanatumia fursa hii kwakuwa serikali inachelewa kuwalipa wakulima hivyo kama ilivyo kwa wajasiriamali wa bidhaa zingine kama vile nyanya, vitunguu, mahindi nk. pia hawa wakorosho mfumo ni uleule wa bidhaa nyingine.
4. Kundi la nne hawa wanapewa mashamba na wakulima wenyewe iwapo mkulima ameshindwa kuhudumia hivyo kwa kuhofia shamba kuungua moto au mikorosho kwakukosa huduma anaamua kukodisha kwa mjasiriamali ambae anauwezo wakuhudumia shamba. Wanaweka makubaliano fulani au mikataba. Lakini kuna mashamba ambayo wakulima wametelekeza hivyo baadhi wanaomba kuhudumia kutoka kwa ndugu wa karibu au kutoka kwa mkulima mwenywewe lakini wengi wao ni wale wakulima waliofariki au wamehama kijiji.
sikiliza audio hapo chini.