Korea Kaskazini: Kuzimu iliyopo duniani

Korea Kaskazini: Kuzimu iliyopo duniani

Uongozi
We mwenyewe ni western agent....kwa kujua au kwa kutokujua! Raia wake wako happy na ndio maana hawajasambaa sana. Kungekua na shida kama unavyodai wangetoroka wakaomba hata hadhi ya ukimbizi kwa majirani. Usiniambie eti wamezuiliwa kuondoka maana kama una shida hakuna mtu anaweza kukuzuia usitoroke. By the way huwezi kuwafunga kamba raia wote ukawaweza!

We mwenyewe umeelezea vizuri jinsi uhusiano wa hii nchi na mataifa ya west ulivyo sijui kwanini huamini kama kunaweza kuwa na propaganda! Mwenye akili finyu pekee ndio anaweza kuwaza kwamba propaganda lazima ifanyike katika vyombo vya habari vya ndani pekee!
Uongozi wowote unaojuhusisha na Ushetani lazima utese watu maana ndiyo kazi za kishetani.
 


Fungua hiyo link uone Pyongyang halafu uniambie hayo magari na majengo ni ya kina nani halafu siku nyingine usije na upupu wako hapa

Hahahahaaaaaa.....yaani we umeangalia clip moja tu wakati kwenye hiyohiyo link kuna clips nyingine nyingi zinaonyesha kabisa hakuna magari kabisa barabarani...hebu ukimaliza kuangalia hiyo uliyoweka angalia hizo clip nyingine ushangae...watu wote wanatembea kwa miguu mwanzo mwisho na jamaa yule anayezunguka kutafuta Pizza anapiga misele mitaa kibao iko empty kabisa tena mitaa mingine haina magari kabisa na ni City centre
 
Almost kila kitu ulichoandika sio kweli. North korea uchumi hauko juu. Nchi yao imepigwa vikwazo vizito hawafanyi biashara na nchi yoyot. Ikwazo tu. e zaidi ya china tena kwa black market, kuna mdau ameshaelezea hapo kwamba hata benki kwao ni shida sasa sijui uchumi wao uko juu kivipi. Kwenye silaha pia hawana silah ya kumtisha marekani kama unavosema labda unitajie ni silah gani hiyo maana kwa miaka mingi wanajaribu kutengeneza makombora ya masafa marefu ila wameshindwa. Na kurusha satellite kwenye orbit ni kitu cha kawaida sana nchi nyingi zilifanya hivyo miaka ya 1950 ila kwa level ya north korea wamejitahidi ndo mana tunasema hii nchi inawatu wenye iq ndogo coz pamoja na kulaza wananchi wao na njaa ili wawekeze kwenye vitu kama hivi bado wako nyuma kwa kila kitu.
Umu watu wanaona north korea ni tishio kwa usa. Ni upuuzi kuwaza hivyo north kawekewa vikwazo kama ni tishio mbona anashindwa kuwapiga waliomwekea vikwazo?. Wanaishi katika utumwa wa vikwazo tu.
 
Unaweza kuona ni mateso lakini raia wake wameridhika na style hiyo ya maisha usikute hata sisi kuna wa wanatushangaa tumeweza vipi kuutawaliwa na CCM miaka yote.
ujue nikweli ukiorodhesha maupuuzi ya hapa kwetu kuna nchi wanatushangaa sana,yaani nyumba ya jirani kuna swimming pool lakini wakazi waeneo hilo wanakosa hata maji ya kunywa
 
Wangekuwa na akili ya kutosha wangekuwa wameshajikwamua na huo utawala dhalimu zamani.
we umeshindwa kuwatoa ccm wewe nawao nani mwenye akili?tena wewe ndio mbumbumbu namba sifuri
 
we umeshindwa kuwatoa ccm wewe nawao nani mwenye akili?tena wewe ndio mbumbumbu namba sifuri

Kwa uandishi wako ni bayana kwamba wewe ni miongoni mwa kundi la watanzania ambao wezi na mafisadi mnawafagilia na kuwanyenyekea kwamba wana akili nyingi.
 
Kwa uandishi wako ni bayana kwamba wewe ni miongoni mwa kundi la watanzania ambao wezi na mafisadi mnawafagilia na kuwanyenyekea kwamba wana akili nyingi.
mafisadi wako ccm
 
Mm nilikwenda huko 2011 na shirika la UNFPA kama volunteer, tulipata visa Sweden ambako ndio kulikua na diplomatic mission, then tukaenda kuondokea china kwenda huko

Currency yao inaitwa won, na kiongozi msaidizi wa chama alikua kim yong nam wakati huo, ila mwenyekiti wa chama raidi wa nchi hiyo marehem kim jong ill, kwa sasa sijui bado utaratibu ni huo au la

Ila karibia yote aliyosema mleta mada ni ya kweli, gari alizoonyesha mdau kwenye picha ni za watu waliokua,authorised, kuna maswali mengi na misukosyko ukinunua gari, na utalinunua wapi?

Wanaruhusu kutembea miji mingine zaidi ya Pyongyang?
Vipi kuhusu usafiri wa umma
Vipi huduma za hoteli, zipo?
 
Mm nimetoa first hand experience, nimeishi kwa miezi 3 mwaka 2011 nilienda kwa program ya UNFPA, hivyo mengi ya aliyosema mleta mada niliyaona, wageni wote tuishio mitaani lazima asubuhi na jioni tulipoti kwa serikali ya mtaa, achin num

Sijawahi kuzipenda nchi za magharibi, lakini siwezi kuzisingizia nchi za magharibi kwa vitu nilivyoviona mwenyewe, napenda kuwa mkweli kwenye ukweli

Raia wa north korea wao wenyewe wameshazoea maisha hayo, hawana jinsi waende wapi?
Raia yoyote haruhusiwi kuondoka nchini humo bila sababu maalum,

Magari yanaendeshwa na watu wengi tu katika nchi hiyo lakini ndio hao waliokua authorised, viongozi wa jeshi, taasisi, viongozi wa mitaa, wakuu wa shule na kadhalika ambao pia ni wengi, magari haya yakiingia barabarani ni mengi, na yakioneshwa kwenye video unaweza kudhani kila raia ana gari

Wapo watu asilia yao ni ubishi, no matter what, ukimwambia hii ni njano yeye anasema ni nyekundu, watu watajaribu kumwelewesha hii ni njano yeye atabaki peke yake akidai ni nyekundu, huyo mtu hawezi kisaidika,
Ni matumaini yangu haupo kwenye kundi hilo

Mkuu,

Tatizo Bongo, wengi hawajaona dunia bado. Wanadanganyika haraka sana.

Kuna vitabu vingi vya wakimbizi wa Korea ya Kaskazini, wameandika jinsi walivyoteseka huko na ndugu zao kuuawa au kufungwa walipokimbilia Korea ya Kusini kupitia China au nchi ya tatu.

Wanaoifaidi hii nchi ni wanajeshi na familia na rafiki karibu wa Kim Jong-Un.

Wanaobisha, waende China. Hapo, raia wengi wanaweza kwenda Korea ya Kaskazini kutalii kwa kutumia kampuni ya kitalii kama Koryo au Uri Tours. Watajionea wenyewe. Waje hapa na mrejesho.

Huruhusiwi kuingia na simu na unafuatwa kila sehemu na intelligence officer wanaojifanya "tour guide". Hauruhusiwi kuongea na wananchi wao na lazima umsujudie sanamu wa Kim Il Sung.

Nilishawahi kuingia ubalozi wao pale Salender, leo ni shule ya Al Muntazir.
Walikuwa wanalala chini. Balozi wao ana zamu ya kufagia na kulinda ubalozi. Hamna Mtanzania anafanya kazi pale hata mmoja. Hawaruhusiwi.
 
Hivi vitabu vinaelezea mateso ya wananchi wa Korea Kaskazini. Vimeandikwa na raia wao walioweza kutoroka.

1. How to Live - Yeonmi Park

2. The Aquariums of Pyongyang- Kang Chol-hwan

3. A Thousand Miles to Freedom: My escape from North Korea - Eunsun Kim
 
Wanaruhusu kutembea miji mingine zaidi ya Pyongyang?
Vipi kuhusu usafiri wa umma
Vipi huduma za hoteli, zipo?

Mtalii ananunua package ya utalii na haruhusiwi kwenda sehemu yoyote peke yako. Siyo kila kona ya nchi unaruhusiwa kutalii. Na lazima ufatane na "Tour Guide". Hawa ni intelligence officers.

Unafuata program ya Package yako.

Huruhusiwi kujichanganya na wananchi. Usafiri wako na hoteli yako imetengwa na wananchi wa kawaida na hawaruhusiwi kuongea na mtaliii. Hamna mtandao na umezungukwa na intelligence officer saa zote. Hata kuwa na biblia ni kosa.

Mungu wao ni Raisi wao.
 
Mtalii ananunua package ya utalii na haruhusiwi kwenda sehemu yoyote peke yako. Siyo kila kona ya nchi unaruhusiwa kutalii. Na lazima ufatane na "Tour Guide". Hawa ni intelligence officers.

Unafuata program ya Package yako.

Huruhusiwi kujichanganya na wananchi. Usafiri wako na hoteli yako imetengwa na wananchi wa kawaida na hawaruhusiwi kuongea na mtaliii. Hamna mtandao na umezungukwa na intelligence officer saa zote. Hata kuwa na biblia ni kosa.

Mungu wao ni Raisi wao.

Duh!! Nilikuwa nasoma makala za Waandishi/Watu ambao wamekwenda huko. Na kuna picha nyingi zimepigwa ila kwa siri. Najiuliza walikuwa na ujasiri gani!! Wamezungumzia pia kuwa korea kuna rushwa sana hasa kwenye kada ya kati na chini, inaonyesha pamoja na mbinyo lakini kuna Wakorea wamechoka kabisa.

Hivi ukifika airport kuna idadi kiasi gani cha Wakorea wanaotoka nje?

Sura za Wakorea unawapowatazama, zinaonyesha matumaini/furaha?
 
Unaweza kuona ni mateso lakini raia wake wameridhika na style hiyo ya maisha usikute hata sisi kuna watu wanatushangaa tumeweza vipi kuutawaliwa na CCM miaka yote.
Ni kweli kabisa , mimi sijaona kama tuna tofauti yoyote na hao.
 
Duh!! Nilikuwa nasoma makala za Waandishi/Watu ambao wamekwenda huko. Na kuna picha nyingi zimepigwa ila kwa siri. Najiuliza walikuwa na ujasiri gani!! Wamezungumzia pia kuwa korea kuna rushwa sana hasa kwenye kada ya kati na chini, inaonyesha pamoja na mbinyo lakini kuna Wakorea wamechoka kabisa.

Hivi ukifika airport kuna idadi kiasi gani cha Wakorea wanaotoka nje?

Sura za Wakorea unawapowatazama, zinaonyesha matumaini/furaha?

Mkuu,

Wakorea wa Kaskazini hawaruhusiwi kusafiri nje ya nchi bila kibali. Wengi ni wafanyakazi wa hoteli za Kikorea China au maofisa wa Ubalozi wao.

Kuruhusiwa kutoka nje ni kuwa VIP na kuwa na connection za nguvu na serikali.

Kila kitu ni propaganda na wao ni mabingwa wa fani hiyo.

Nakumbuka kusoma magazeti yao ubalozini kwao Tanzania. Picha za chakula cha kila aina mezani mwa mwananchi na sura za furaha kila pahali.

Lakini, wafanyakazi wa Ubalozi wao walikua wanakula viazi vitamu na njegere tu. Hamna chandarua wala kitanda chumbani. Hii nimeona kwa macho yangu, sijahadithiwa.

Sura zao ni za furaha tu kwa kuwa wote ni actors. Kijijini wanapokufa watoto na njaa, huruhusiwi kwenda ili picha zilitoroshwa kuonyesha dunia. Karibu pesa zote za nchi zinatumiwa kijeshi.

Katika hizi picha zilizopigwa kisiri, utaona wananchi wapo mstari kupata chakula cha ration kama kwetu zamani. Utakuta watoto wamekonda na njaa, utakuta mtu ana kompyuta lakini hana umeme. Utakuta watoto wanashangaa ngazi za umeme. Utakuta watu wamekaa kati kati ya barabara kwa kuwa hamna magari mingi. Utakuta watu wanaoga na kufua katika mito. Utakuta watu wanasukuma mikokoteni kama kwetu. Utakuta chakula cha misaada . Lakini daima hutakuta mwanajeshi njaa.

ImageUploadedByJamiiForums1455811951.970738.jpg


ImageUploadedByJamiiForums1455811968.569536.jpg


ImageUploadedByJamiiForums1455811983.217267.jpg


ImageUploadedByJamiiForums1455811995.650166.jpg


ImageUploadedByJamiiForums1455812011.200733.jpg


ImageUploadedByJamiiForums1455812025.017343.jpg


ImageUploadedByJamiiForums1455812038.217142.jpg


ImageUploadedByJamiiForums1455812049.583477.jpg


ImageUploadedByJamiiForums1455812065.548647.jpg


ImageUploadedByJamiiForums1455812077.916610.jpg


ImageUploadedByJamiiForums1455812112.365729.jpg
 
Back
Top Bottom