Kopesha ushangazwe

Kopesha ushangazwe

fact only

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2024
Posts
975
Reaction score
1,356
Wakuu Kama title inavyo sema kopesha ushangazwe. Mimi nimeshangazwa wiki hii na wadaiwa wangu(kuonekana mbaya kudai changu).

Naomba experience yenu nyinyi ambao tayari mlishawahi kukopesha na mkashangazwa na mli handle vipi?.
 
Kumkopesha mtu shida sana,
Mimi wiki kama 2 kuna jamaa alinifata home usiku akaniomba nimsaidoe kiasi kidogo cha fedha alikuwa mpole sana na mnyenyekevu nikamwambia sina.
Akanifata tena siku iliyofata akiwa na mtoto wake anatia huruma kwamba mtoto anaumwa akanisisitiza nimkopeshe atanirudishia baada ya wiki moja.
Imefika wiki simuoni nikaanza kumtafuta nikikutana naye ananiambia hana hela hajapata. Ananiahidi kesho ,ikifika hiyo kesho aliyosema haji naanza kumtafuta nikimpata ananijibu hajapata ananipa ahadi ambazo hatekelezi.
Yaani ikawa mimi ndio namtafuta namdai .
Jinsi ambavyo sipendi kufatilia watu nimeamua kumchunia kila akiniona anajistukia saa nyingine anajificha wakati mimi nishamuona na mimi nampotezea.
Kukopesha watu imekuwa jau sana .
Unapata kazi ya kuanza kumfatilia akulipe wakati alipokuwa anashida yeye ndiye alikutafuta
 
Wakuu Kama title inavyo sema kopesha ushangazwe. Mimi nimeshangazwa wiki hii na wadaiwa wangu(kuonekana mbaya kudai changu).

Naomba experience yenu nyinyi ambao tayari mlishawahi kukopesha na mkashangazwa na mli handle vipi?.
Wabongo bado tuna shida sana, unakopesha una leseni? Ukimpa mtu mali yako binafsi ni kwamba umedonate, kama mtu anataka mkopo aende kwa wakopeshaji rasmi waliosaijiliwa ukijipendekeza umeliwa tu na futa kwenye vitabu vyako! Wakilipa ujue ni waungwana na wanakuheshimu sana
 
Wakuu Kama title inavyo sema kopesha ushangazwe. Mimi nimeshangazwa wiki hii na wadaiwa wangu(kuonekana mbaya kudai changu).

Naomba experience yenu nyinyi ambao tayari mlishawahi kukopesha na mkashangazwa na mli handle vipi?.
Kwa uzoefu wangu, ni asilimia 10 tu (au pungufu) ya watu ambao unaweza kuwakopesha na wakarudisha kwa wakati bila tatizo. Waliobaki, kuna mawili, ama usirudishiwe kabisa, au urudishiwe baada ya kugombana sana!!
 
Back
Top Bottom