Kongamano la Azimio la Arusha

Kongamano la Azimio la Arusha

Huyu mfungaji ansema wako watu ambao hawakubaliani kabisa na azimio la arusha ila ni bahati mbaya hawakupata nafasi ya kuongea leo maoni yao
 
Ni shukurani kwa waandaaji, washiriki, wanaongalia kwenye tv, redio.....agggrrrh!...amewasahau na wale wanaofatilia kupitia JF
 
Walisidia kuwezesha kongomano la AA Pro. Shivji, Bashili ally, Pro. Athumani ............................................................................................
 
Mfunga mada: Ipo haja ya kufanya tafakari ya kina kuhusiana na AA maana hata hapa kuna watu walikuwa wanapinga AA. Shukrani zinatolewa kwa wadau wote. Ujamaa upo unaendelea maana hapa udsm wanafunzi asilimia kubwa wanafadhiliwa na bodi ambazo ni kodi za watanzania.
 
Kuna msanii ataimba wimbo kuhusiana na katiba mpya, unasemaje? watch out
 
AA halikuuliwa pale Zanziba na Azimio la Zanzibar, bali na hotuba ya Kingunge Ngombale Mwiru pale Chimwaga pale Dodoma. Na huo ukawa ndio mwanzo wa mafisadi kuingia katika chama na ndio mwanzo wa Kingunge mwenyewe kubadilika kuwa fisadi naye na kusahau misingi ya AA.
kimsingi kongamano limehudhuriwa na watu wa mrengo mmoja limekaa kimagambagamba ndo maana kulikuwa hakuna kukinzana.
 
je makala zinazotolewa katika makongamano ya chuo kikuu zinaweza kuandaliwa kama kitabu cha maoni ya kitaaluma katika mustakabali wa kuandaa katiba yetu?
 
Kama alivyosema Butiku kule Zanzibar Halmashauri kuu ya CCM haikuwaruhusu viongozi wote kukiuka miiko ya uongozi kama ilivyoainishwa katika Azimio la Arusha bali liliruhusu viongozi wa chama kuweza kupangisha nyumba walizokuwa nazo kama njia ya kujipatia kipato cha kujikimu badala ya kuwa omba omba na kukitia aibu chama; wajanja wakatafsiri ruhusa hiyo kama ndio mwanya wa kujiingiza kwa viongozi wote katika biashara kitu ambacho hakikuruhusiwa!! Tafsiri kama hiyo pia ilitumiwa na wajanja serikalini kwenye mpango wa kuziuza nyumba za serikali; inasemekana uamuzi wa baraza la mawaziri haukuwa kuwauzia nyumba viongozi wote serikalini bali wale waliokuwa wanastaafu na walikuwa hawana mahala pa kujisetili na familia zao; sasa Magufuli na genge lake wakatafsiri uamuzi huo kuwa ni ruhusa ya kuuza nyumba zote za serikali kwa viongozi waliokuwa madarakani!! Na ili kufanikisha azma yao kirahisi mtu wa kwanza kuuziwa nyumba akawa Katibu Mkuu Kiongozi Lumbanga!! Ni muhimu kwa wana zuoni kufanya utafiti wa kina ili kujua ukweli wa maamuzi haya ambayo yameathiri sana uchumi wa nchi yetu!!
 
wanafunzi 300 wa UDSM walifukuzwa wakipinga AA na mwalimu mwenyewe

kaka hawakufukuzwa kwa kupinga azimio la arusha bali walikuwa wanapinga kupelekwa JKT huku wakilipwa asilimia 60 ya mshahara. Ilikuwa mwaka 1966 mwaka mmoja kabla ya kuanzishwa azimio la arusha. Nadhani hukumpata vizuri profesa.
 
kimsingi kongamano limehudhuriwa na watu wa mrengo mmoja limekaa kimagambagamba ndo maana kulikuwa hakuna kukinzana.

wa mlango wa pili walikuwa wapi?acha unafiki tafakari na kuongea kwa busara,
ingekuwa tupo kanisan ningekwambia ushindwe na ulegeeee,
 
wanafunzi 300 wa UDSM walifukuzwa wakipinga AA na mwalimu mwenyewe

kaka hawakufukuzwa kwa kupinga azimio la arusha bali walikuwa wanapinga kupelekwa JKT huku wakilipwa asilimia 60 ya mshahara. Ilikuwa mwaka 1966 mwaka mmoja kabla ya kuanzishwa azimio la arusha. Nadhani hukumpata vizuri profesa.
 
wanafunzi 300 wa UDSM walifukuzwa wakipinga AA na mwalimu mwenyewe

kaka hawakufukuzwa kwa kupinga azimio la arusha bali walikuwa wanapinga kupelekwa JKT huku wakilipwa asilimia 60 ya mshahara. Ilikuwa mwaka 1966 mwaka mmoja kabla ya kuanzishwa azimio la arusha. Nadhani hukumpata vizuri profesa.
 
huyo ni mzalendo bora kuliko kikwete mwenye ngozi nyeusi , na kabila lake m-kwe-re ,
lakini ni huyo huyo pamoja na kuwa mtanganyika halisi hachiambali kuzaliwa yeye ameshiriki vilivyo kuwakikingia kifua wezi wa mali za umma kupitia epa,
ni bora shivji kuliko kuliko wabantu wa nchi hii.

shivji dzaini fluni ni mhindi inakuaje anaijua tz kiasi hicho, maanake yupo fit katika kila jambo
 
Kama wewe ni mfanyabiashara na una mali, na unagombea uongozi kama Ubunge, na kama umepata ule uongozi utakuwa na mgongano wa kimaslahi katika kufanya maamuzi, ndiyo maana ya maadili.

Dhana ya Miiko ya AA sio dhana ya Mgongano wa maslahi. AA halizungumzii mgongano wa Maslahi, azimio linazungumzia sifa za kiongozi. Maana yake kama una mali hata kama umeiweka kwenye trust wewe huna sifa za kuwa kiongozi.

Ni vizuri tutofautishe miiko na maadili ya uongozi

Nawashukuru sana Mbogela F Sanga na Nicky82 kwa kuwahabarisha wale ambao hawakufuatilia kwa TV juu ya mdahalo huu mzuri sana.
Naamini hata kwa chama tawala hili litakuwa somo zuri sana ya kule chama kilikotoka na kiendako na matatizo yanayo kipata z sasa hivi.

Kwamba CCM wameonyesha muelekeo wa kuya kubali makosa yao ni mwendo sahihi kabisa kulingana na wakati.Na wasiposahihisha mwendo wa CCM ukaendana na falsafa ya Azimio la Arusha basi ni lazima chama kitadhoofika na kuondolewa madarakani.
Kwa upande mwingine tungependa kuona kongamano la falsafa inayofuatwa na CDM ikoje, na mustakabali wa wananchi katika falsafa yao ikoje.
Falsafa ya AA inakata pande zote,mfanya biashara hawezi kuwa kiongozi katika hali halisi ya kiTanzania, hili liko wazi.
Wafanyabiashara wako kote CCM na CDM, hili likoje wajameni?
 
Falsafa ya AA inakata pande zote,mfanya biashara hawezi kuwa kiongozi katika hali halisi ya kiTanzania, hili liko wazi.
Wafanyabiashara wako kote CCM na CDM, hili likoje wajameni?


Katika moja ya hoja prof.Shivji alisema misingi ya mwanzo ya CCM ilikuwa ni chama cha wakulima na wafanyakazi...ila katika moja ya kikao kilichofanyika Kizota enzi hizo Kingunge Ngombaremwiru aliwasilisha mada kwa chama kuwafungulia milango wafanyabiashara na hapo ndipo chama kilipokaribisha wafanyabiashara..na mtu akishakuwa mwanachama anakuwa na haki ya kuchagua kiongozi au yy mwenyw kuchaguliwa kuwa kiongozi
 
Hivi Mdahalo huu na ile miwili ya katiba imeratibiwa na taasisimoja? maana wadau wachangiaji waliokuwepo kwenye ile midahalo iliyopita sijawaona hususan wale wa vyama pinzani na CCM. lakini ajabu leo hata Nape amekuwepo japo kulingana na kijana kiongozi wa mdahalo anasema hakuna mtu aliyepewa mwaliko rasmi. kweli wazee wote akina Butiku wamekuja hapo bila mwaliko rasmi! tena wakawa wachangiaji wazuri vile! this is so interesting. Lisije likawa ni Gamba linajaribu kufunika nguvu ya midahalo iliyopita.
 
Nawashukuru sana Mbogela F Sanga na Nicky82 kwa kuwahabarisha wale ambao hawakufuatilia kwa TV juu ya mdahalo huu mzuri sana.
Naamini hata kwa chama tawala hili litakuwa somo zuri sana ya kule chama kilikotoka na kiendako na matatizo yanayo kipata z sasa hivi.

Kwamba CCM wameonyesha muelekeo wa kuya kubali makosa yao ni mwendo sahihi kabisa kulingana na wakati.Na wasiposahihisha mwendo wa CCM ukaendana na falsafa ya Azimio la Arusha basi ni lazima chama kitadhoofika na kuondolewa madarakani.
Kwa upande mwingine tungependa kuona kongamano la falsafa inayofuatwa na CDM ikoje, na mustakabali wa wananchi katika falsafa yao ikoje.
Falsafa ya AA inakata pande zote,mfanya biashara hawezi kuwa kiongozi katika hali halisi ya kiTanzania, hili liko wazi.
Wafanyabiashara wako kote CCM na CDM, hili likoje wajameni?[/QUOTE]

Wengi hawataki ku-discuss hapo

unajua kuna tofauti kati ya kuwa mshabiki wa mabadiliko na mtaka sustainable mabadiliko

Niliishawahi kuwauliza hapa JF

https://www.jamiiforums.com/habari-...her-future-rostam-aziz-or-edward-lowassa.html

Kama kawaida yangu, huwa nasoma vitu vingi kwa wanaojiita wanaipenda hii nchi, wakati tunawaza matatizo ya sasa,wengi huwa hawawazi tutayazuia vipi in future generations!

Ulichouliza hapo ni challenge kwa vyama vyote, lakini usishangae hakuna wa kukujibu kwa ufasaha kwa sababu hatuwazi kuhusu nchi hii, ila tunakurupuka. Wafanyabiashara wanaweza kuwa accomodatated kwenye politics, lakini how? how ina a such to convince somebody that it will work? kwa sasa hakuna hiyo system so at a glance wote wanakuwa disqualified..wakubali wakatae.

Nilikuwa mmoja wa washiriki kuandaa makongamano ya leo, nadhani umeona kuna tofauti kubwa ya SIASA na FACTS

Till then
 
Back
Top Bottom