Kongamano la Azimio la Arusha

Kongamano la Azimio la Arusha

Mdau: Nilikuwa na elfu 30 wakati wa AA, niliulizwa umepata wapi (nilikuwa mjasiliamali kipindi hicho). Nilibanwa sana, haikuwa mchezo. Nililazimika kwenda butiama kujionea Nyerere alikuwa ni mtu wa aina gani. Kweli nyerere aliipenda nchi yake na alikuwa mzalendo wa kweli.
 
Kuna mzee anatema point "mema yote yote yaingizwe kwenye katiba kwa maslahi ya taifa"
 
kuna mzee mmoja amewaasa vijana kuungana na wasio nacho ili kuleta mabadiliko ya nchi yetu akamalizia kwa kusema aluta continue
 
Shivji: ukweli unapatikana kwenye mijadala, anagusia challenge ya Kaduma kuhusu ufundikishaji wa maadili
 
Anasema CCm inabidi isimamia misingi ya azimio la Arusha kupitia chama kwanza kabla haijaenda kwenye katiba
 
Shivji: ccm isimamie kurudishwa misingi ya azimio la Arusha. Lakini watasimia wakati hawafuati hiyo miiko?
 
Shivji: CCM wanapaswa kwanza kusimamia misingi ya azimio kwenye chama kabla ya kusimamia misingi ya azimio kwny katiba
 
Vijana wa udsm kujiunga na upinzani na kupata cheo haraka ni kuenzi AA. Shivj: habari ndo hiyo
 
Shivji: Vijana someni kuhusu azimio la arusha, na someni sana historia ya nchi hii....anawaasa vijana kuwa watafiti na ndicho wakulima na wafanyakazi wanachotegemea toka kwao
 
Vijana wa wakati ule walikuwa wana questioned every thing hata mwalimu walikuwa wana mquestion.
 
Shivji: Tabaka la wanaotawala siku zote watajihalalisha on expenses kwa wale wa tabaka la chini...anasema hata mabepari wanpoluja kuwekeza wanasema wamekuja kutoa ajira na hawasemi wamekuja kutunyonya
 
Prof. Shivji: Ukweli unapatikana kwenye mijadala. Kugusia ya kaduma- Je ilingewezekana kwa mtu mwenye kiwanda kujiunga na tanu kwakuwa anaamini ktk ujamaa? Wangapi tunawafundisha watoto wetu wasiwe mabepari. Kuhusiana na mbita: Tulisema wazi kwamba hatuwezi kununulika,je kweli leo hatuwezi kununulika? Kujiunga na chama kwa ahadi ya cheo sio kununulika? Kuwa na msimamo ni muhimu sana.

Vijana someni historia ya nchi yetu na chambueni AA. Historia ya nchi yetu kisiasa haijaandikwa vzuri. Hatujafanya uchambuzi kutathmini athari za kuachana na azimio la arusha. Vijana tu-question everything, hata nyerere hatukuwa tunamkubalia kila kitu. Hata wakulima wanataka tufanye utafiti ili waweze kujua mazingira yao. AA haikubadilishwa kwa ajili ya watu wadogo (azimio la ZNZ), bali lilihalalishwa kwa kutumia watu wadogo. Wewekezaji hawaji kuwapa ajira watu wadogo.
 
Back
Top Bottom