Kongamano la Azimio la Arusha

Kongamano la Azimio la Arusha

Anasema turudi kwenye imani ya mwana Tanu.
1) Binadamu wote ni sawa
Rushwa ni adui wa haki sitakubali kutoa wala kupokea rushwa.
Nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu na kutumia elimu yangu kwa faida ya wote.(GONE WERE THOSE DAYS)
 
Kama wewe ni mfanyabiashara na una mali, na unagombea uongozi kama Ubunge, na kama umepata ule uongozi utakuwa na mgongano wa kimaslahi katika kufanya maamuzi, ndiyo maana ya maadili.

Dhana ya Miiko ya AA sio dhana ya Mgongano wa maslahi. AA halizungumzii mgongano wa Maslahi, azimio linazungumzia sifa za kiongozi. Maana yake kama una mali hata kama umeiweka kwenye trust wewe huna sifa za kuwa kiongozi.

Ni vizuri tutofautishe miiko na maadili ya uongozi
 
Shivji kasema ili kuepusha mgongano wa maslahi,si vema wafanyabiashara kugombea uongozi! Na ndo miiko ya AA.
 
Hizi ndizo tunu zetu ambazo hawa wabinafsi Magamba ndio wameziharibu.
 
Matabaka ya wakulima na wafanyakazi ndio msingi wa maendeleo, sio wawekezaji, HAPANA, na maendeleo yawe kwa ajili ya wao kwa manufaa yao, so development is for them and for their development. Chama chenye itikadi ya kijamaa kiwe chama cha wakulima na wafanyakazi hivyo wanachama wake wawe wakulima na wafanyakazi na viongozi wake wawe wakulima na wafanyakazi. My Take: wafanyabiashara hawaingii katika chama cha kijamaa

Sasa hawa mabepari wameingiaje CCM?:frusty:
 
Ushiriki wa vijana katika AA.

Vijana wengi walitembea na waliunga mkono AA, na hatimaye mwalimu mwenyewe alitembea kutoka Butiama.
Vijana wa Chuo waliunga mkono pia suala zima la Ujamaa.

Vijana walijadili falsafa, nadharia na itikadi ya ujamaa, walikosoa sera za serikali. Na walijadili kama sera za seriakli zingeweza kujenga ujamaa, mijadala ilijikita katika Umarx, na walitumia gazeti lao la Cheche.

Walifanya uchambuzi na utafiti, mfano walidadisi Utalii, Je Utalii unaweza kujenga Ujama?

Je utalii Unaweza kujenga ujamaa kwa Utalii?

Vijana walichambua Dola, je dola inaweza kutufikisha kwenye ujamaa?

Na je dola hii ni ya wafanyakazi na wakulima?

Walichambua jamii na matabaka yao, mijadala iliendelea na mara nyingine ilikuwa ya moto moto sana.

Anasema Shivji.
 
Rushwa ni adui wa haki sitakubali kutoa wala kupokea rushwa.
Nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu na kutumia elimu yangu kwa faida ya wote.(GONE WERE THOSE DAYS)

Umenikumbusha primary school tulikuwa tunakula kiapo 'mimi ni chipukizi wa ccm' na kuzisema ahadi kumi za mwana Tanu.
 
katika mijadala mambo matatu yalijitokeza;

1. Haitoshi kutaifisha mali na njia za uzaishaji na kuziweka mikononi mwa dola, kwani unaweza ukaanza kujenga tabaka jipya.

2. Mapinduzi ya kijamaa sio lelemama, ni mapambano ya kitabaka, kwani maslahi ya kitabaka yanagongana.

3. Huwezi kujenga ujamaa au kuendeleza mapambano kutoka juu au kupitia vyombo vya Dola ni budi wafanyakazi na wakulima wawe na vyombo vyao vya kuongoza mapambano
 
Sasa hawa mabepari wameingiaje CCM?:frusty:

Azimio lilipinduliwa miaka ya 90, mazingira yalijengwa ya kupindua azimio. Moja ya sehemu ya AA lilikuwa ni utaifishaji. Walijitokeza watu wenye jaziba kwenye chama waliaanza kutofautisha kila kitu hata maduka madogo.

Na hakuna sehemu yoyote duniani ambapo serikali inaweza kuendesha biashara ndogo kama maduka madogo kiserikali na kufungua saa 2 na kufunga saa 11
 
Wakulima na wafugaji wote walitakiwa kuhama katika makazi yao ya asili, walilazimishwa kukaa katika vijiji.

Kwa maoni ya Shivji hapo ndio ulikuwa mwanzo wa mwalimu kupoteza kuungwa mkono na tabaka la wakulima.
 
nini kinaongelewa?
Nilikuwa nimesaanza kutoa up date kwenye ile thread ya kongamano na katiba njoo kule utaona up date nimepost, nimemuomba mod waunganishe thread naona wamechelewa kuona ombi langu
 
Shivji anasoma mwongozo wa CCM wa 1981/82. Anasoma "leo ubepari umekuwa na vishawishi vingi zaidi nchini kuliko ilivyokuw akabla ya AA,,,,,,, Ubepari umefaulu kujipenyeza hata ndani ya sekta ya umma, ndio maana ubepari unaweza kujitokeza hadhari na kukashfu ujamaa na kututaka tubadirishe siasa yetu.
 
Nafasi ya AA katika mjadala wa katiba mpya. Atazungumzia kw amuhtasari katika muundo wa kuibua maswali:
 
Kuanzia mwka 1985, tulikubali na kukumbatia sera za soko za ubepari mambo leo, sera za soko hurua, sera zilizozaa soko holera, bei za vitu vingi kama mafuta, unga sukari zinapanda kigholela na hakuna uwezo wowte wa kuweza kudhibiti. wananchi pamoja serikali yao wamekuwa watazamaji katika soko linalojiendesha lenyewe?? swali je mfumo huu utatupeleka wapi?? ni suala la kujadiri kwani ni suala la kikatiba, nafasi ya dola katika sera ya uchumi.
 
tukakumbatia sera ya uwekezaji sera iliyozaa ni sera ya Ufisadi. hii sio sera ya chama tawala ni sera ya uchumi wetu, haitoshi kuorodhesha majina tu, kuna haja ya kufanya uchambuzi, ukifanya uchambuzi utaona kuna mfumo tunaozungumzia ambao ni mfumo wa kifisadi unaojikita katika ulimbikizaji mali. kam huna mtaji utatumia vyeo vyako katika dola kujilimbikizia, Ufisadi ni uporaji, na ndio mfumo mzima wa ubepari, ufisadi ni uporaji, wanapora mali asili setu na kuzifanya zao
 
Anasema hakuna mtu anayetoa njia ya kutibu ugonjwa wa ufisadi labda atokee babu w akikombe kutibu Ufisadi
 
Je tunaweza kujadili ufisdi nje ya mfumo tulionao, tunaweza kujadili katiba mpya nje ya mfumo tulio nao?
 
Anazungumzia ufisadi na kusema mfumo wa ubepari ndio chanzo cha ufisadi
 
Shivji anasema tunahitaji siasa ya ukombozi sbb mfumo huu wa sasa wa siasa za ushindani umeleta mfumo wa ununuzi wa kura
 
Kila siku tunaambiwa tunajenga demkrasia, wkaati uwezo wetu wa kujiamulia mambo yetu wenyewe unapungua kama nchi, kama serikali? sasa tunajenga demokrasia ya namna gani hiyo na sisi hatuna uwezo wetu wa kujiamulia mambo yetu wenyewe? Nadhani ni jambo muhimu tujadili katika majadiliano yetu ya katiba mpya, demokrasia ni nini? labda tuwe na mfumo w akujadili kutoka chini
 
Back
Top Bottom