Konda na dereva wa daladala kuwa wachafu na rafu kazini kwao

Tlaatlaah

JF-Expert Member
May 18, 2023
9,824
13,194
Kuanzia sare zao za kazi yaani, shati na suruali. kwanza ni vichafu, lakini pia ni vichakavu na sielewagi vinachakaaga kwa kazi gani au kuvaliwa wapi zaidi ya humo humo kwenye daladala 🐒

Sawa, kazi ni kazi ilia angalau wawe wanaoga, wawe wanasafisha midomo, walau kunyoa ndevu na kua nadhifu kiasi...

Mfano unakuta konda kavaa sare juu ya t-shirt yake, anavuja jasho, mdomoni ameng'ata kalamu, mdomo unatema harufu nzito, halafu anakusanya nauli, abiria mmebanana nae anataka kupenya humohumo mlipobanana dah, na wewe umeulamba kweli, umechomekea zako shati jeupe unaelekea town 🐒

Huu mtindo au fashion yao inakera, inaudhi na kwakweli inatia kichefuchefu na ni aibu inayotia doa unadhifu wa waTanzania

Hivi hali ile ya makondakta na madereva wa daladala inachochewa na nini hasa?🐒
 
Pole mheshimiwa, unapanda daladala mara moja moja kucheki wananchi wako bila shaka, make we ni mtu wa mavieite.....
hapana mim si wa mavieti. mimi ni kiongozi mchapakazi wa wanainchi, mnyonge, na nisiestahili kitu...

na kwa maisha haya,
sina hakika kama kuna kiongozi humu nchini haijawahi kutumia usafiri wa kidala 🐒

bilashaka hayupo.
katika muktadha huo, ndipo msingi wa hoja yangu ukaanzia....

actually dinga yangu binafsi iko polisi tangu juzi nilipopata ajali, na sasahivi natumia mkoko wa wanainchi....

hii kasumba ya konda na dereva wa daladala imeibuka kichwani mwangu baada ya kumuona dereva wa treka ya shamba yuko smart mno akisomba mchanga wa kujengea.

nikajiuliza why hawa wa kwenye daladala wako rafu 🐒
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom