Kombe la Dunia 2022: Tunavikosa sana vionjo tulivyovizoea kwenye mitanange ya Kombe la Dunia

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,664
18,039
Kukosekana kwa wachezaji fulani kwenye Kombe la Dunia kunachangia kutukosesha vionjo tulivyovitarajia. Kwa mfano kokosekana kwa mchezaji bora wa Dunia kwa sasa Benzema (mtaalam wa kutupia), kukosekana kwa Halaand (mtupiaji mwenye mabavu), kukosekana kwa Mane (mtalaam wa kutupia), kukosekana kwa Mohamed Salah (mshambuliaji machachari).

Wachezaji hawa aidha ni majeruhi au mataifa yao hayakufuzu kuingia kwenye kinyang'anyiro cha Kombe la Dunia. Nguli waliopo wamepoteza sana makali kama vile Christiano Ronaldo na Messi ambao hawapo kwenye kiwango chao kutokana na umri (pengine).

Kiukweli hakuna anayeweza kutusahaulisha vionjo kama vya kina Zinedane Zidane, Ronaldinho, Ronaldo wa ukweli (the phenomenone), n.k.

Kwa kweli vitu adimu hatujaviona kabisa hadi sasa! Kwa wakongwe kwenye ushabiki wa soka wananielewa! Pasi zenye macho na 'free kick' kama za David Beckham zimekuwa simulizi za kale! Naona kama Kombe la Dunia linakuwa la kawaida sana!
 
Kukosekana kwa wachezaji fulani kwenye kombe la dunia kunachangia kutukosesha vionjo tulivyovitarajia. Kwa mfano kokosekana kwa mchezaji bora wa dunia kwa sasa Benzema (mtaalam wa kutupia), kukosekana kwa Halaand (mtupiaji mwenye mabavu), kukosekana kwa Mane (mtalaam wa kutupia), Kukosekana kwa Mohamed Salah (mshambuliaji machachari). Wachezaji hawa aidha ni majeruhi au mataifa yao hayakufuzu kuingia kwenye kinyang'anyiro cha kombe la dunia.
Nguli waliopo wamepoteza sana makali kama vile Christiano Ronaldo na Messi ambao hawapo kwenye kiwango chao kutokana na umri (pengine).
Kiukweli hakuna anayeweza kutusahaulisha vionjo kama vya kina Zinedane Zidane, Ronaldinho, Ronaldo original (the phenomenone), nk.

Kwa kweli vitu adimu hatujaviona kabisa hadi sasa!! Kwa wakongwe kwenye ushabiki wa soka wananielewa! Cross zenye macho na free kick kama za David Beckham zimekuwa simulizi za kale!! Naona kama kombe la dunia linakuwa la kawaida sana!!
Umekua na majukumu yamebana huwezi kuona rahaa ya kombe la dunia
 
Kukosekana kwa wachezaji fulani kwenye kombe la dunia kunachangia kutukosesha vionjo tulivyovitarajia. Kwa mfano kokosekana kwa mchezaji bora wa dunia kwa sasa Benzema (mtaalam wa kutupia), kukosekana kwa Halaand (mtupiaji mwenye mabavu), kukosekana kwa Mane (mtalaam wa kutupia), Kukosekana kwa Mohamed Salah (mshambuliaji machachari). Wachezaji hawa aidha ni majeruhi au mataifa yao hayakufuzu kuingia kwenye kinyang'anyiro cha kombe la dunia.
Nguli waliopo wamepoteza sana makali kama vile Christiano Ronaldo na Messi ambao hawapo kwenye kiwango chao kutokana na umri (pengine).
Kiukweli hakuna anayeweza kutusahaulisha vionjo kama vya kina Zinedane Zidane, Ronaldinho, Ronaldo original (the phenomenone), nk.

Kwa kweli vitu adimu hatujaviona kabisa hadi sasa!! Kwa wakongwe kwenye ushabiki wa soka wananielewa! Cross zenye macho na free kick kama za David Beckham zimekuwa simulizi za kale!! Naona kama kombe la dunia linakuwa la kawaida sana!!
Na hatuwezi kuja kuviona Kwa sababu siku hizi wachezaji hawachezi kuonesha vipaji vyao bali wanaucheza mfumo wa kocha

Sent from my 2201116TG using JamiiForums mobile app
 
Na hatuwezi kuja kuviona Kwa sababu siku hizi wachezaji hawachezi kuonesha vipaji vyao bali wanaucheza mfumo wa kocha

Sent from my 2201116TG using JamiiForums mobile app
Kudive kumezidi
Kujiangusha kwingi na kujifanya kuumia
Kadi za njano zingine na nyingi siyo halali

Ladha imepotea kwa asilimia kubwa tu

Kombe la Dunia la mwaka 1998 mpira ulikuwa dizaini ya mpira wa Saudi Arabia hivi na Japan wachezaji walijitoa sana
 
Be specific!! Hata hivyo ninaposema vitu adimu ni vitu adimu hasa!! Kwa mfano ni nani anaweza kuwaliwadha na kuwaburudisha watazamaji kama Ronadinho!!

Hebu angalia vionjo hivi:

Ukishamtaja babe wangu Ronaldinho gaucho ushanivuruga akili. Nilianza kuangalia mpira 2002 nikiwa mdogo madaftari yangu ya secondari yamechorwa picha za Ronaldinho bae
 
Back
Top Bottom