Kombani na Lissu Live on Star TV

Kama kila mtanzania atapata uhakika wa kupata chakula, maji, umeme, elimu na afya sina muda na katiba mpya hata raisi awe anasema aitwa muungu, sina time nae ili mradi basic rights are realized
Uelewa wako umatia mashaka, wewe ni kama mtu mwenye mke na mkewe ana mahusiano na Muuza duka (Mpemba) halafu yeye hajali akisema maadamu sukari na mchele vinapatikana bila jasho ya nini kusumbuka?
Jifunze kwanza katiba ni nini na haki zako kikatiba zapaswa kuwa nini kabla hujasema hayo uliyosema.
 
mweye kutupa videp tafadhali sana mtuwekee hapa,
jf ndio live tv yetu kwa tusio na tv
 
Wabunge nao akili mbovu kama wamekubali kujadili muswada wa katiba c wajadili mbona wanamjadili Tundu Lisu na chadema tu.du nahisi wamesahau kilichowaleta hebu mchek Wacla

kimsingi ccm wamepotoka, hawajui walitedalo, kodi zetu zinaangamia kwa ujinga wa watu wa watu wanaojiita wabunge!
 
Kwanini usifanyika mjadala huu wa Katiba ya Tz baina ya Chadema (Tundu lissu ) na CUF mwakilishi (Aboubakar Hamis) ili tujue mbivu na mbichi. Kwani siku zote Lissu anapewa watu dhaifu na hivyo kutumia nafasi hiyo kuinanga Znz na wa Znz .

Apambanishwe na Mh Abobakar Hamis ili asomeshwe ili kujua katiba ni nini?

Mmeo CCM kashindwa ww mke wake CUF utaweza?
 
Haya lini tena?? Umeme ndiyo umerudi Unguja muda huu..Nimekosa Mambo...?? Mchakato wa bidhaa used maadam ulishapita inabidi nitafute Generator sasa kuokoa jahazi....
 
Komban aliwahi kusema kuwa wanaodai katiba mpya ni watu wa mtaani wasio na kili nzuri. Namkubali mzee Mkinga alipoomba wanachuo wampe haki yake siku moja akiwa kwenye mjadala wa katiba mpya hapo UDSM.

Pinda nae alisema haoni tatizo na katiba iliyopo kwa sasa.

Wasira naye akasema katiba iliypo iko sawa na hatuhitaji katiba mpya

Mwnasheria mkuu naye akarudi kama wasira

JE, kuna sababu ya kuendelea kumwangalia kombani Star tv!? Hakuna kiongozi wa CCM aliye tayari kuona katiba mpya kwakuwa nchi hii ni yao. Ni kama shamba au plot yao wanaolithishana. Ni jukumu letu kuwaondoa madarakani alafu wakajibu mabaya yote wanayoendelea kutufanyia hasa wanapojilinda na ufisadi wao.


Unajua nimegundua sisi wabongo tuna tabia ya kusahau ama sio wafwatiliaji wa matukio ya bongo maana kwa mambo yaliokua yakitokea tangu mipango ya kudai katiba mpya mpaka kufikia leo tungekua na maswali maguma kwa hawa wahusika wakuu serekalini, ambao leo wanalazimisha CDM wajadili utumbo wao wanaouita mchakato wa kuelekea katiba mpya, hakika wasengekua na majibu ya msingi kwa nini walifoka na kupinga kwa kebehi hapo mwanzo na leo wanaushadidia ni mzuri ilhali hauna uwakilisha wa wazi na sawa kwa wadau wa katiba ambao ni raia, wanatuburuza ili wapitishe nini haswa? huo uharaka umetokea wapi wakati wao hawakuuweka mkakati huu wa katiba ktk sera zao 2020? tuamke nduguzanguni wabongo.,
 
Kama kila mtanzania atapata uhakika wa kupata chakula, maji, umeme, elimu na afya sina muda na katiba mpya hata raisi awe anasema aitwa muungu, sina time nae ili mradi basic rights are realized

Walibya walipewa zaidi ya basic needs na nchi iliyostawi kimaendeleo, lakini waliamua kuivuruga nchi na kumtoa Gaddafi madarakani. Ubinadamu ni zaidi ya basic needs-ukiridhika na hivyo unakuwa huna tofauti na ng'ombe!
 
Kama kila mtanzania atapata uhakika wa kupata chakula, maji, umeme, elimu na afya sina muda na katiba mpya hata raisi awe anasema aitwa muungu, sina time nae ili mradi basic rights are realized
pole rafiki yangu.nadhani siyo wewe kutakuwa na tatizo nyuma ya mawazo haya.ccm wanahitaji sana watu wa upeo wa aina yako.
 
Kwenye hotuba yake Bungeni Jumatatu yeye mwenyewe Lissu amesema Serikali ilitoa maagizo hayo, Lissu has some explaining to do:

"Mheshimiwa Spika...
Bunge - kwa kupitia Spika - liliigiza Serikali kufanya yafuatayo....iandae Muswada huu kwa lugha ya Kiswahili ili wananchi...

...kwa mujibu wa k
anuni ya 84(2) Kamati ilikwishaanza kupokea maoni ya wadau “...Kazi iliyokuwa imebaki kwa Kamati ilikuwa ni kutumia mamlaka yake chini ya kanuni ya 84(3) “... kufanya marekebisho katika Muswada wa Sheria kwa kumshauri Waziri ... anayehusika na Muswada huo kufanya mabadiliko....”

Kwa hiyo Lissu kasema Bungeni ( a ) Bunge lilitoa maagizo ...( b ) muswada ulishaanza kufanyiwa kazi na kamati... ( c ) Kanuni zinasema mwisho wa siku Waziri anayehusika na Muswada ndio anaefanya mabadiliko ya muswada . Sasa je:

( 1 ) Kama Bunge halikutoa maagizo muswada urudi kwa Kombani, nani kwa mfano angeutafsiri kwa Kiswahili, Tundu Lissu na Spika?

( 2) Kama hakuna Hansard za ruhusa ya Tume, kina Lissu walikuwa wanafanya nini wakati Kombani anaingia kuwaibia makabrasha ya muswada, walikuwa "wanatafakari" kama Wassira?

(3) Kama tume ya kina Lissu haikumpa Kombani muswada, na wala Kombani hakuingia kwenye makbrasha ya Tume kuiba muswada bali alifanya mabadiliko juu kwa juu akiwa wizarani (maana kila mtu ana nakala) ni kwa nini Tume iliacha kuendelea na kazi ikasubiri Kombani aka take over the marekebisho?

( 4 ) Kama Kombani anayo mamlaka ya kuzuia Tume isiendelee na kazi, Lissu atoe barua ya amri ya Kombani iliyowazuia kuendelea na kazi, na kama hana, Kombani kosa lake nini?
Rafiki Spika alivua joho la uspika na kuamua kufanya kazi za serikali,so huna haja ya kutumia nguvu kujua kombani aliupataje muswada huo ingawa ulikuwa mikononi mwa Kamati.Kumbuka pia Spika aliwaongeza kwenye kamati akina Hamad Rashidi kinyume kabisa na kanuni.
 
Vivaaaaaaaaaaaaaa, aluta Conitinuaaaaaaaaaaaaa

njaghamba iuhoma ilolo aghwida!
 
Komban aliwahi kusema kuwa wanaodai katiba mpya ni watu wa mtaani wasio na kili nzuri. Namkubali mzee Mkinga alipoomba wanachuo wampe haki yake siku moja akiwa kwenye mjadala wa katiba mpya hapo UDSM.

Pinda nae alisema haoni tatizo na katiba iliyopo kwa sasa.

Wasira naye akasema katiba iliypo iko sawa na hatuhitaji katiba mpya

Mwnasheria mkuu naye akarudi kama wasira

JE, kuna sababu ya kuendelea kumwangalia kombani Star tv!? Hakuna kiongozi wa CCM aliye tayari kuona katiba mpya kwakuwa nchi hii ni yao. Ni kama shamba au plot yao wanaolithishana. Ni jukumu letu kuwaondoa madarakani alafu wakajibu mabaya yote wanayoendelea kutufanyia hasa wanapojilinda na ufisadi wao.


Aaah! hawa jamaa hawajaweka kitufe cha like ila nimeukubali mchango wako. Mimi ninawaelewa sana hawa jamaa wa CCM kwa sababau haikuwa na sera ya katiba mpya kwenye manifesto yao na serikali yote imeshasema wazi kuwa hakuna haja ya katiba mpya. Mchakato unaoendelea ni wa KUHUISHA katiba iliyopo ili iendane na wakati.
 
quote_icon.png
By Barubaru
Kwanini usifanyika mjadala huu wa Katiba ya Tz baina ya Chadema (Tundu lissu ) na CUF mwakilishi (Aboubakar Hamis) ili tujue mbivu na mbichi. Kwani siku zote Lissu anapewa watu dhaifu na hivyo kutumia nafasi hiyo kuinanga Znz na wa Znz .

Apambanishwe na Mh Abobakar Hamis ili asomeshwe ili kujua katiba ni nini?

mtazamo wa KAFU ni nini katika muswaada huu?Angalia maoni ya naibu katibu mkuu wake BARA, Bw. Mtatiro vs.Maneno ya wabunge wA kAFU

Julius Mtatiro
Wadau wa masuala ya katiba,
Baada ya kuutaa muswada wa sheria ya uundwaji wa tume maalum itakayoshughulika na kukusanya maoni ya wananchi ili kuleta katiba mpya, Serikali imeandaa muswada mwingine ambao tayari ninao na ndio utawasilishwa bungeni hivi karibuni.
Muswada huu mpya umeingiza mambo kadhaa ambayo wadau waliyalalamikia kama vile:
1. Ushiriki sawa wa rais wa Zanzibar katika uteuzi kama ilivyo kwa rais wa muungano.
2. Muswada kuwa katika lugha za kiswahili na Kiingereza.
3. Kuwepo kwa bunge la katiba(japo wamelichanganya na wabunge wa sasa na wajumbe wa baraza la wawakilishi wa sasa).
4. Time frame zinazoeleweka kidogo n.k

Tatizo kubwa ambalo tunalikataa na bado serikali imelirudisha ni madaraka ya rais katika uundaji wa katiba mpya. u-Rais wa Tanzania ni cheo kinacholalamikiwa kuwa na madaraka makubwa mno, na sasa katika uandikaji wa katiba ya watanzania wote bado rais anapewa kusimamia kila kazi inayohusiana na katiba hii.

Tume ya taifa ya uchaguzi NEC na tume ya taifa ya uchaguzi ya Zaznibar ZEC bado zinapewa malaka yaleyale ya kusimamia masuala ya kura za maoni za wananchi wakati wa kupitisha katiba.

Serikali ya CCM ina kichwa kigumu sana, haisikii wala kusikiliza. Yaani tume ile ile inayochakachua matokeo ya uchaguzi kila kukicha ndiyo inapewa kazi ya kusimamia suala muhimu la katiba. Tume ya rais, katiba ya rais,nchi ya rais.

Ati mkuu wa wilaya, mtendaji wa kata,mtendaji wa kijiji na mtendaji wa mtaa ndio wanapewa kazi ya kusimamia taratibu za ukusanyaji wa maoni ngazi ya chini, ARE WE SERIOUS?

Kwani mpaka watu wabebe bunduki ndiyo serikali ione wananchi wanahitaji katiba mpya ya wananchi na siyo ya rais, DC,WEO,VEO,NEC,ZEC n.k?

Hivi ikulu ina hofu gani ikitengeneza utaratibu wa uhakika na wa haki wa kuleta katiba mpya? Kwa nini kila jambo katika kuleta katiba anapewa rais, kwa nini tusiunde tume maalum itakayoteuliwa kwa utaratibu maalum ikiwa na watu maalum ambao hata upatikanaji wao utatokana na uadilifu wao na watu hao watahojiwa kikamilifu live mbele ya watanzania wote katika televisheni n.k?

Kuna biashara gani katika ku-complicate hivi suala la katiba? Kwani serikali haijui ma-WEO, VEO, NEC, ZEC, DC, RAIS na kadhalika ni watu ambao wamelaumiwa sana kwa udhaifu mkubwa ambao wamekuwa wakiuonesha katika chaguzi mbalimbali na katika utendaji wao kwa ujumla kwa maana ya kuisaidia CCM?

Hivi sasa nchi inayumba sana kiuchumi, mfumuko wa bei, matatizo ya umeme na mauchafu kedekede, kwa nini rais wetu asishughulikie haya suala la katiba likawekwa katika mikono ya watu safi wanaoaminiwa na jamii ya watanzania?

Wasiwasi wangu ni kwamba, CCM wana hofu kuwa tukipata katiba ya haki ya ukweli ya maadili ya dira safi - wanajua wataondoka madarakani immediately. Lakini njia ya mwongo ni fupi sana, hii katiba ya RAIS na IKULU yake na chama CHAKE, tutaipinga kwa nguvu zote.

Kwa bahati mbaya hapa duniani, tangu ulimwengu uumbwe, haijawahi kutokea SERIKALI na MAJESHI yaliyowashinda wananchi wenye kiu ya haki na mabadiliko ambavyo ni haki yao.

TAFUTENI NAKALA YA MUSWADA HUU, SOMENI KWA MAKINI - SOTE TUCHUKUE HATUA KWA UMOJA WETU.

Julius Mtatiro,
26 Oktoba 2011.
 
Kwenye hotuba yake Bungeni Jumatatu yeye mwenyewe Lissu amesema Serikali ilitoa maagizo hayo, Lissu has some explaining to do:

"Mheshimiwa Spika...
Bunge - kwa kupitia Spika - liliigiza Serikali kufanya yafuatayo....iandae Muswada huu kwa lugha ya Kiswahili ili wananchi...

...kwa mujibu wa k
anuni ya 84(2) Kamati ilikwishaanza kupokea maoni ya wadau “...Kazi iliyokuwa imebaki kwa Kamati ilikuwa ni kutumia mamlaka yake chini ya kanuni ya 84(3) “... kufanya marekebisho katika Muswada wa Sheria kwa kumshauri Waziri ... anayehusika na Muswada huo kufanya mabadiliko....”

Kwa hiyo Lissu kasema Bungeni ( a ) Bunge lilitoa maagizo ...( b ) muswada ulishaanza kufanyiwa kazi na kamati... ( c ) Kanuni zinasema mwisho wa siku Waziri anayehusika na Muswada ndio anaefanya mabadiliko ya muswada . Sasa je:

( 1 ) Kama Bunge halikutoa maagizo muswada urudi kwa Kombani, nani kwa mfano angeutafsiri kwa Kiswahili, Tundu Lissu na Spika?

( 2) Kama hakuna Hansard za ruhusa ya Tume, kina Lissu walikuwa wanafanya nini wakati Kombani anaingia kuwaibia makabrasha ya muswada, walikuwa "wanatafakari" kama Wassira?

(3) Kama tume ya kina Lissu haikumpa Kombani muswada, na wala Kombani hakuingia kwenye makbrasha ya Tume kuiba muswada bali alifanya mabadiliko juu kwa juu akiwa wizarani (maana kila mtu ana nakala) ni kwa nini Tume iliacha kuendelea na kazi ikasubiri Kombani aka take over the marekebisho?

( 4 ) Kama Kombani anayo mamlaka ya kuzuia Tume isiendelee na kazi, Lissu atoe barua ya amri ya Kombani iliyowazuia kuendelea na kazi, na kama hana, Kombani kosa lake nini?

Tume iliundwa lini wakati ndio mjadala wa kuunda tume unashindaniwa Bungeni? Au ulimaanisha kamati ya katiba na sheria?
 
Walibya walipewa zaidi ya basic needs na nchi iliyostawi kimaendeleo, lakini waliamua kuivuruga nchi na kumtoa Gaddafi madarakani. Ubinadamu ni zaidi ya basic needs-ukiridhika na hivyo unakuwa huna tofauti na ng'ombe!

nimepata kitu hapo..good good 2 my side
 
Studio na 3 Dodoma alikuwepo Lissu,Kombani na Mwanaharakati mmoja toka kituo cha sheria na haki za binaadam,Studio na.2 alikuwepo Paul Mabuga na Mwanaharakati mmoja.Kombani kimsingi kabisa anasema anakubaliana na mawazo ya akina Lissu,ila angependa akina Lissu wawepo Bungeni ili waujadili kwa pamoja.Lissu anasema kuwepo kwao Bungeni ni sawa na kuubariki,kuhalalisha mswada ambao kimsingi ni haramu kwa kuwa umekiuka kanuni za kudumu za bunge na haujafuata matakwa ya wananchi ambao kimsingi ndo wanaipa madaraka serikali.

Komboni anasema muswada ni halali kwani serikali iliagizwa na bunge kufanya marekebisho,alivyouliza aeleze ni hansadi ipi na ya tarehe ngapi ambayo imelekodi maagizo hayo akaishia kukenua kwa aibu.kuhusu wananchi kutoa maoni yao Kombani anasema ana file kubwa lenye maoni ya wananchi.alipoulizwa maoni hayo kama ni ya muswada uliosomwa bungeni mwezi wa nne au huu wa mwezi wa kumi na moja,hakutoa majibu.Kwa ujumla Kombani hakuongea lolote la maana zaidi ya kuinama na kucheka cheka nahisi ilikuwa aibu pamoja na maswali ya haja aliyoulizwa na watangazaji.

Mungu tusaidie watanzania,Kiukweli kwa Serikali hii,tusipoweka woga wetu kando,tutaangamia.

AMANI HAIJI ILA KWA NJIA YA UPANGA-----------KIjua ndicho hiki Usipouanika

Hahahah 'utautwanga mbichi' - RIP Mzee Jongo
 
Kwanini usifanyika mjadala huu wa Katiba ya Tz baina ya Chadema (Tundu lissu ) na CUF mwakilishi (Aboubakar Hamis) ili tujue mbivu na mbichi. Kwani siku zote Lissu anapewa watu dhaifu na hivyo kutumia nafasi hiyo kuinanga Znz na wa Znz .

Apambanishwe na Mh Abobakar Hamis ili asomeshwe ili kujua katiba ni nini?

Mkuu huyu Abobakar Hamis ndiyo waziri wa JK mwenye dhamana ya katiba siyo? na counterpart wake waziri kivuri ni Lissu eenh!. Tatizo watu tunaweka ushabiki mbele bila kungalia logic, ushauri huu mpatie JK amuweke huyo A Hamis kuwa waziri wake wa katiba ili apambane na Lissu.

Otherwise utakuwa umeongea kishabiki zaidi and great thinking has lost signal in your post.
 
Back
Top Bottom