Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 6,132
- 10,514
Ni Desemba 16, 2025, Kampuni ya Meta ilithibitisha rasmi kupokea ombi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) la kukata kodi ya asilimia 5 kwa kila malipo yanayolipwa kwa Watengeneza Maudhui (Content Creators) wanaoishi Tanzania. Utekelezaji wa mfumo huu unaanza Desemba 21, 2025, hatua inayozua mjadala mpana kuhusu mustakabali wa ubunifu wa kidijitali nchini.
Kwa mujibu wa utaratibu huu, mtengeneza maudhui aliyepaswa kulipwa TSh milioni mbili atalazimika kukabidhi TSh 100,000 kama kodi, bila kujali ukubwa wake au changamoto alizopitia kufikia kiwango hicho. Makato haya yanahusu mapato yanayotokana na programu za Facebook kama Stars, Subscriptions, Bonuses na Content Monetisation Beta, pamoja na Instagram kupitia Gifts, Subscriptions na Bonuses.
Meta inajiunga na YouTube, ambayo tayari imeanza makato ya aina hii tangu Julai 2025. Hata hivyo, swali kubwa linalobaki ni: Je mfumo huu unahamasisha ubunifu au unauua kabsa?
Kwa uhalisia, kodi hii inaumiza zaidi watengeneza maudhui wadogo—wale wanaojitahidi kukuza akaunti zao, kununua vifaa, intaneti na muda. Asilimia 5 kwa mkubwa na mdogo ni sawa kisheria, lakini kiuchumi ni pengo kubwa. Mbaya zaidi, makato haya yanakuja juu ya mlolongo mrefu wa kodi zingine: vocha, miamala ya simu, benki na huduma za mtandao ambazo poa TRA huchukua kodi.
Badala ya kujenga mazingira rafiki ya uchumi wa kidijitali, hatua hii inaonekana kama kukata tamaa ya ubunifu kabla haujakua. TRA inaonekana mahiri sana katika kubuni njia za kukusanya kodi, lakini dhaifu katika kueleza wazi matumizi ya fedha hizo kwa maendeleo ya wananchi.
Swali la msingi linabaki: Je Tanzania inataka kukuza uchumi wa ubunifu au kuudhibiti mpaka ufe? Kama sera hazitatazamwa upya, huenda ndoto ya vijana wengi wa kujitegemea kupitia maudhui ya mtandaoni ikabaki kuwa hadithi tu. Wataalamu wenu wa masuala ya ushauri wa kodi wanawashauri vitu gani?
Kwa mujibu wa utaratibu huu, mtengeneza maudhui aliyepaswa kulipwa TSh milioni mbili atalazimika kukabidhi TSh 100,000 kama kodi, bila kujali ukubwa wake au changamoto alizopitia kufikia kiwango hicho. Makato haya yanahusu mapato yanayotokana na programu za Facebook kama Stars, Subscriptions, Bonuses na Content Monetisation Beta, pamoja na Instagram kupitia Gifts, Subscriptions na Bonuses.
Meta inajiunga na YouTube, ambayo tayari imeanza makato ya aina hii tangu Julai 2025. Hata hivyo, swali kubwa linalobaki ni: Je mfumo huu unahamasisha ubunifu au unauua kabsa?
Kwa uhalisia, kodi hii inaumiza zaidi watengeneza maudhui wadogo—wale wanaojitahidi kukuza akaunti zao, kununua vifaa, intaneti na muda. Asilimia 5 kwa mkubwa na mdogo ni sawa kisheria, lakini kiuchumi ni pengo kubwa. Mbaya zaidi, makato haya yanakuja juu ya mlolongo mrefu wa kodi zingine: vocha, miamala ya simu, benki na huduma za mtandao ambazo poa TRA huchukua kodi.
Badala ya kujenga mazingira rafiki ya uchumi wa kidijitali, hatua hii inaonekana kama kukata tamaa ya ubunifu kabla haujakua. TRA inaonekana mahiri sana katika kubuni njia za kukusanya kodi, lakini dhaifu katika kueleza wazi matumizi ya fedha hizo kwa maendeleo ya wananchi.
Swali la msingi linabaki: Je Tanzania inataka kukuza uchumi wa ubunifu au kuudhibiti mpaka ufe? Kama sera hazitatazamwa upya, huenda ndoto ya vijana wengi wa kujitegemea kupitia maudhui ya mtandaoni ikabaki kuwa hadithi tu. Wataalamu wenu wa masuala ya ushauri wa kodi wanawashauri vitu gani?