CCM wamesha tuona sisi ni bendera fuata upepo.
Wanatuendesha kwa remote control a.k.a kitendambali
kijana kwenye hili atakayekuunga mkono ni chizi na limbukeni, jalibu kufikilia babu na bibi zako uliowanunulia simu ili huwe unawajulia hali acheni upumbavu, mnafaham hadi sasa kodi ya vocha za sim ni kiasi gani au unaongea tu ili uonekane? acha UNYANTIRANaungana na Juliana Shonza bora serikali ikate toka mwezi wa kwanza mwaka huu 2013. Watumiaji simu tupo kama 7mil sasa ukichukua 7m * 1000* 3=21B . Hapo tayari ushatengeneza kilometa 26 za barabara Serikali oyee Ahsanteni
da umenena, ilo nalo neno, ktk kila elfu moja kodi ni Tshs. 300 mnaitaji kuona wananchi hawapigi sim?bora mie niko bongo lakini natumia laini ya safaricom na airtel ya kenya.
Nimehangaika kusoma thread kumbe source ni jarida la udaku wa kisiasa?
Anyway najisikia fahari kuchangia pato la nchi kwa maendeleo ya nchi yangu
Naomba kukatwa kuanzia mwezi wa kwanza mwaka huu.
Nawasilisha.
Hahaaaa eti vipesa vyakupaka rangi kucha ,we unajua hayo tu ndo upeo wako wakufikiri ulipofikia na ww.
Serikali isiyokusanya kodi ni legelege
ccm si serikali legelege ni lazima ikusanye kodi ili kupush maendeleo
Tatizo lenu mnaleta mahaba ya vyama kwenye mambo ya msingi,kila kitu mmezoea kupinga.
kwakifupi hamueleweki.
Tozo liko palepale
Ni kuwaumbua tu hapo 2015kaka hawa ccm tuwafanyaje jamani kwanini wanatuendesha kama golikipa anavyoendeshwa uwanjani kuangalia mpira utaingia golini au la? wameniuzi sana tena sana hawajui kuwa kuna watu ambao wanategemea simu kula ugali
Mnalalamika umeme haujafika vijijini halafu hamtaki kukatwa
This time mtakatwa tu
Nimesoma habari kwenye mitandao ya kijamii kuwa serikali ya Jamuhur ya Muungano wa Tanzania imeridhia tozo ya kila mwezi ya kadi za cm ambayo ni Tsh 1000.Je haya ndo maisha bora yaliyoahidiwa na serikali?Inashangaza kuwa tozo hyo inaanza mwez october kwa sharti la kukata kodi hyo kuanzia mwez july mwaka huu.Hivyo wananch watatozwa sh 3000 kwa maana ya july,august na septemba.Namfikiria sana bibi aliye kijijin kwetu kule Sungwizi mkoani Tabora anayesubiri kupigiwa tu.Haya ndo maisha bora tuliyoahidiwa na serikal ya chama cha mapinduzi.Sitaki kuamin kama viongoz wang wa serikali ni wavivu wa kufikiri.Kwel wameshndwa kubuni vyanzo vingne vya mapato mpaka kwenye tozo ya kadi za cm?wazibe mianya ilyopo sekta mbalmbali kama vle bandari,wafanya biashara wakubwa walipe kodi,wawadhibiti wakusanya mapato ipasavyo kwan wanapiga dili nying.Zipo sehem nying ambazo zipo zipo tu bila usimamizi wa kutosha.Serikal kuruhusu tozo za kadi za cm ni kuwaonea wananchi.Serikal ifikirie vyanzo vngne vya mapato.Waache uzembe!!
Wakati mwingine hizi sumu ya siasa ni sawa na ya Alshababu au Alkaida.Mtu unatetea uovu kama huna akili nzuri!? Hivi ni njaa au ni ugonjwa?!
Kuna mambo mawili yataigalimu sana Ccm kwenye.uchaguzi wa 2015. Swala la katiba iwapo watazidi kucheza rafu na kodi ya simcard!
machungu ya kiwango hiko hayanabudi kutokea ili ule mwisho wao upate kufika kirahisi ! haya shime wananchi, haya shime wapinga ufisadi , akili ndogo haiwezi kutawala akili kubwa...wameshindwa kutoza vyakutosha kwenye Gas, Dhahabu na Maliasili wanatusukumia mizigo wananchi