Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,926
- 31,169
Kobe mkubwa anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka zaidi ya 120, (pichani), bado anaendelea kuishi kwenye shamba la kahawa la Kibo na Kikafu, Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro.
Kobe huyo anadaiwa kuwa na nguvu kubwa kiasi cha kuweza kuangusha hata baadhi ya vitu likiwemo gari.
Inadaiwa kwamba kobe huyo amekuwepo katika shamba hilo tangu enzi za ukoloni kabla ya Tanzania haijapata uhuru.
Meneja wa shamba hilo lenye ukubwa wa ekari 2,054, Jackson Matenge, alisema kobe huyo anajulikana kwa jina la Tony na kwamba hivi karibuni alionyesha uwezo wake baada ya kulipindua lori la tani saba na kusababisha ajali.
Alisema kobe huyo alikuwa amelala barabarani ambapo lori hilo liliegeshwa mahali alipokuwepo na aliponyanyuka, alilipindua lori hilo lakini hakuna mtu aliyepoteza maisha wala kujeruhiwa.
Naye Mwenyekiti wa Vyama vya Msingi vya Masama Saawe, Modio na Masama, Roo na Sonu Ngira, Hatibu Mwanga, alisema mwaka 1952 akiwa na umri wa
miaka minne, walikuwa wakicheza na kobe huyo akiwa mkubwa kama alivyo na kwamba hadi sasa ana miaka 58 lakini bado ana nguvu.
Alisema wakoloni waliokuwa wanamiliki shamba hilo kabla ya serikali kuyataifisha mwaka 1975, ndio waliomuweka shambani humo ambapo baada ya kuondoka walirudi na kutaka kumnunua kwa zaidi yaSh. milioni 100 lakini wanachama walikataa na kudai kuwa hiyo ni sawa na hirizi ya shamba hilo.
Alisema wazungu hao walirudi tena na kuomba kuuziwa kobe huyo lakini bado walikataliwa na kwamba idadi kubwa ya wazungu hufika katika shamba hilo kwa ajili ya kumuona kobe huyo na kupiga naye picha.
Kwa upande wake, Mkuu wa wilaya hiyo, Dk. Norman Sigalla aliutaka uongozi wa shamba hilo kumjengea mazingira mazuri ya kuishi kobe huyo ili aweze kutumika kama sehemu ya utalii kwa watalii wa ndani na nje.
CHANZO: NIPASHE
Duh hii kali wanaoishi karibu na hilo shamba tunaomba habari za huyu kobe
Kobe huyo anadaiwa kuwa na nguvu kubwa kiasi cha kuweza kuangusha hata baadhi ya vitu likiwemo gari.
Inadaiwa kwamba kobe huyo amekuwepo katika shamba hilo tangu enzi za ukoloni kabla ya Tanzania haijapata uhuru.
Meneja wa shamba hilo lenye ukubwa wa ekari 2,054, Jackson Matenge, alisema kobe huyo anajulikana kwa jina la Tony na kwamba hivi karibuni alionyesha uwezo wake baada ya kulipindua lori la tani saba na kusababisha ajali.
Alisema kobe huyo alikuwa amelala barabarani ambapo lori hilo liliegeshwa mahali alipokuwepo na aliponyanyuka, alilipindua lori hilo lakini hakuna mtu aliyepoteza maisha wala kujeruhiwa.
Naye Mwenyekiti wa Vyama vya Msingi vya Masama Saawe, Modio na Masama, Roo na Sonu Ngira, Hatibu Mwanga, alisema mwaka 1952 akiwa na umri wa
miaka minne, walikuwa wakicheza na kobe huyo akiwa mkubwa kama alivyo na kwamba hadi sasa ana miaka 58 lakini bado ana nguvu.
Alisema wakoloni waliokuwa wanamiliki shamba hilo kabla ya serikali kuyataifisha mwaka 1975, ndio waliomuweka shambani humo ambapo baada ya kuondoka walirudi na kutaka kumnunua kwa zaidi yaSh. milioni 100 lakini wanachama walikataa na kudai kuwa hiyo ni sawa na hirizi ya shamba hilo.
Alisema wazungu hao walirudi tena na kuomba kuuziwa kobe huyo lakini bado walikataliwa na kwamba idadi kubwa ya wazungu hufika katika shamba hilo kwa ajili ya kumuona kobe huyo na kupiga naye picha.
Kwa upande wake, Mkuu wa wilaya hiyo, Dk. Norman Sigalla aliutaka uongozi wa shamba hilo kumjengea mazingira mazuri ya kuishi kobe huyo ili aweze kutumika kama sehemu ya utalii kwa watalii wa ndani na nje.
CHANZO: NIPASHE
Duh hii kali wanaoishi karibu na hilo shamba tunaomba habari za huyu kobe