KKKT: kufungisha ndoa mnatoza 100,000/=!

KKKT: kufungisha ndoa mnatoza 100,000/=!

Kuna rafiki yangu mmoja ameamua kubariki ndoa, hii ni baada ya kuishi katika ndoa ya Kimila kwa mwongo mmoja! Ila hasa na mashinikizo ya kidini kuwa ni lazima wafunge ndoa kanisani ili wakamilike kiroho. Sasa alipokwenda kanisani ndio kakumbana na hiyo hela kama sehemu ya masharti. Ameogopa akajua anaibiwa.

Ndio kanifuata mimi "mzee wa Kanisa " kuuliza hili ni tozo gani! Ama kweli katika ufahamu wangu wa Kanuni za KKKT hii kwangu ni mpya.

Hebu mnijuze naogopa kumpigia mchungaji kuuliza !Kam ndiyo ilivo mh....!Tafadhali tuchangie kwa staha bila jazba.

Mbona pombe mtakunywa za mil.3?
 
Kuna rafiki yangu mmoja ameamua kubariki ndoa, hii ni baada ya kuishi katika ndoa ya Kimila kwa mwongo mmoja! Ila hasa na mashinikizo ya kidini kuwa ni lazima wafunge ndoa kanisani ili wakamilike kiroho. Sasa alipokwenda kanisani ndio kakumbana na hiyo hela kama sehemu ya masharti. Ameogopa akajua anaibiwa.

Ndio kanifuata mimi "mzee wa Kanisa " kuuliza hili ni tozo gani! Ama kweli katika ufahamu wangu wa Kanuni za KKKT hii kwangu ni mpya.

Hebu mnijuze naogopa kumpigia mchungaji kuuliza !Kam ndiyo ilivo mh....!Tafadhali tuchangie kwa staha bila jazba.

Nijuavyo mimi unachajiwa hela ya cheti cha ndoa pamoja kulipa zaka ..hii nimeiona catholic church..
 
Whatever na mambo ya martin luther. Mie nashangaa kwa nini mchungaji wangu hajawaza ac kanisani. Kama nyumbani naweka ac na kwenye gari nnayo, si itakuwa safi nikipata kiyoyozi kanisani?
Kuna dhambi kuenjoy ya dunia? Kama Bible inasema nchi na vyote viijazavyo dunia (i bet hata dhahabu na fedha ) ni mali ya bwana. Na sie ni wana wa huyo Baba. Sasa nani akavienjoy kama sio sie? Kajifunze nguvu ya sadaka manake wema hauozi atii
Nini kilimfanya Martin Luther kulihama Kanisa Katoliki na kuanzisha hili Kanisa ?
Ni haya ambayo yanahojiwa hapa.
Kanisa kuanza kuwekeza kwenye mambo ya kidunia ndiko kunaleteleza Ukengeufu wa kuanza kuuza huduma za kiroho.
Kanisa kuongozwa na wanadamu ambao mawazo yao yamejikita kuimarisha kesho ya kidunia ndiyo msingi wa Ukengeufu.
Kanisa limepoteza dira liko kwenye ushindani wa majengo mazuri na fahari za kidunia huku likijitenga na Kweli ya Bwana Wetu Yesu Kristo.
Waamuni wanatoa sadaka na matoleo mengi mengi kila wiki ni uwekezaji mbaya na priority za kidunia zinazofanya Kanisa lionekane linapungukiwa.
Hakika Kanisa limepoteza wito imebaki kuwa kijiwe cha kufarijiana ujinga...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom