KIWIRA na MCHUCHUMA: A Campaign To Reclaim...

Hili ni funzo na weakness ya nchi nyingi za third world,kwanini tumtegemee mtu mmoja (raisi) kupambana au kuwa deal breaker wa wa mambo kama haya,tunahitaji very strong insitution ambazo ni fair,smart & independent ambazo upuuzi kama huu ukitokea ni straight up zinajua kazi yake na wala sio raisi au bunge....ingekuwa nchi kama US usingesikia jina la president wala nini sana sana kama yeye ni fisadi jamaa wangeenda after yeye na kumshtaki Congress ila vifisadi vingine vyote leo vingekuwa subpoenaed followed by heavy prosecution,huu ufisadi ni loopholes nyingi ambazo zipo kwenye consitution yetu,kazi wajomba tunayo maana kujenga taifa imara sio hizi temporary fix,inabidi tuanzie na katiba yetu ambayo itakuwa na check & balance sio ubabe wa mtu mmoja ambaye anaonekana kama mungu mtu na nchi nzima inategemea yeye maamuzi yake...je akiwa mjinga si ndio tumekwisha.
 
Ahsante Slaa, hao ndiyo alowarithisha nyerere ufisadi, mimi nalalamika na nyerere tuu, mpaka kufa, yeye ndie aliyetutakia yote haya. M/mungu amuweke popote atakapo.
 
Koba: Nimekusoma!

Mambo hayoko solid and clear. Wala hayako Straight f.

Yamekaa kiswahili mno.

JKikwete alikuwa confronted na media wakati fulani amuwajibishe Mkapa. nafikiri lilikuwa ni swali. You know what he said. Hatafutilia hilo jambo. For Gods sake anatowapi hiyo nguvu ya kujibu kama vile yeye ni Mungu? Kiweke anajua fika what happened yet Kwa Mkapa! lakini anaamua kuchuna.. mambo ya kishwahili tu!! tumuache mzee astaafu kwa amani...! You see! we need somthing very OBJECTIVE here! Sio kama mtu anavyojisikia...Ni kamasheria fulani ya nchi inavyosema..sasa Prez' ana nguvu kama nini!

1.We need new constitution!Itakayo deal na swaala la uogozi wa Taifa very objectively

2.Tunataka pia wananchi waamke na ku_voice this out.

vingine tunapokwenda tutahitaji nguvu kubwa sana kurekbisha mambo. better now kabla hayajaharibika zaidi.
 
Very strong points, heshima mbele kwa Dr. Slaa, a true mpinzani bongo, abarikiwe tu!

Dr Slaa on Kiwira mine takeover saga: ’Mkapa should be held accountable’

1. Dr Wilbrod Slaa yesterday challenged President Jakaya Kikwete to hold his predecessor, Benjamin Mkapa, accountable for ’illegally’ acquiring the Kiwira coal mine in Mbeya Region.

2. that Mkapa’s move to privately acquire the Kiwira mine while still in power was a violation of the national Constitution.

3. that President Kikwete take appropriate disciplinary measures against both the ex-president and his apparent associate in the Kiwira mine takeover, former energy and minerals minister Daniel Yona.

4. The two are understood to have jointly registered a private company called Tanpower Resources Company Limited, with various close relatives including wives, children and in-laws in tandem,

5. in 2004 and the same company then went on to acquire 85 per cent of shares in the Kiwira mine after its privatization.

6. It has also been established that during both the Tanpower Resources establishment and Kiwira coal mine privatization processes, Mkapa and Yona were still serving as president and minister for energy and minerals, respectively.
 
Ahsante Slaa, hao ndiyo alowarithisha nyerere ufisadi, mimi nalalamika na nyerere tuu, mpaka kufa, yeye ndie aliyetutakia yote haya. M/mungu amuweke popote atakapo.

Nikiwa chekechea kuna mwalimu mmoja (wa somo la kuandika) ambaye kila mara kabla ya kufundisha alikuwa anaanza kumlaumu baba yake kuwa ndiye amemsababisha awe mwalimu wa chekechea.

Yeye kila wakati anaanza kulialia kuwa kama baba yake angesoma na kupata kazi serikalini basi mwalimu wetu angekuwa somebody somewhere akila kuku kwa mlija. Cha kusikitisha zaidi, mwalimu wetu alikuwa in the twenties, yaani akiwa kabisa na nafasi ya kurudi shule akasoma mpaka chuo kikuu na kuwa somebody huko somewhere anakotaka kuwa.

Miaka ya karibuni nimeanza kumkumbuka mwalimu wangu nikaconclude kuwa muda mwingi alioutumia nasi (vitoto vichanga) ulimuharibu akili yake na kumfanya alielie kila wakati kama kitoto kichanga tu badala ya kufanya something about matatizo yake.
 
poor Mkapa anatia huruma sana,tamaa gani ya kuiba mabilioni yote hayo,mtu mwenyewe miaka zaidi ya 70 na hujawahi kushika pesa zote hizo sasa sijui anataka mzee huyu? bora angetuliza tuu na tungemtunza kwa heshima zote lakini sasa kila akipita anaonekana fisadi tuu na sijui hata kama anaweza kusema chochote sasa watu wakamsikiliza,akiwa mjanja arudishe mgodi kimya kimya tutamsamehe
 
Ahsante Slaa, hao ndiyo alowarithisha nyerere ufisadi, mimi nalalamika na nyerere tuu, mpaka kufa, yeye ndie aliyetutakia yote haya. M/mungu amuweke popote atakapo.


Nyerere hakuwa fisadi na enzi zake watu kama hawa wenye kashfa nzito kama hizi angeshawafukuza kazi zamani kwa manufaa ya umma. Nyerere kama binadamu hakuwa perfect lakini msimtwishe lawama asizozistahili.
 
Kuwafukaza kazi haitoshi, kwani Nyerere si alisema, "it ca be done play your party"

kipi kizuri alichokifanya nyerere? Jee, hakupeleka watu wakaliwa na simba, chui na kung'atwa na nyoka? huo kama si ufisadi ni nini? Au hujuwi system ni nini?
 
kuwafukaza kazi haitoshi, kwani Nyerere si alisema, "it ca be done play your party"

kipi kizuri alichokifanya nyerere? Jee, hakupeleka watu akauliwa na simba, chiu na kung'atwa na nyoka? huo kama si ufisadi n nini? Au hujuwi system ni nini?

huh!? Son, you don't remember anything good Nyerere did for our beloved country!? :confused:
 
Koba: Nimekusoma!

Mambo hayoko solid and clear. Wala hayako Straight f.

Yamekaa kiswahili mno.

JKikwete alikuwa confronted na media wakati fulani amuwajibishe Mkapa. nafikiri lilikuwa ni swali. You know what he said. Hatafutilia hilo jambo. For Gods sake anatowapi hiyo nguvu ya kujibu kama vile yeye ni Mungu? Kiweke anajua fika what happened yet Kwa Mkapa! lakini anaamua kuchuna.. mambo ya kishwahili tu!! tumuache mzee astaafu kwa amani...! You see! we need somthing very OBJECTIVE here! Sio kama mtu anavyojisikia...Ni kamasheria fulani ya nchi inavyosema..sasa Prez' ana nguvu kama nini!

1.We need new constitution!Itakayo deal na swaala la uogozi wa Taifa very objectively

2.Tunataka pia wananchi waamke na ku_voice this out.

vingine tunapokwenda tutahitaji nguvu kubwa sana kurekbisha mambo. better now kabla hayajaharibika zaidi.

Kikwete hajakosea, angeanza na kumfuatilia mwinyi kwanza, aliyesema kila kitu "ruksa" halafu angemfatilia nyerere aliyetutia kwenye ujinga na umasikini usio kifani na hali sisi ni matajiri.

Mkapa kakomba, hakuna raisi wa tanzania aliejitajirisha kama mkapa, lakini looooh, wote kimya, au kwa kuwa yeye ni mwana wa ....

Kikwete, ndie mkuu pekee aliyeweza kuwabainisha kina balali, kwani balali aliiba wakati wa kikwete? Kikwete pekee ndie aliye-anza kuwaweka wapinzani kwenye kamati za serikali inayo-ongoza. Jee, yote hamuyaoni hayo? au hamuijuwi system ni nini?
 
Nyerere hakuwa fisadi na enzi zake watu kama hawa wenye kashfa nzito kama hizi angeshawafukuza kazi zamani kwa manufaa ya umma. Nyerere kama binadamu hakuwa perfect lakini msimtwishe lawama asizozistahili.
Nyerere ndie fisadi wa kwanza kwenye nchi hii, na nyerere ndiye aliyeifanya nchi hii kuwa masikini wa kutupwa. Sijuwi kwa nini alivalishwa suruwali na wanajiji la Dar es Salaam wakati alikuwa hana asili ya kuvaa suruwali?
 
poor Mkapa anatia huruma sana,tamaa gani ya kuiba mabilioni yote hayo,mtu mwenyewe miaka zaidi ya 70 na hujawahi kushika pesa zote hizo sasa sijui anataka mzee huyu? bora angetuliza tuu na tungemtunza kwa heshima zote lakini sasa kila akipita anaonekana fisadi tuu na sijui hata kama anaweza kusema chochote sasa watu wakamsikiliza,akiwa mjanja arudishe mgodi kimya kimya tutamsamehe
Mkapa si alipewa ukuu na nyerere, wakati kura zote za maoni zilimtaka Kikwete! sasa unalalamika kuwa kikwapa ndio mwizi? ajabu ganui hii? si aliwekwa na nyerere, au system huijuwi ni nini?
 
Kama Nyerere ni fisadi basi neno fisadi halina maana duniani.
Kweli kabisa, ufisadi ulianza kwa nyerere, hao wanaoitwa mafisadi leo hii kawafichuwa kikwete. Jee wakati wa nyerere ni fisadi gani aliyefichuliwa? au wakati wa mkapa ni fisadi gani aliyefichuliwa? mafisadi wanafichuliwa na kikwete, ndio, kikwete ndye aliye-wafichuwa. Au unatatizo na hilo? Jee, huijuwi system ni nini?
 
Slaa Mungu akupe maisha marefu uenelee kuitetea Tanzania tajiri lakini inamilikiwa na watu wachache na wake na watoto wao na marafiki zao .Mimi nasema saga la BTO JK has failed before hakujakucha . Hana lolote na Kiwira ndiyo hatagusa kabisaaaaaaaaaaaaaa
kumbuka, wakati wa JK ndio unajuwa kuwa kuna-saga BoT, Jee unafahamu kuwa wakati wa nyerere BoT iliibwa mpaka ikawashwa moto? na hakuna kilichotokeya, si tume wala uchunguzi wala kupelekwa mtu mahakamani wala kufukuzwa mtu kazi! kwa hili nani bora? nyerere au kikwete?
 
With all due respect ZOMBA

Nimesoma Post zaidi ya ishirini kama sijakosea-kwa uzomba wako unanga'nga'nia sistem ni nini-mii naelewa sistem ni nini

1) Hauomo kwenye system yeyote

If you are trying to lay a groundwork for a system you're advocating for-which I belive does not exist- You have failed.

Ukifikia sehemu unaleta mzaha-huna sehemu ya System yako hapa-You have failed.

Sasa wewe upo kwenye system gani? Free swinging?
Asante
 
With all due respect ZOMBA

Nimesoma Post zaidi ya ishirini kama sijakosea-kwa uzomba wako unanga'nga'nia sistem ni nini-mii naelewa sistem ni nini

1) Hauomo kwenye system yeyote

If you are trying to lay a groundwork for a system you're advocating for-which I belive does not exist- You have failed.

Ukifikia sehemu unaleta mzaha-huna sehemu ya System yako hapa-You have failed.

Sasa wewe upo kwenye system gani? Free swinging?
Asante
Mimi, system ninayo-elezeya ni Political system.

Na sina mzaha, haya ni mambo yanayomgusa kila m-Tanzania.

Au huijuwi system ni nini?
 
Haya unipata hiyo wana JF ndo weshaanza kuendeleza ufisadi wao; kweli mchimba mgodi makaa ya mawe analipwa Shs 48,000 kwa mwezi halafu tena unamdhulumu kwa kutokumlipa??

Mungu atusaidie


Mgodi wa Kiwira kunafuka moshi

na felix mwakyembe, mbeya
Mtanzania Jan 22, 2008


UHUSIANO baina ya uongozi wa Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira mkoani Mbeya na jamii inayouzunguka pamoja na wafanyakazi wake unaonyesha wazi si mzuri, bali umetawaliwa na chuki na uhasama.

Hali hiyo ilijidhihirisha mwishoni mwa wiki, katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na Kamati ya Rais inayopitia sekta ya madini nchini, ambako wananchi na wafanyakazi walimshutumu hadharani Meneja Mkuu wa mgodi huo, Adam Abdu, kwa ufanisi duni wa mgodi na wafanyakazi kutolipwa haki zao.

Mchungaji Israel Mwakisabwe ni miongoani mwa wananchi ambao walijitokeza kueleza hali hiyo mbele ya wajumbe wa Kamati hiyo ya Rais, ambako alisema Meneja Mkuu huyo, ndiye kiini cha chuki na uhasama uliopo kati ya wananchi, wafanyakazi kwa upande mwingine dhidi ya uongozi wa mgodi huo, pamoja na wawekezaji wake kwa ujumla.

“Wananchi na wafanyakazi wa Kiwira Coal Mine hawajakombolewa, wanahitaji ukombozi, kwanza huyu Meneja Mkuu ana lugha chafu, husikika akisema wazi kwamba hao Wanyakyusa waache tu, wajinga,” alisema Mchungaji Mwakisambwe.

Madai ya wananchi hao yanalingana na yale ya wafanyakazi wa mgodi huo yaliyowasilishwa kwenye Kamati hiyo kwa maandishi, yakionyesha madai yao ya zaidi ya Sh bilioni 47 pamoja na mishahara duni. Kima cha chini cha mshahara mgodini hapo ni Sh 48,000.

Wafanyakazi wa mgodi huo walidai kuwa pamoja na Serikali kutangaza kima cha chini cha Sh 350,000 kwa wafanyakazi wa migodini, uongozi wa mgodi huo umekataa kulipa kiwango hicho na kutishia kufunga mgodi. Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Iddi Simba, alilazimika kumwita tena kiongozi wa Chama cha Wafanyakazi aliyefahamika kwa jina la Kibona, kusoma taarifa yao mbele ya mkutano huo, ili madai yaliyomo yathibitishwe na wafanyakazi wote na wananchi, baada ya kusomwa wote walikubaliana nayo.

Madai mengine yaliyotolewa na wananchi wa vijiji vinavyouzunguka mgodi huo ni kutonufaika kwao na uwepo wa mgodi huo, wakitoa mfano wa huduma za jamii kama vile kukosa umeme, japokuwa unazalishwa kwenye mgodi huo, na huduma nyingine za kijamii kama vile elimu, afya na maji.

Ilielezwa bayana kwenye mkutano huo uliohudhuriwa vile vile na uongozi na mwekezaji wa mgodi huo, kuwa miongozi mwa wafanyakazi 600 wa mgodini hapo, ni 10 tu ndio walioajiriwa, wanaobaki ni vibarua wanaojaza mikataba ya mwezi mmoja mmoja.

Awali Mkurugenzi wa Mgodi huo, Evans Mapundi, aliwaeleza wajumbe wa Kamati hiyo ya Rais kuwa Mgodi huo wa Kiwira, ni mradi wa wazalendo wenye shughuli kuu tatu ambazo ni uchimbaji mkaa, uzalishaji umeme na usambazaji umeme kuingiza kwenye mfumo wa taifa wa TANESCO.

Alisema kukamilika kwa mradi wa uzalishaji umeme kutawezesha kupatikana kwa megawatt 200 zaidi za umeme toka mgodini hapo, ambapo awamu ya kwanza wataingiza TANESCO megawatt 50 ifikapo mwezi Aprili mwaka huu na zinazobaki 150 zitaingizwa Septemba mwakani.

Wajumbe wengine katika kamati hiyo ni pamoja na Maria Kejo, Mugisha Kamugisha, Salome Makange, Dk. Harrison Mwakyembe, Ezekiel Maige, Edward Kihundwa na Katibu wa Kamati, Mathias Kabunduguru.

Jana asubuhi wajumbe wa kamati hiyo waliondoka mkoani hapa kuelekea Mchuchuma katika wilaya ya Ludewa, mkoani Iringa.
 
Back
Top Bottom