FRANCIS DA DON
JF-Expert Member
- Sep 4, 2013
- 40,530
- 46,614
Baada ya kusua sua kwa mda mrefu, kiwanda hiki kilichopo Arusha hivi sasa kina mpango kabambe wa kujiimarisha kimataifa ikiwemo kuanza kuuza bidhaa zake nje ya nchi ikiwemo Kenya, Rwanda, Zanzibar na Burundi..! Hii inatokana na ubora wa hali ya juu sana wa bidhaa zinazozalishwa kiwandani hapo.., pia wanapokea order za kimataifa kwa sasa..!
1.)
Tranformer (MADE IN TANZANIA)
2.)
Switch gear (MADE IN TANZANIA)
Source
==================================
Waziri Kalemani apiga marufuku TANESCO na REA kuagiza transfoma kutoka nje
1.)
2.)
Source
==================================
Waziri wa Nishati Dk Medard kalemani amepiga marufuku shirika la umeme TANESCO na wakala wa umeme vijijini REA kuacha kuagiza transfoma nguzo na vifaa vingine kutoka nje ya nchi ili kudhibiti uingizwaji holela wa vifaa visivyo na ubora ambavyo vinaathiri uchumi na kukandamiza viwanda vya ndani.
Waziri Kalemani ametoa taarifa hiyo alipotembelea kiwanda cha kutengeneza trasfoma tanalec kilichopo jijini Arusha amesema serikali imepata hasara kubwa kwa uingizwaji wa transfoma kutoka nje ambapo hivi karibuni ziliingizwa zaidi ya trasfoma ishirini zilizogundulika kuwa chini ya kiwango.
Mkurugenzi wa ufundi na huduma wakala wa umeme vijijini REA Bengiel Msofe amesema wamepokea agizo la serikali na wataanza kununua vifaa vya ndani kama walivyo agizwa na waziri mwenye dhamana.
Mkurugenzi wa TANALEC Zahri Salehe anasema wamejipanga kuzalisha transfoma elfu kumi ili kumudu soko la ndani na mkuu wa mkoa wa arusha mrisho gambo anasema kama serikali ya mkoa watahakikisha wanasimamia utekelezezaji wa agizo hilo.
Chanzo: ITV
Waziri Kalemani apiga marufuku TANESCO na REA kuagiza transfoma kutoka nje