Kiwanda cha TANALEC kuanza ku-export Transformer Kenya!

Kiwanda cha TANALEC kuanza ku-export Transformer Kenya!

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
40,530
Reaction score
46,614
Baada ya kusua sua kwa mda mrefu, kiwanda hiki kilichopo Arusha hivi sasa kina mpango kabambe wa kujiimarisha kimataifa ikiwemo kuanza kuuza bidhaa zake nje ya nchi ikiwemo Kenya, Rwanda, Zanzibar na Burundi..! Hii inatokana na ubora wa hali ya juu sana wa bidhaa zinazozalishwa kiwandani hapo.., pia wanapokea order za kimataifa kwa sasa..!

1.)
transformer2.jpg
Tranformer (MADE IN TANZANIA)

2.)
switchgear1.jpg
Switch gear (MADE IN TANZANIA)

hmhead.jpg


Source

==================================

Waziri wa Nishati Dk Medard kalemani amepiga marufuku shirika la umeme TANESCO na wakala wa umeme vijijini REA kuacha kuagiza transfoma nguzo na vifaa vingine kutoka nje ya nchi ili kudhibiti uingizwaji holela wa vifaa visivyo na ubora ambavyo vinaathiri uchumi na kukandamiza viwanda vya ndani.

Waziri Kalemani ametoa taarifa hiyo alipotembelea kiwanda cha kutengeneza trasfoma tanalec kilichopo jijini Arusha amesema serikali imepata hasara kubwa kwa uingizwaji wa transfoma kutoka nje ambapo hivi karibuni ziliingizwa zaidi ya trasfoma ishirini zilizogundulika kuwa chini ya kiwango.

Mkurugenzi wa ufundi na huduma wakala wa umeme vijijini REA Bengiel Msofe amesema wamepokea agizo la serikali na wataanza kununua vifaa vya ndani kama walivyo agizwa na waziri mwenye dhamana.

Mkurugenzi wa TANALEC Zahri Salehe anasema wamejipanga kuzalisha transfoma elfu kumi ili kumudu soko la ndani na mkuu wa mkoa wa arusha mrisho gambo anasema kama serikali ya mkoa watahakikisha wanasimamia utekelezezaji wa agizo hilo.

Chanzo: ITV

Waziri Kalemani apiga marufuku TANESCO na REA kuagiza transfoma kutoka nje
 
Safi sana kama wanaachiwa wafanye kazi kwa ufanisi zaidi.
Isije ikapelekwa jirani kama ya matairi uliyoiandika.
 
shida ya hiki kiwanda ni moja tu
tanesco
tanesco wananunua transfomers ghali zaidi na mbuvu zaidi kutoka kwa importers wahindi
why wanafanya hivyo no one knows for sure

haya ndio masuala ya rais ajaye kuanza ku-deal nayo, manunuzi ya tanesco hasa upande wa transformer na switchgears gharama zake zinatia shaka sana, cha ajabu hakuna aliye kuwa anahoji kwa nini walikuwa wanapendelea kununua vitu hivyo kutoka nje wakati arusha wanahunda transformers, wako radhi kiwanda kife.
 
Siyo siri bidhaa za Tanalec ni bora sijui kuna nini kinachokwamisha maendeleo yake,
Kuna majiko yao ya umeme mazuri sana.
 
Ni hatua nzuri sana bado tukaze buti tuendelee juzalisha na bidhaa nyingine
 
Nachokifahamu ni kuwa owners wa hiki kiwanda kwa sasa ni wa Kenya, niko tayari kusahihishwa.
 
apige marufuku kitu ambacho na yeye atakuwa ananufaika?
tukitaka kufanikiwa nchi hii ni kuiondoa ccm madarakani, vinginevyo hakuna chochote.
hichokiwanda watakihujumu kife.

kama nguzo walikuwa wanazisafirisha kutoka mufindi mpaka kenya aafu wanakuja kutuambia zimetoka SA na kuingilia bandari ya mombasa unadhani watanunua hizo transformer?
 
Tanelec ni noma, tanesco waachane na vya nje wabaki na ndani...
 
Baada ya kusua sua kwa mda mrefu, kiwanda hiki kilichopo Arusha hivi sasa kina mpango kabambe wa kujiimarisha kimataifa ikiwemo kuanza kuuza bidhaa zake nje ya nchi ikiwemo Kenya, Rwanda, Zanzibar na Burundi..! Hii inatokana na ubora wa hali ya juu sana wa bidhaa zinazozalishwa kiwandani hapo.., pia wanapokea order za kimataifa kwa sasa..!

1.)
transformer2.jpg
Tranformer (MADE IN TANZANIA)

2.)
switchgear1.jpg
Switch gear (MADE IN TANZANIA)

hmhead.jpg


Source

Vipi kuhusu general tyre?
 
Baada ya kusua sua kwa mda mrefu, kiwanda hiki kilichopo Arusha hivi sasa kina mpango kabambe wa kujiimarisha kimataifa ikiwemo kuanza kuuza bidhaa zake nje ya nchi ikiwemo Kenya, Rwanda, Zanzibar na Burundi..! Hii inatokana na ubora wa hali ya juu sana wa bidhaa zinazozalishwa kiwandani hapo.., pia wanapokea order za kimataifa kwa sasa..!


Source

Zanzibar ni nchi ya nje kumbe.???
 
Shida ya hiki kiwanda ni moja tu
TANESCO
Tanesco wananunua transfomers ghali zaidi na mbuvu zaidi kutoka kwa importers wahindi
why wanafanya hivyo no one knows for sure
hata mabehewa mabovu tunauziwa tu na wahindi. transformer nzuri zipo hapa tanzania ila mpaka tununue india kwa bei mbaya. kweli rushwa inapofusha.
 
Safi sana kama wanaachiwa wafanye kazi kwa ufanisi zaidi.
Isije ikapelekwa jirani kama ya matairi uliyoiandika.

Kwa taarifa yako tu,TANELEC ni mali ya jirani zetu Wakenya, Tanesco/ABB kiliwashinda, ndipo kikabinafsishwa kwa Wakenya. Cc: Ngongo.

Vv
 
Mamaweeeeeeeee kama na hiki ni cha wakenya inatia aibu.....naishi kwenye nchi isiyomiliki hata kiwanda cha madodoki uwwwiiiiii
 
Back
Top Bottom