Haya ni masahibu wanayokutana nayo vijana wengi wa Tz.
Mifumo ya uchumi na maendeleo ya Nchi hii siyo rafiki sana kwa shughuli za uchumi na maendeleo. Kwa mfano, kijana analima na kupata mtaji wa biashara (e.g. milioni mbili), anaanzisha biashara ya duka, TRA wanaingia na kumkadiria kodi ya laki nne wakati hiyo ndiyo faida ya biashara yake, achilia mbali kodi ya kibanda, ushuru wa soko, nauli ya bidhaa, luku, simu, n.k. Ni majanga. Ndiyo maana vijana wengi wanakimbilia kuajiriwa japo kwa salary ya 250,000/= kwa mwezi. Watafanyaje sasa.