Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,817
- 11,993
Katika ziara hiyo Haniu ameagiza Mkandarasi anayetekeleza mradi huu kufanya kazi kwa bidii ili kusaidia upatikanaji wa nishati hiyo kwa wakati.
Aidha, ameagiza kuendelea kuajiri vijana wanaopatikana katika mazingira yanayozunguka mradi huu ili kupanua wigo wa ajira kwa Watanzania.
Kituo hiki kilichopo ndani ya Msitu wa Ziwa Ngosi kinatarajia kuzalisha kiasi cha Megawati 70 mara kitakapokamilika.
Mkuu wa Wilaya ameeleza kuwa mradi huu unaenda kuondoa adha ya ukataji miti ovyo kwa ajili ya upatikanaji wa nishati hasa katika viwanda vya ukaushaji wa mali mbichi.