Kituo cha Polisi Chachomwa Kyela

Nsaji Mpoki

JF-Expert Member
Nov 5, 2007
396
65
Taarifa nilizopata kutoka Kyela zinaeleza kuwa vurugu kubwa zimetokea jana na kusababisha kifo cha mtu mmoja aliyepigwa risasi na POLISI. Hasara kubwa kwa mali za Umma na Watu binafsi ikiwemo mahakama ya mwanzo na kituo cha POLISI kimechomwa moto na kuteketea.Taarifa kamili ya chanzo cha vurugu hizo nitawaletea baadaye.
 
Taarifa nilizopata kutoka Kyela zinaeleza kuwa vurugu kubwa zimetokea jana na kusababisha kifo cha mtu mmoja aliyepigwa risasi na POLISI. Hasara kubwa kwa mali za Umma na Watu binafsi ikiwemo mahakama ya mwanzo na kituo cha POLISI kimechomwa moto na kuteketea.Taarifa kamili ya chanzo cha vurugu hizo nitawaletea baadaye.

tik...tik...tik...
 
Mimi nashangaa IGP Mwema na Waziri Masha bado hawajaona kasoro iliyopo ktk jeshi la polisi. Katika kipindi kifupi wameshauwa wananchi wengi wasio na hatia. Kwa mfano Ubungo, Dar (dereva taxi), Tandika (kijana mwanafunzi wa UDSM mtarajiwa), Arusha (vijana wawili), Tunduma (mfanyabiashara), ongeza na ile ya akina Zombe. Hii inaonyesha kuwa nidhamu ya polisi imepungua mno. Hali ikiachwa hivi hivi amani itapotea.
 
Mafisadi wanatesa, Mapolisi wanatesa.

Nani wa kumkamata mwenzake hapo?

tik......tak......tik........tak, Time bo?# in the making
 
Nangoja tangazo la kuunda Mkoa Maalimu wa kipolisi sasa huko Kyela maana things are really getting hotter
 
Hakuna kitu chochote kinachohalalisha uvunjajji wa haki na mashambulizi dhidi ya mali ya umma. Watu waliofanya kitendo hiki ni wahalifu kama wale waliovamia shamba la Kimaro. Mahali pao ni jela tu. Vinginevyo tutaka tukae nao kiti kimoja halafu tujadiliane ili tueleze ilikuwaje wakashambulia sehemu hizo nyeti za serikali. Hakuna udhuru katika uhalifu.
 
i just do suppose that we shall be in a good position to give out our comments on that issue of kyela immediately after getting the truth and bold information surrounding the whole saga,
i submitt.
 
Msiwe na hofu wacheni serikali ihamishe polisi wote kwenda Pemba maana huko Pemba ndio kunako tokea matukio ya uvunjaji sheria ,na bado CCM itatafuta sehemu ya kuziba lakini wakiziba Pemba basi kutatoboka Tanganyika.
 
Mahakama yachomwa, ofisi ya DC yaharibiwa
* Ni baada ya polisi kudaiwa kuua raia
  • Risasi, mabomu ya machozi vyarindima
  • Biashara, barabara zafungwa kwa muda

Na Solomon Mwansele, Mbeya

VURUGU zilitawala jana eneo lote la Kyela mjini, mkoani Mbeya, kutokana na kifo cha mkazi wa Mbugani, Lucas Mwaipopo, aliyedaiwa kuuawa kwa kipigo kutoka polisi watatu.

Kwa mujibu wa habari kutoka eneo la tukio, Mwaipopo alikamatwa na polisi waliokuwa doria saa mbili usiku, eneo la Mashineni, akiwa na mwenzake ambaye aliachiwa njiani kabla ya kufikishwa kituo cha polisi kwa madai kwamba, alitoa kitu kidogo.

Kwa mujibu wa chanzo cha habari, baada ya Mwaipopo kufikishwa kituoni alipigwa na kupoteza fahamu, hivyo kupelekwa hospitali ya wilaya ambako alifariki dunia akipatiwa matibabu.

Mamia ya wananchi waliandamana jana asubuhi kuelekea kituo cha polisi kupata ufafanuzi juu ya tukio hilo, ambapo wakiwa njiani waliuona msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile.

Wananchi hao waliamua kuufuata msafara huo ili kwenda kuwasilisha malalamiko yao, ambapo polisi waliwafukuza, hivyo kuamua kuvamia kituo cha polisi wakiwa na mawe mikononi.

Polisi walilazimika kutumia risasi za moto na mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi hao, ambapo watu watatu walipigwa risasi, miongoni mwao akiwamo Jacob Anthony, aliyepigwa risasi tumboni na kutokea kwenye kalio la upande wa kulia.

Anthony alipelekwa kwa matibabu kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, ambapo wengine waliojeruhiwa kwa risasi ni Daud Kibona, aliyepigwa mkono wa kulia na Ramadhan Hassan, ambaye risasi imeingia na kutokea upande mwingine wa bega la kulia.

Askari D.9713 Koplo Mbanga na E. 7787 Koplo Robert walijeruhiwa kwa kupigwa na mawe na wananchi na walipelekwa hospitali ya wilaya ya Kyela kwa matibabu.

Vurugu hizo pia zilisababisha ajali, ambapo mwanamke ambaye hajatambuliwa alishindwa kulimudu gari alilokuwa akiendesha na kujikuta akigonga mti kutokana na kuchanganyikiwa. Amelazwa katika hospitali ya wilaya kwa matibabu.

Baada ya wananchi hao kuona wanazidiwa nguvu na polisi waliondoka na kwenda Mahakama ya Mwanzo ya Kyela, ambako waliichoma moto na pia kwenda kufanya uharibifu kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ya Kyela.

Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Harrison Makinda, akizungumzia tukio hilo, alisema ameshangazwa na kitendo cha wananchi kuvamia mahakama na kuichoma, kwani haihusiani na kupigwa na kuuawa kwa Mwaipopo.

Makinda alisema walipofika kazini asubuhi kabla ya tukio hilo, walilazimika kuahirisha kesi zote baada ya nyumba iliyo jirani na mahakama kuwa na msiba, hivyo kuwafanya kushindwa kufanya kazi.
 
Hakuna kitu chochote kinachohalalisha uvunjajji wa haki na mashambulizi dhidi ya mali ya umma. Watu waliofanya kitendo hiki ni wahalifu kama wale waliovamia shamba la Kimaro. Mahali pao ni jela tu. Vinginevyo tutaka tukae nao kiti kimoja halafu tujadiliane ili tueleze ilikuwaje wakashambulia sehemu hizo nyeti za serikali. Hakuna udhuru katika uhalifu.

That is what i thought. Kama sheria ikivunjwa na wanaotakiwa kusimamia sheria hizo wanachekelea. Kama wanaosimamia sheria wanavunja sheria unategemea, nani ataekeleze justice.

Nadharia tunazosoma kwenye vitabu kuhusu kuhusu sheria kuna wakati hazitekelezeki hapa Tanzania. Zinaweza kutekelezeka kwenye jamii ambayo watekelezaji wa sheria na walinzi wa sheria wanaheshimu kazi zao.
 
jamani huko Mbeya kuna nini? mara wapige Mawe msafara wa Rais,wavamie vituo vya polisi Tunduma,sasa Kyela kuna
 
Nasikia kyela ni mfanyabiashara kauwawa kama ile ya Tunduma so wananchi wakaandamana mpaka kwa RC ambaye alikuwa kyela wakati huo,mkuu akala kona.
So wananchi baada ya kuona ivyo wakachukua sheria mkononi kuanzisha fujo mpka zikaja defender 3 za FFU.
No way hao watu waliouwawa mahari tofauti tofauti ikawa ni bahati mbaya.
Mwema needs to work on that kuna ukweli wake.
 
Hakuna kitu chochote kinachohalalisha uvunjajji wa haki na mashambulizi dhidi ya mali ya umma. Watu waliofanya kitendo hiki ni wahalifu kama wale waliovamia shamba la Kimaro. Mahali pao ni jela tu. Vinginevyo tutaka tukae nao kiti kimoja halafu tujadiliane ili tueleze ilikuwaje wakashambulia sehemu hizo nyeti za serikali. Hakuna udhuru katika uhalifu.
Usilazimishe maji kujaa kwenye chungu!!!
Siyo vyema kabisa kuchukua hatua za kuchoma moto mali ya umma! na siyo vyema kuhamasisha umma kuchukua sheria mkononi maana kuna hatua mwanadamu anapata sitofahamu ya maamuzi.Tulizeni hasira vijana na poleni kwa yote.
Serkali jichunguzeni kasoro yenu.
Joune,
Ndikupasya Buno malafyale anganile Kangi Ambokile.
Ndaga.
 
Hakuna kitu chochote kinachohalalisha uvunjajji wa haki na mashambulizi dhidi ya mali ya umma. Watu waliofanya kitendo hiki ni wahalifu kama wale waliovamia shamba la Kimaro. Mahali pao ni jela tu. Vinginevyo tutaka tukae nao kiti kimoja halafu tujadiliane ili tueleze ilikuwaje wakashambulia sehemu hizo nyeti za serikali. Hakuna udhuru katika uhalifu.


Heshima kwako mzee;

Nakubaliana kabisa nawe katika utii sheria na haki za binadamu, lakini wakati huo huo tujiulize katika mazingira yepi, haya ya Tanzania ya leo! Hapana tuende mbali zaidi na kuachana na nadharia za vitabuni, viongozi ndio chimbuko la yote haya, hawawajali wananchi wao, wanawabeza na kuwadharau.

Wananchi wanakujia kukulilia kuhusu wanavyouawa na askari, wewe unawatimulia vumbi, kweli ni haki, inahitaji uvumilivu wa Yesu tu!

RC alikuwa wilayani, mapigano yameanza mara baada ya yeye akiongozana na kamati yote ya ulinzi na usalama kuwakimbia wananchi waliomfuata kuelezea masikitiko yao juu ya kuawa kwa kijana wao kwenye kituop cha polisi, waliwadharau wakawatimulia vumbi na kukimbilia pilau wanazoandaliwa vijijini, ulitaka wafanye nini.

Watanzania sasa wamechoka ni wakati wa viongozi kujihoji na si kuwatafutia mikakati wananchi ya jinsi ya kuwanyamazisha, hawatanyamaza, wamefikishwa mahali ambapo uhai kwao hauna faida tena, wanaweza kufanya lolote.
 
Mahakama yachomwa, ofisi ya DC yaharibiwa
* Ni baada ya polisi kudaiwa kuua raia
  • Risasi, mabomu ya machozi vyarindima
  • Biashara, barabara zafungwa kwa muda

Na Solomon Mwansele, Mbeya

...... Mamia ya wananchi waliandamana jana asubuhi kuelekea kituo cha polisi kupata ufafanuzi juu ya tukio hilo, ambapo wakiwa njiani waliuona msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile.

Wananchi hao waliamua kuufuata msafara huo ili kwenda kuwasilisha malalamiko yao, ambapo polisi waliwafukuza, hivyo kuamua kuvamia kituo cha polisi wakiwa na mawe mikononi.

....

nae mwakipesile bwana kwanin hakuwasikiliza?

1. au alikuwa na haraka sana?
2. au alikuwa anaogopa angeletewa fujo?

sina uhakika na chochote katka hayo au mengine

lakin mwakipesile, mwanasiasa, mkuu wa mkoa husika na ambaye aliwah kuwa mbunge wa sehem hiyo hiyo naamin alikuwa na cha kufanya ambacho kingeepusha rabsha na baadae mauaji yale
 
It is very terrible, yaliotokea kyela Mbeya yanasikitisha na ni mfano mbaya. it said that RC scape them why what would them did? they dicided to go on, step to step for 4 hours if ffu delay for 12 hours ingekuwa INTRAGEDY.
SO MWALIMU J.K. NYERERE ALISEMA
AMANI NI AMANA NA TUNU KUBWA
ISIOKUWA NA BEI.
NIMENUKUU WAKUU JF.
MBONENYAI.
 
Back
Top Bottom