BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,377
- 8,121
Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani imeunda kamati maalum kuchunguza ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Butiama mkoani Mara unaokadiriwa kutumia Sh802 milioni hadi kukamilika kwake. Kamati hiyo inaundwa na wataalam wa masuala ya manunuzi, ukadiriaji wa majengo, wahandisi ujenzi na wakaguzi wa fedha kutoka idara na taasisi mbalimba za umma.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza leo Jumatatu Novemba 27, 2023, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Jumanne Sagini amesema uamuzi wa kuunda kamati hiyo inayojumuisha wataalam kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa ndani umetokana mapokeo ya wananchi juu ya gharama za ujenzi wa kituo hicho kuonekana kubwa kulinganisha na majengo yanayojengwa.
Amesema pamoja na kujiridhisha na matumizi sahihi ya fedha za umma, taarifa ya uchunguzi huo pia itaiwezesha Serikali kufanya maamuzi ikiwemo kuchukua hatua stahiki za kisheria na kinidhamu iwapo patabainika ukiukwaji wa sheria, kanuni na taratibu za ujenzi na matumizi ya fedha za umma.
Uchunguzi huo umetokana na kelele zilizopigwa na umma baada ya taarifa za gharama za ujenzi wa kituo hicho kusambaa kupita mitandao ya kijamii.
Pia soma
Kituo cha Polisi Wilaya ya Butiama chajengwa kwa Tsh. Milioni 802, kukamilika Desemba 2023
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa Jimbo la Butiama, Jumanne Sagini ameagiza kukamilika kwa wakati Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Polisi Daraja B cha Wilaya ya Butiama Mkoani Mara, ifikapo mwezi Disemba 2023 kama ilivyoelekezwa. Maagizo hayo ameyatoa leo Novemba 18, 2023 wakati...
www.jamiiforums.com
Mkuu wa Mkoa wa Mara atembelea Mradi wa Kituo cha Polisi Butiama unaojengwa kwa Tsh. Milioni 802
Nimesoma kupitia mitandao ya kijamii kuhusu mjadala wa kukamilika kwa kituo cha Polisi Butiama kwa thamani ya sh mil 802. Kwanza nawapongeza waandishi kwa kuibua hoja na mjadala, ingawa hoja na mjadala haukusikia wala kutaka kufahamu kutoka upande wa serikali. Kwa kuwa serikali yetu ni...
www.jamiiforums.com