Kituo cha ITV, kwa hili nimewashusha

Kituo cha ITV, kwa hili nimewashusha

Grena

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2016
Posts
656
Reaction score
1,557
Habari zenu wakuu,

Hii Chanel ya ITV inakuwaga na utaratibu wa kurusha matangazo kutoka katika vyombo vya habari vya kimataifa Kama Aljazeera na DW.

Na katika habari kuu za leeo za Aljazeera mojawapo ilikuwa Kuhusu Tanzania na Corona. Cha kushangaza habari zingine zikarushwa lakini ilipofika Ile habari ya Tanzania wakakatisha habari ya Aljazeera na kuweka matangazo ya Isidingo halafu wakarudisha Tena Aljazeera baada ya Ile habari ya Tanzania kupita.

Kweli ITV mmefikia kiwango cha kuwa waoga namna hii kukataa raia wasione vyombo vya nje vinavyoizungumzia Tanzania?

Joyce Mhavile, Mkurugenzi wa ITV radio one angalia hili mama. Mnapoteza uaminifu na mvuto wenu kwa Watanzania.
 
Joisi ana familia mkuu, ana watoto na anasomesha. Asipofanya hivyo anajua atapambana na ada za watoto bila mafanikio, kukaa bila kazi kunauma mkuu! Kuishi ni kuchanga karata tu, ukizubaa na kujifanya gangwe utavuna magalasa. Msamehe dada wa watu tu na muhurumie alee watoto wake.
 
Mnamo saa 5 asubuhi ITV ilijiunga na Aljazeera English. Heading moja wapo ya news ilihusu hali ya Corona Tanzania.

Ilipofikia hiyo taarifa ITV WAKAWEKA MSULULU WA MATANGAZO na hivyo kuminya hiyo taarifa. Nilipokwenda jaazira moja kwa moja waliongelea tunavyoipuuza covid kwa kuonyesha yaliyotokea Dar es Salaam wakati wa Eid.

Zitto akazungumza yake. Wakazungumzia ya ubalozi wa Marekani. Wakaongelea pia ukosefu wa takwimu. Nikarudi ITV wakamaliza matangazo yao wakajiunga na Al Jazeera kwa topic iliyofuata.

HIVI NDIO VYOMBO VYETU VYA HABARI TUNAVYO VIAMINI. Au ndio uzalendo huo?
 
Watu Wa kanda ya nyonyo hawatakiwi kupewa nchi, wana ushamba mwingi wizi ubabe, utendaji zero, exposures zero.
Mnatakiwa mjifunze.
 
Mmhhh sasa kama corona haitakiwi kusikiwa mbona kuna matangazo mengi tu ya corona kwenye redio yanaendelea
 
That is what a dictatorship can do. Watu wanakuwa waoga. Wanaweza kukimbia hata kivuli chao. That's what is happening in Tanzania now. Siyo tatizo la ITV. Ni tatizo la udikteta. Those are just manifestations of a dictatorship.
Mnamo saa 5 asubuhi ITV ilijiunga na Aljazeera English. Heading moja wapo ya news ilihusu hali ya Corona Tanzania. Ilipofikia hiyo taarifa ITV WAKAWEKA MSULULU WA MATANGAZO na hivyo kuminya hiyo taarifa.

Nilipokwenda jaazira moja kwa moja waliongelea tunavyoipuuza covid kwa kuonyesha yaliyotokea dar es salaam wakati wa Eid. Zitto akazungumza yake. Wakazungimzia ya ubalozi wa marekani.

Wakaongelea pia ukosefu wa takwimu. Nikarudi itv wakamaliza matangazo yao wakajiunga na al jazeera kwa topic iliyofuata. HIVI NDIO VYOMBO VYETU VYA HABARI TUNAVYO VIAMINI. Au ndio uzalendo huo?
 
Habari zenu wakuu,

Hii Chanel ya ITV inakuwaga na utaratibu wa kurusha matangazo kutoka katika vyombo vya habari vya kimataifa Kama Aljazeera na DW.

Na katika habari kuu za leeo za Aljazeera mojawapo ilikuwa Kuhusu Tanzania na Corona. Cha kushangaza habari zingine zikarushwa lakini ilipofika Ile habari ya Tanzania wakakatisha habari ya Aljazeera na kuweka matangazo ya Isidingo halafu wakarudisha Tena Aljazeera baada ya Ile habari ya Tanzania kupita.

Kweli ITV mmefikia kiwango cha kuwa waoga namna hii kukataa raia wasione vyombo vya nje vinavyoizungumzia Tanzania?

Joyce Mhavile, Mkurugenzi wa ITV radio one angalia hili mama. Mnapoteza uaminifu na mvuto wenu kwa Watanzania.
Kwa hiyo wakireport Jambo baya la Tanzania kwako nifuraha?
 
Back
Top Bottom