Hawana shida na Nape kwa sababu anachosema hakimtishi mtu yeyote hata mtoto wa chekechea anajua huu ni uzushi , ila kinachosemwa na Mbowe kina madhara makubwa kwa mafisadi na policcm ambao wanajua hivi karibuni kutapambazuka na uhuru wa kweli utapatikana na wao hawatakuwa na mahali pa kuficha nyuso zao. Wakati ni ukuta. Polisi wa TZ wamekuwa waongo hadi wanakera, bomu la kanisani walisema limerushwa na Ambrose mwendesha bodaboda wakawaachia wahusika, Daudi Mwangosi kapigwa na kitu kizito, Dr Ulimboka kateswa na Mkenya, Mhariri Kibanda kateswa na Lwakatare, bomu lililorushwa kwenye mkutano wa CDM lilirushwa na wanaCDM wenyewe, hivi hii ni akili kweli. Halafu eti wapo kwa ajili ya kulinda usalama wa raia na mali zao. Hawa wapo kwa ajili ya maslahi ya kikundi kidogo cha waTZ wanaowamiliki.