Kituko cha mwaka 90

Kituko cha mwaka 90

prospa

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2012
Posts
554
Reaction score
157
Nakumbuka enzi hizo nilikuwa sijawahi kuingia Hotelini wala mgahawani,

sasa one day rafiki yangu akanipa offer ile kufika kwenye mgahawa wa kisasa kimtindo si nikaanza kupiga hodiii, hodiiii wacha rafiki yangu aangue kichekoooooo, wewe ulifanya yepi enzi za ushamba
 
Mbona mwenzio siku yangu ya kwanza kusafiri na ndege nilianza kusalimia wasafiri wote ndani ya ndege,unacheza na ushamba nini..
 
mimi nilienda kwa rafiki angu nikakaribishwa chakula kilikuwa kwenye hotipoti, nikala chote, kumbe kilikuwa cha watu wote, niliona aibu je?

Nimecheka sana. Lazima wewe utakuwa unatokea Mwanza au Shinyanga
 
Hii nilikuwa mdogo sana (mtoto) ila nakumbuka. Ni pale asubuhi njaa ilikuwa inauma na moto upo tayari umewashwa majiko ya kuni.
Nilichukua kikombe cha plastic nikaweka maharage ya jana halafu nikabandika jikoni. Nasubiria yapate moto ili nile nikakuta kikombe kimeteketea ikabidi nimuite mama. Mama alivyokuja alishindwa hata kunipiga alibaki kucheka tu na kikombe kikawa ndio kimeteketea hivyo.
 
Mara ya kwanza naingia kwa hotel na kukutana na mlango wa sensor, kabla sijaugusa ukafunguka weeeee....
 
mimi nilienda kwa rafiki angu nikakaribishwa chakula kilikuwa kwenye hotipoti, nikala chote, kumbe kilikuwa cha watu wote, niliona aibu je?

Nimecheka saaana aisee,thanks for making my day mkuu
 
Siku ya kwanza kupanda lift ya gorofa niliona kama haiendi
 
Mi kwangu huu si ushamba aisee, naona hii inaweza kumtokea karibu kila mtu!

dah.... kuna hivi vioo ambavyo vinachukua nafasi ya milango ya mbao, vile vioo vigumuuuu!

Basi bwana, lile likioo lilikuwa limesafishwa vizuri haswaaa!! linang'aa effectively!

Kuna wakati ilikuwa ukiangalia kwenye kioo pale unaona kama vile hamna kioo! kumbe wapi!...

Haya! mi na ugeni wangu, nikakurupushwa kutoka recreation centre na kuambiwa kuwa muda wa kazi ushafika!! unacheza pool mpaka saa hizi?

kusikia hivyo, wacha nikimbie kuokoa kibarua! lahaulaaaa! mtoto wa watu nikaruka na kuparamia kioo kile nikidhani ni empty space ambayo naweza kupita!!!!!

dah! mpaka leo nikikumbuka ile hali, inabidi nicheke, kiukweli niliumia sana paji la uso pamoja na baadhi ya viungo vya mwili!

enzi hizo ndo kwaanza naanza na kukutana na automatic doors! kabla hujafika tu, usha-sense na kufunguka wenyewe! hm! ushamba mzigo..!

ni hayo tu!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom