Kitu pekee nilichokiona kwa Wasemaji wa sasa Ahmed Ally Simba SC na Ally Kamwe Yanga SC ni hiki Kifuatacho...

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Apr 2, 2015
8,011
16,748
Wote wana Corporate Personalities za Asili hasa na siyo ile ya Kulazimisha, Wasomi wazuri wa Mass Communication na wana Mvuto wa Kiushawishi hasa kwa Biashara na Mashabiki wa Vilabu vyao husika.

Siyo unakuwa na Msemaji muda wote ukiwa nae Jirani unasikia tu harufu ya Sigara, Bangi, Pombe na harufu ya Kujamba jamba hovyo huku akiwanyeshea tu Mvua Waandishi wa Habari akiwa anaongea nanyi katika Press Conference.

Heko kwa Azam Media Company kwa Kuwapika vyema Vijana Wenu hawa Wawili ( ambao ni Marafiki wakubwa sana ) Ahmed Ally Msemaji wa Simba SC na Ally Kamwe Msemaji wa Yanga SC.

Nina matumaini makubwa nao mno.
 
Back
Top Bottom