Kitu gani kinakwamisha ukuaji wa kilimo cha umwagiliaji Tanzania?

Red Giant

JF-Expert Member
Mar 9, 2012
15,658
20,889
Tanzania imebarikiwa kila kitu kinachofaa kwa kilimo cha umwagiliaji. Tuna ardhi ya kutosha kabisa. Nchi yetu ina eneo kubwa la kilomita za mraba 900,000+ . Wanasema tuna eneo la hekari milioni kama 30 zinazofaa kwa umwagiliaji lakini eneo linalomwagiliwa halifiki hata 1m.

Maji, Tanzania ni moja ya nchi yenye maji kwa wingi duniani(surface fresh water). Ziwa Tanganyika lina kama asilimia 16 ya surface fresh water yote duniani. Tanzania inamiliki 45% ya ziwa hilo. Ziwa nyasa lina karibu asilimia 6 ya maji yote safi yaliyopo juu duniani. Haya ni maji mengi sana. Hapo bado hatujazungumzia maziwa yenye maji machache kama Victoria, Rukwa na mito mingi ambayo huishia baharini. Pengine kuna changamoto kutoa maji kwenye maziwa ya bonde la ufa lakini ni ishu inayowezekana.

Kwanini basi hili suala haliendelezwi Tanzania? Ni ajira ngapi zinaweza tengenezwa ukijenga irrigation scheme ya ekari 1m?

Siku moja nilitembelea irrigation scheme ya Kapunga mbeya, ni kubwa nilishangaa sana na ile ni Hekta sijui ni ekari kama 7,000 hivi. Wakati wa kilimo watu wanajaa vibaya mno eneo lile, ajira za kutosha. Nasikia hii ilijengwa na wajapan, serikali yetu hii sidhani kama imewahi kujenga Irrigation scheme.

Nyie wadau mnasemaje, kwanini nchi kilimo cha umwagiliaji hakiendelezwi na hali kinaonyesha kuwa ni kitu chenye faida sana? Au ndiyo ile in abundance of water the fool is thirsty!!?
 
Palikuwa na taasisi moja inaitwa TIP kwa kifupi. Ilikuwa na makao makuu Moshi Mjini. Yenyewe ililenga wakulima wenye kufanya kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia mbinu za asili. Taasisi hii ilipata mafanikio makubwa. Nenda popote TIP ilipokuwa ikifanya miradi yake, utakuta inazungumzwa vema.

Namna TIP ilikuwa ikisaidia wakulima kwa methodolojia yake mahususi, ilibadilisha kwa mafanikio makubwa maisha ya wananchi.

Nadhani Wizara yenye dhamana ya Kilimo na Ushirika zingeweza kuitumia TIP kwa kukasimisha sehemu za bajeti zao ili kupata matokeo makubwa ya ukweli kwenye eneo hilo la kilimo cha umwagiliaji.

Natamka: Wakati fulani niikuwa mjumbe wa bodi ya taasisi ya TIP.
 
Palikuwa na taasisi moja inaitwa TIP kwa kifupi. Ilikuwa na makao makuu Moshi Mjini. Yenyewe ililenga wakulima wenye kufanya kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia mbinu za asili. Taasisi hii ilipata mafanikio makubwa. Nenda popote TIP ilipokuwa ikifanya miradi yake, utakuta inazungumzwa vema.

Namna TIP ilikuwa ikisaidia wakulima kwa methodolojia yake mahususi, ilibadilisha kwa mafanikio makubwa maisha ya wananchi.

Nadhani Wizara yenye dhamana ya Kilimo na Ushirika zingeweza kuitumia TIP kwa kukasimisha sehemu za bajeti zao ili kupata matokeo makubwa ya ukweli kwenye eneo hilo la kilimo cha umwagiliaji.

Natamka: Wakati fulani niikuwa mjumbe wa bodi ya taasisi ya TIP.
Mkuu kumbe una uzoefu na hii sekta. Unaweza kutujuza zaidi. Hasa faida zilizotokana na hiyo taasisi na nini kifanyike kuinua kilimo cha umwagiliaji.
 
Mkuu kumbe unauzoefu na hii sekta. Unaweza kutujuza zaidi. Hasa faida zilizotokana na hiyo taasisi na nini kifanyike kuinua kilimo cha umwagiliaji.
Faida yake kubwa ni skeli ya kilimo.

Pale Chang'ombe karibu na Uwanja wa Taifa, palikuwa na wakulima wa mchicha almaaruf "Waluguru" waliokuwa wakilima matuta ya mchicha na kuyamwagilia. Je, wakulima wa sampuli hii wanaguswa na mijadala ya kilimo cha umwagiliaji?
 
Faida yake kubwa ni skeli ya kilimo.

Pale Chang'ombe karibu na Uwanja wa Taifa, palikuwa na wakulima wa mchicha almaaruf "Waluguru" waliokuwa wakilima matuta ya mchicha na kuyamwagilia. Je, wakulima wa sampuli hii wanaguswa na mijadala ya kilimo cha umwagiliaji?
Red Giant

Hakuna sababu za kushindwa kilimo cha umwagiliaji.

Tunasababu za kukosa watu wenye fira , wadadisi na wanaoweza kuhoji vitu.

Kama ulisikia Bungeni hivi karibuni tatizo kubwa linalozungumzwa ni Mbegu za kiume !

Huyu anayejadili nguvu za chumbani ana muda gani wa kufikiri kuhusu irrigation.

Hapo ndipo tatizo lilipo!
 
Faida yake kubwa ni skeli ya kilimo.

Pale Chang'ombe karibu na Uwanja wa Taifa, palikuwa na wakulima wa mchicha almaaruf "Waluguru" waliokuwa wakilima matuta ya mchicha na kuyamwagilia. Je, wakulima wa sampuli hii wanaguswa na mijadala ya kilimo cha umwagiliaji?
Rais amesema kwenye hotuba yake kuwa. Mpaka kufikia 2025 tuwe na ekari milioni 1.2 chini ya umwagiliaji . Kutoka ekari laki tano.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom