1PETRO 18-19. 18 Maana mnafahamu kwamba mlikombolewa kutokana na maisha duni yasiyofaa ambayo mlirithi kutoka kwa baba zenu. Hamkukombolewa kwa kutumia vitu viharibikavyo kama fedha na dhahabu, 19 bali mlikombolewa kwa damu ya thamani ya Kristo, Mwana-Kondoo asiye na dosari wala doa. 20 Yeye alichaguliwa kabla ya dunia kuumbwa lakini akadhihirishwa katika siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
kitu chenye thamani kuliko vitu vyooote, ni DAMU YA YESU KRISTO. tukisoma Isaya 53 utaona kuwa ulikuwa mpango wa Mungu tangu zamani sana kutengeneza njia ya ukombozi wa mwanadamu. Damu ya Yesu Kristo in thamani kuliko vitu vyote kwasababu zifuatazo.
- ni Damu isiyo na hatia, Yesu hakuwahi kutenda dhambi hata moja hivyo ni Damu safi.
- ni Damu ya Mungu mwenyewe, in athamani kuliko gemstones, gold, silver, etc
- ni Damu ya mtu mwenye haki aliyeamua kuimwaga kwa ajili ya wengine (sisi sote)
- ni Damu pekee yenye uwezo kumsambaratisha Shetani na utawala wake wote. Ushindi wa Yesu juu ya mauti na kuzimu una maanisha kwamba Shetani asikiapo Damu ya Yesu Kristo anakumbuka jinsi alivyosambaratishwa na kuwekwa chini kabisa mbele za Yesu aliposhuka kuzimu kumfunga na nguvu zake zote.
- ni Damu pekee yenye uwezo wa kurestore vitu vyako vilivyoharibiwa au kuibiwa na shetani, wachawi na uchafu wote wa kuzimu.
- ni Damu pekee inayonena mema juu ya maisha ya mtu anayemwamini Yesu Kristo na kuikiri. Tunamkiri Yesu Kristo na tunaomba kwa Jina lake, lakini hayo yote msingi wake upo kwenye kufa (kumwaga damu) na kufufuka kwa Yesu. kitendo cha Yesu kufa na kufufuka kilimshinda shetani na mamlaka zote zipo mikononi mwa Yesu Kristo. shetani akikuonea tu ukimkumbusha Damu ya Yesu Kristo na kumwamuru kwa Jina la Yesu Kristo aliyemwaga Damu yake shetani aondoke, anatii mara moja.
- Damu ya Yesu Kristo itajwapo na mwamini, inasababisha malaika wa Mungu kusogea na kufanya mema juu ya maisha yako.
- kuna mengi sana yatajaa.
kwasababu hizo, ni kitu gani kilicho cha thamani kuliko hicho? mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya ndugu zake? maisha ni kitu chenye thamani kuliko vyote kwa wanadamu wengi lakini YESU KRISTO alinunua uzima wa milele (upatanisho) kwa njia yake, kwa njia ya kuutoa uhai wake. hakuna kitu chenye thamani sana kama kitu ambacho mtu amekitolea uhai wake, na idadi ya watu unaosacrifice uhai wako kwa ajili yao pia ina matter, Yesu Kristo ali sacrifice uhai wake kwaajili ya wanadamu woote duniani...akatununua sote. ni kwa fedha kiasi gani tungelipa deni letu la dhami? deni la dhambi za wanadamu wote duniani? that cost is unimaginable. ni gharama kubwa isiyofikirika, ndio Yesu alitoa kupitia kumwaga Damu yake Msalabani, na hiyo gharama kubwa ndio inamfanya Shetani akimbie asikiapo Damu ya Yesu Kristo. kwa wale wenye kusikia kuanzia leo, uombapo iite Damu ya Yesu katika maisha yako na katika maeneo mbalimbali katika maisha yako ukimalizia kwa Jina la Yesu Kristo aliyemwaga Damu yake Msalabani kwa ajili yangu....hakika ukombozi utapatikana kwako. hicho ndicho kitu cha thamani kuliko vyote ambacho wengi hawakithamini ila kuna siku watakitafuta lakini muda utakuwa umeisha, itabaki hukumu ya milele na milele. Mungu awabariki.