Kitila Mkumbo: Ndalichako amekosea

Nilivyomuelewa Kitila anataka haya mambo yawe kwenye Katiba na sio tu mtu unaamka asubuhi unatangaza kufuta au kubadilisha jambo fulani alafu unaweka miguu juu ya meza na kutikisa kichwa Kazi imekwisha.....Nchi za Wenzetu huwezi ukabadilisha tu kila jambo kwa Utashi wako bila kuwa Na Maridhiano ya Kitaifa. Sera za Elimu zinapaswa ziwekwe kwenye Katiba.
 
Kitila angewasaidia NECTA kuandika maelezo pale walipotakiwa kueleza ni kwa nini mfumo wa GPA ni bora kuliko division na kwa nini usifutwe. Sasa yeye anasubiri matukio yatokee ili apate cha kuandika.
 
Iwe mfumo wa GPA ambao ni (unajumlisha alama na kugawanya kwa idadi ya masomo unapata wastani) au Division (unajumlisha alama) tofauti ni ndogo, karibu ni kitu kile kile ISIPOKUWA kilicho fanyika ni kupanua wigo wa wanafunzi kushinda kwa malengo ya kisiasa. Mfumo wowote unafaa ikiwa tu alama za ufaulu si chini ya asilimia 40. GPA inaanzia 0 hadi 5. Kichekesho kipo hivi eti mwanafunzi aliye pata GPA 0.1 kwamba amefaulu (PASS). Ukitafuta asilimia ya 0.1 ya 5.0 ina maana kuwa ufaulu una anzia 2%!!!! Huu in mzaha. Hitimisho ni alama za kufaulu. Kiwango cha chini cha kufaulu isiwe chini ya asilimia 40%.
 
Hivi umekisoma alicho kiandika Kitila? ni wapi wana tofautiana na Ndalichako? Anacho hitaji Kitila ni msimamo na Debate! Muulize Kitila atupe mifano ya nchi iliyo andaa Debate ili kujadili mfumo wa elimu au upangaji matokeo!

Mimi ninachojua hapa kinacho hitajika ni utafiti wa kisayansi na sio kelele za kwenye Debate!
Tafiti zilifanyika zikaona mfumo wa division ndio unafaa na kama kuna tafiti zilifanyika kuonesha GPA ndio mfumo mzuri na pia kwa kushusha marks vile basi walitakiwa wawe wametuonesha na kueleza..! Wameshindwa kuitetea GPA ndio maana tumerudi kule tulipokuwa.

Hatuhitaji Debate kwenye mambo ya msingi bali tunahitaji tafiti!
 
Ndalichako et...ra... Issue si GPA au DIVISION!! Issue ni viwango/ alama za ufaulu. Kwa uelewa mdogo tu ukipata chini ya 50% katika jambo lolote unalo lifanya umeshindwa!!!!! Sasa, acha tushushe kiwango hadi 40% basi. Vinginevyo hata kama itakuwa Division bado alama ya chini ya ufaulu ni 21% bado utakuwa hujasaidia kupandisha kiwango cha elimu Tanzania!
 
Ndalichako na serikali wawaeleze watanzana ni namna gani wataboresha au kuongeza maarifa ya watoto wao. Elimu haiboreshwi kwa mfumo wa Division au GPA!
 
Kama ungekuwa umemsikiliza vizuri Prof Ndalichako wala usinge andika haya ... aliwaagiza Necta warudishe na kupitia upya viwango vya ufaulu si kurudisha tuu Division!
 
Mkumbo hakupewa kitengo ndo maana anahangaika aonekane yupo nae akumbukwe siku za usoni. Tutawazoea tu. Mwishowe tutawapiga mawe. Anyway ni maoni yako ila hayana tija.
 
Ruta, ngoja tusubiri tuone. Utakumbuka kuwa kipindi wanaanzisha GPA serikali ilisema kwamba wameamua kutumia GPA kwa sababu ni mfumo unao tumika katika nchi nyingi duniani. Hivyo kuepuka usumbufu kwa watahiniwa wetu kufanyiwa ulinganifu wa division vs gpa wanapo taka kujiunga na elimu ya juu au kazi nje ya Tanzania.
 
Hii nchi kila mmoja anataka mawazo yake yawe sahihi

Hahahaha GPA imelalamikia sana na haohao wasomi Leo wametoa anakuja MTU kulalamika hawajafanya research hahahaha
Kama kilichopo yaani GPA hakikufanyiwa research kuna haja gani kukibadili kifanyiwe research

Sababu kubwa hapa ya Kitila ni kwamba hajashirikishwa japo kazunguka saana ila lengo kuu ni kushirikishwa
 
Wangefanya kama chuo 2.0 pass below that fail
 
Prof. Ndalichako amerejesha mfumo wa zamani uliobadilishwa bila utafiti wala ushirikishi wa wadau. Prof. Ndalichako ameirudisha wizara kwenye ground zero au back to square one ili ijipange kutafuta mfumo mpana wa kupima ufaulu wa watahiniwa katika ngazi mbali za elimu. Mfumo utakaopatika sharti utokane na utafiti ambao matokeo yake yaongoze mjadala shirikishi wa kitafa. Waziri alichokiuka ni kutoa agizo badala kanuni na kuzitangaza kwenye gazeti la serikali. It can be done retrospectively
 

Kama tafsiri ya alichokifanya Prof Ndalichako ni ku- restore system, basi tuna shida kubwa ya uelewa...
 
Je alichofanya Ndalichako kina tatizo? Kwanini tusiseme huu ndio mwanzo mzuri?
Ndalichako na serikali wawaeleze watanzana ni namna gani wataboresha au kuongeza maarifa ya watoto wao. Elimu haiboreshwi kwa mfumo wa Division au GPA!
 
Watu wanatakiwa kujua hapa ni kuwa kibaya zaidi Necta wametumia mfumo wa GPA vibaya na kushusha viwango vya ufaulu...
 
Kitila Mkumbo ni type za kina mulugo mbona walivyounganisha masomo na kuleta div 5 hakusema chochote? Professor anashabikia kutanua goli mabao yawe mengi badala ya kuwafundisha wachezaji mbinu za Ushindi.....GPA kwa secondary ni uzushi Safi Ndalichako kuroll back Division.
 
Tatizo la elimu yetu sio mfumo kutoa matokea tatizo ni ubora wa elimu inayotolewa ,nafikiri tunatakiwa kuwa na elimu ya kumuandaa mwanafunzi kujitegemea ,kujitambua na kuwa mbunifu kwa sasa tumebase sana katika kumfanya mwanafunzi ajue kuelewa 1*2 ni ngapi tumesahau vingine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…