Jana ilikuwa siku mbaya sana kwa Kitila Mkumbo ambaye ni mwanachama mwandamizi wa chama cha ACT, ikumbukwe kuwa Kitila Mkumbo kufikia jana alikuwa mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam (UDASA), Kitila amekikalia kiti hicho kwa mda mfupi sana kuliko wenyeviti wote na kuandika rekodi.
Jana UDASA walikutana kwenye kikao chao cha kawaida kama ilivyo vikao vingine ila ijulikane kuwa Bwana Kitila Mkumbo alikuwa Sabbatical Leave ila cha kushangaza wasomi hao wa UDASA ni kumuona mtu aliyekuwa kwenye leave aki chair mkutano huo wa UDASA, Ndipo hapo wasomi nguli wa sheria kutokea kitivo cha sheria cha UDSM walianza kuhoji, wakipewa sapoti na Profesa Mkandala kwa nini mtu aliye kwenye likizo aje kuongoza kikao? Nini maana ya likizo? Au ndio Unkurunziza wenyewe?
Bila aibu au adabu Bwana Kitila Mkumbo alianza kujibizana na Maprofesa hao nguli na hata kumjibu shombo Prof Mkandala hali iliyopelekea Maprofesa hao kumshambulia ipasavyo pamoja na kueleza madhaifu yake yote ya Kitaaluma na Kinidhamu, walianza kumuelezea kuwa Mojawapo ya makosa anayoyafanya kama mwenyekiti wa UDASA ni kulitumia jukwaa hilo la wasomi kujijengea umaarufu wake binafsi pamoja na kuliigeuza kuwa jopo la kisiasa badala ya kuwa jopo la Kitaaluma, walimsema kuwa amekuwa akilitumia jukwaa hilo la wasomi kueneza propaganda za chama chake cha ACT hali iliyopelekea ukumbi mzima kuzizima kwa kelele na kumtaka Ang'oke haraka sana kabla hajang'olewa kitini hapo maana hakimfai tena.
Kitila Mkumbo kwa aibu kubwa huku akiwa anatiririkwa na machozi kwa jinsi alivyoanikwa hadharani atemeshwa mzigo. Hivyo basi nawaomba mjue kuwa kufikai mda huu Ndugu Kitila Mkumbo siyo Kiongozi wa UDASA tena.
Ameingia kwenye historia ya kuwa kiongozi alietimuliwa kila sehemu anayokimbilia, alianza CHADEMA, wakamtimua, akaenda ACT akatimuliwa akarudishwa na genge lake, sasa katimuliwa tena UDASA.
Pole sana ACT, Pole sana Kitila Mkumbo.